Waziri Dr. Kigwangalla aje atolee ufafanuzi hili la Loliondo maana mwenye eneo kaja

Kwa haraka ambayo Waziri Kigwangala alitoa ile kauli ya kuondoa OBC ilikuwa wazi kuwa waziri alikurupuka. OBC ni mboni ya jicho la ccm na serikali yake. Ili kufanya uamuzi wowote unaoweza kuathiri OBC sharti kwanza ngazi za juu kabisa katika siasa na uongozi wa nchi ziridhia. Waziri alitoa kauli yake muda mfupi tu baada ya kuteuliwa hivyo hakuwa na muda wa kuifahamu kampuni yenyewe wala msimamo rasmi wa serikali yake kuhusu kampuni hiyo.
 
Aiseee

Tabu hawa wenye magazeti na TV na resio pia wao huwa wapo bizi kusubiria udaku badala ya kutuletea habari nyingi za kutuvutia sisi wananchi kufatilia..

Halafu wakitunga na kuingia kwenye matatizo wanalalamika na kulia eti uonevu..

Hawa wamebakia na Udaku umbeaumbea, analeta habari za saloon hata vyanzo alipotoa hakunaa..

Pumbavu kabisa..
 
Wana-body mtakumbuka kwamba Dr. Kigwangalla alipiga mkwara mzito sana na kutoa siku kama sio wiki au kama sio mwezi kwamba mwarabu awe ameondoka Loliondo. Zaidi soma => Waziri Kigwangalla aagiza kampuni ya Uwindaji ya OBC ya Loliondo kurudi walikotokea kabla ya Januari 2018

Ila cha kushangaza mwarabu mwenye mali ninavyoandika yuko Loliondo kaja kustarehe na kuangala mali zake.

Sasa je mpango wa Waziri Hamisi kumtimua uliishia wapi?
Unamfahamu marehemu Stan Katabalo? alikuwa mwandishi wa gazeti la zamani Mfanyakazi. Alitumia kalamu yake kuzuia isiuzwe akafa anajiona! nakumbuka hadi alipiga picha za hirizi alizotumiwa wakati wa serikali ya ruksa!! Si bure Ruksa bure kulipenda jiwe! birds of a feather once!
 
Rais Atamuondoa Mwarabu
Awamu Hii Sasa Hivi Majizi Hayana Nafasi
Mikataba Tata Kiama Chake Kimefika

Yaani Mwarabu Anapitia Wapi Hivi Haji Ikulu Dar Kuomba Ruhusa
Vipi Rais Wako alimuondoa huyo Mwarabu😁😁,naon.post Yako ilipata Like ya Dk Slaa!
 
Back
Top Bottom