Waziri Dorothy Gwajima: Wanafunzi waliojirekodi picha za utupu na kusambaza kurekebishwa tabia na kurudi shule

Waufukweni

JF-Expert Member
May 16, 2024
1,395
3,499
Wakuu sauti iliyopzwa imemfikia Waziri Dkt. Gwajima D Wanafunzi hao kurudi shule baada ya kupita kwenye programu ya marekebisho tabia.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema wanafunzi wa kike mkoani Tabora waliofukuzwa shule kwa makosa ya kujirekodi picha za utupu, watapelekwa kwenye programu ya marekebisho tabia kisha watarejeshwa katika shule nyingine. Waziri Gwajima amesema Serikali inapochukua hatua ni kwa lengo la kufanya marekebisho ya tabia na kuwalinda watoto.
1729766549071.png
"Kwa ufupi ni kuwa, hawa ni watoto chini ya miaka 18 ambapo, chini ya sheria ya mtoto watapelekwa kwenye mpango wa program ya marekebisho tabia kama wanavyopelekwa wengine wote na baada ya hapo watarejeshwa tena shuleni eneo lingine. Wito wangu ni jamii kukumbuka kuwa, sisi ni viongozi wenye dhamana na watoto wote hivyo, tunapochukua hatua ni kwa lengo la kufanya marekebisho ya tabia na kuwalinda wengine."

Waziri Gwajima ameongeza kuwa; "Naomba sasa hii taarifa nayo muisambaze vilevile. Aidha, wazazi tuendelee kukaa karibu na watoto Ili kuhakikisha wanakuwa na makuzi na malezi mema kipindi chote cha utoto wao. Ahsanteni sana kwa mjadala moto moto na Mungu awabariki."
Screenshot 2024-10-24 134128.png
Pia, Soma:
 
Wakuu sauti iliyopzwa imemfikia Waziri Dkt. Gwajima D Wanafunzi hao kurudi shule baada ya kupita kwenye programu ya marekebisho tabia.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema wanafunzi wa kike mkoani Tabora waliofukuzwa shule kwa makosa ya kujirekodi picha za utupu, watapelekwa kwenye programu ya marekebisho tabia kisha watarejeshwa katika shule nyingine. Waziri Gwajima amesema Serikali inapochukua hatua ni kwa lengo la kufanya marekebisho ya tabia na kuwalinda watoto.
"Kwa ufupi ni kuwa, hawa ni watoto chini ya miaka 18 ambapo, chini ya sheria ya mtoto watapelekwa kwenye mpango wa program ya marekebisho tabia kama wanavyopelekwa wengine wote na baada ya hapo watarejeshwa tena shuleni eneo lingine. Wito wangu ni jamii kukumbuka kuwa, sisi ni viongozi wenye dhamana na watoto wote hivyo, tunapochukua hatua ni kwa lengo la kufanya marekebisho ya tabia na kuwalinda wengine. Naomba sasa hii taarifa nayo muisambaze vilevile. Aidha, wazazi tuendelee kukaa karibu na watoto Ili kuhakikisha wanakuwa na makuzi na malezi mema kipindi chote cha utoto wao. Ahsanteni sana kwa mjadala moto moto na Mungu awabariki."
Pia, Soma:

Kuwafukuza ilikuwa too cruel.

Hongera zake Dkt. Gwajima kulisikia hilo kwa wakati.
 
Tatizo la watoto wa sasa linaanzia kwa Sisi wazazi, tupo bize sana kukimbizana kutafuta fedha kuliko kuangalia malezi. Hongera Waziri
 
Jambo jema sana hili
Hongera sana.
Mh Mkuu wa Mkoa namuona kama mtu makini sana ila sijui kwa nini aliona awafukuze hawa watoto....sijui alipatwa na nini?...
Huu ulikuwa uamuzi mbovu sana...watoto hawa wanahitaji msaada sana..hii dunia imejaa utata sana
 
Jambo jema sana hili
Hongera sana.
Mh Mkuu wa Mkoa namuona kama mtu makini sana ila sijui kwa nini aliona awafukuze hawa watoto....sijui alipatwa na nini?...
Huu ulikuwa uamuzi mbovu sana...watoto hawa wanahitaji msaada sana..hii dunia imejaa utata sana
Wakuu wengi wa mikoa ni wanasiasa wapenda kiki
 
Kwahyo kuna watu wana hizo koneksheni wanapigia ufuska...tena tupu za watoto...mhhh wazazi tuna kazi ya ziada...wale wazee wa kusambaza koneksheni mara paap umetumiwa ya mwanao...laanakum hii
 
Back
Top Bottom