Waziri Dkt. Mwigulu ataka sheria zitafsiriwe kwa lugha ya Kiswahili

Kwa maelez
Unaweza kujifanya unajua sana lakini hiyo haitaondoa ukweli wa usichokijua.

Lugha ni kielelezo cha mambo mengi. Kulazimisha kutumia Kiswahili wakati Sheria zenyewe zinafundishwa kwa Kiingereza, mfumo wenyewe wa Sheria tunaoutumia ni wa UK (jumuia ya Madola), fani nyingine zote, na mfumo wote wa sheria ni wa Kiingereza, ni kukurupuka kwa hali ya juu.

Huwezi kuwa na uhuru wa lugha kama huna uhuru wa tekinolojia na uchumi. Ukilazimisha kutumia lugha yako, unajitesa mwenyewe. Dunia imekuwa hivyo tangu enzi za Yesu. Wayahudi walikuwa na lugha yao lakini kutokana na uduni wa tekinolojia, lugha iliyokuwa inatumika kwenye mambo yote ya kitaalam ilikuwa Kigiriki. Imekuwa hivyo kwa mataifa mengi.

Ni nchi gani maskini inayotumia lugha yake ya asili? Hakuna anayekukataza lakini ukifanya hivyo, utajitesa mwenyewe.

Huyo mkurupukaji Mwigulu, anayesema sheria zote zitafsiriwe kwa Kiswahili, atatafsiri na marejeo yote ya hukumu kutoka jumuiya ya madola kwenda kwenye Kiswahili? Atawapeleka wanasheria wote masomoni ili wakapate uoanishi mzuri wa walichojifunza toka Kiingereza kwenda Kiswahili?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hoja yako hii,basi peleka mswada tuondoe kiswahili kuwa lugha ya taifa.
tunaposema kiswahili ni lugha ya taifa huku tunaendelea kutumia kiingereza tunamdanganya nani?

Mambo yote lazima kuwepo mwanzo wake,na mwanzo ni mgumu.
Mfano mzuri ni uthubutu wa mh. Rais kuihamishia ikulu mjini Dodoma.
Nimesoma habari hizi na faida za ikulu kuhamia dodoma toka nipo shule ya msingi,marais wamepita wanne hakuna aliyethubutu nadhani hofu ilikuwa kama hii ya kwako.Mmmoja amethubutu na mambo yanaenda vizuri.Tuchukulie huu mfano,kufanya na mengine.
Tuache hofu na woga wa kuthubutu,vinginevyo tuanze kufundisha kiingereza kuanzia shule za misingi.
 
Makaratasi yoote ya kupigia kura yalichapishwa kwa kiswahili lakini mliiba kura!!!

Watawala wanatumia kiswahili kubambikizia kesi feki wananchi wasio na hatia.

Nina mashaka Kama matumizi ya kiswahili pekee yanaweza kuleta HAKI

Kweli kabisa, tatizo ni kutotenda haki kwa wakati. Ni kweli sheria kuwekwa kwenye kiswahili ni jambo sahihi, lakini tatizo la msingi ni utoaji wa haki, tena utoaji wa haki kwa wakati.
 
Kiswahili nacho kinaandikwa kwa herufi za Latin, Latin alphabet ambazo zilitoka kwa Warumi. Lugha ni yetu lakini tunaiandika kwa msaada wa wazungu.
 
Kwa maelez

Kwa hoja yako hii,basi peleka mswada tuondoe kiswahili kuwa lugha ya taifa.
tunaposema kiswahili ni lugha ya taifa huku tunaendelea kutumia kiingereza tunamdanganya nani?

Mambo yote lazima kuwepo mwanzo wake,na mwanzo ni mgumu.
Mfano mzuri ni uthubutu wa mh. Rais kuihamishia ikulu mjini Dodoma.
Nimesoma habari hizi na faida za ikulu kuhamia dodoma toka nipo shule ya msingi,marais wamepita wanne hakuna aliyethubutu nadhani hofu ilikuwa kama hii ya kwako.Mmmoja amethubutu na mambo yanaenda vizuri.Tuchukulie huu mfano,kufanya na mengine.
Tuache hofu na woga wa kuthubutu,vinginevyo tuanze kufundisha kiingereza kuanzia shule za misingi.
Jamii ya Kitanzania, kwa kiasi kikubwa, imejaa unafiki mkubwa.

Huyo Mwigulu anayetaka kuonesha kuwa Swahili to the Tanzania community is above all languages, wanawe wanasoma kwenye English medium schools, na huenda hata wengi wanaotetea kuwa tufanye kila kitu kwa Kiswahili, ndio hao ambao wanataka watoto wao wasome english medium school, na wanafarijika mioyoni mwao wanapoona watoto wao wanamudu vizuri lugha ya Kiingereza.

Kama Taifa, tunahitaji kuweka msisitizo kwenye lugha ambayo inaturahisishia maisha, inatusaidia kuchangamana na Dunia kiurahisi, kujifunza tekinolojia na science kiurahisi. Kwa nchi kama Tanzania, ambayo haiwezi kutengeneza hata baiskeli, kulazimisha kila kitu kifanyike kutumia lugha ya Kiswahili ni kuwapa ugumu watu wetu wa kujifunza, ni kuwapa ugumu watu wetu wa kuchangamana na Dunia katika nyanja mbalimbali ili tuinue uchumi wetu, ni kuwapa ugumu watu wetu wa kuuzika katika soko la ajira la kimataifa.

Usijilinganishe na mataifa makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa wanajitosheleza kwa mambo mengi, na hivyo mataifa mengine kulazimika kujifunza lugha zao.

Mwalimu Nyerere alikipenda Kiswahili, aliipenda Tanzania, alipenda tujitegemee, lakini bado aliona umuhimu wa Tanzania kutumia lugha ya wakoloni wetu, siyo kwa sababu alikosa uzalendo au alitaka kuwaabudu wazungu. Leo hii kwa kufahamu vizuri Kiingereza, Kifaransa au Kispanish, umejirahisishia kupata maarifa mbalimbali yanayowakilishwa kwa kutumia lugua hizo. Kwa kufahamu lugha hizo, unakuwa umejirahishia kwa kiasi kikubwa kuwasiliana na sehemu kubwa sana ya Dunia.

Wachina sasa hivi wana programu madhubuti ya kukuza Kiingereza katika vyuo vyao, Waafrika Kusini wameweka mkazo mkubwa kwa lugha ya Kiingereza baada ya miaka mingi ya ubaguzi wa rangi ambapo mtu mweusi hakuruhusiwa kusoma kqenye shule zilizokuwa zinaendeaha masomo kwa lugha ya Kiingereza. Msumbiji lugha yao ya Taifa ni Kireno, lakini kwa sasa wameamua kuingiza somo la Kiingereza katika mitaala yao ili baadaye masomo yote yafundishwe kwa Kiingereza. Hiyo ipo kwa mataifa mengi kama vile Rwanda, Burundi, DRC, Brazil, Mexico, Switzerland, India, n.k.

Sidhani kama kwa kukipiga kisogo Kiingereza, tutafaidika na chochote, zaidi ya kupoteza.

Tutambue kuwa tangu enzi na enzi, kanuni ya utambuzi ni kuwa ni jukumu la maskini kujifunza kutoka kwa aliyefanikiwa, na ili ujifunze vizuri, ni lazima uifahamu lugha yake, desturi zake, na tabia zake nyingine.

Tanzania, mpaka leo, bado tunapewa msaada wa vitabu vya science na tekinolojia toka mataifa mengine, halafu eti tunafikiria tufanye mambo yetu yote kwa lugha ya Kiswahili!!

Kiswahili chenyewe, siyo kweli kuwa ndiyo lugha yetu asilia. Kiswahili kilikuja na biashara ya utumwa. Ndiyo maana kina maneno mengi ya kiarabu. Tuliamua tu, lugha hiyo iwe lugha ya pili rasmi ya Taifa letu baada ya Kiingereza ambacho ndiyo lugha rasmi ya kwanza. Tukaendelea kuiongezea maneno mpaka hapa tulipofikia. Kulikuwa na uwezekano wa kukitupa kiswahili kwa hoja kuwa ni lugha iliyoletwa na Waarabu.

Canada wanatumia English and French, wamepungukiwa nini? English na French, zote siyo lugha asilia za Wahindi wekundu.

Switzerland wanatumia French na Germany, zote siyo lugha zao za asili. Wamepungukiwa na nini?

US wanatumia English, wakati wao siyo Waingereza, wamepungukiwa nini?

Brazil, wanatumia Kireno, wakati wao siyo Wareno. Chile, Argentina, Mexico, Peru, n.k. wote wanatumia kihispania, wakati wao siyo wahispania, wamepungukiwa na nini?

Tunapoteza muda mwingi kwa mambo yasiyo na msaada kwa maendeleo ya Taifa, huku tukiacha yale yatakayowasaidia watu wetu kuondokana na umaskini. Mataifa mengi ya America Kusini, ambayo, yote hayatumii lugha zao za asili, yapo mbele kimaendeleo kuizidi Tanzania maradufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiswahili nacho kinaandikwa kwa herufi za Latin, Latin alphabet ambazo zilitoka kwa Warumi. Lugha ni yetu lakini tunaiandika kwa msaada wa wazungu.
God, grant me the serenity to accept the things I cannot change,
courage to change the things I can,
and wisdom to know the difference (by Reinhold).

Kutambua vitu ambavyo huwezi kubadili au ukivibadili, vitakuletea hasara, inahitaji kuwa na hekima.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamii ya Kitanzania, kwa kiasi kikubwa, imejaa unafiki mkubwa.

Huyo Mwigulu anayetaka kuonesha kuwa Swahili to the Tanzania community is above all languages, wanawe wanasoma kwenye English medium schools, na huenda hata wengi wanaotetea kuwa tufanye kila kitu kwa Kiswahili, ndio hao ambao wanataka watoto wao wasome english medium school, na wanafarijika mioyoni mwao wanapoona watoto wao wanamudu vizuri lugha ya Kiingereza.

Kama Taifa, tunahitaji kuweka msisitizo kwenye lugha ambayo inaturahisishia maisha, inatusaidia kuchangamana na Dunia kiurahisi, kujifunza tekinolojia na science kiurahisi. Kwa nchi kama Tanzania, ambayo haiwezi kutengeneza hata baiskeli, kulazimisha kila kitu kifanyike kutumia lugha ya Kiswahili ni kuwapa ugumu watu wetu wa kujifunza, ni kuwapa ugumu watu wetu wa kuchangamana na Dunia katika nyanja mbalimbali ili tuinue uchumi wetu, ni kuwapa ugumu watu wetu wa kuuzika katika soko la ajira la kimataifa.

Usijilinganishe na mataifa makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa wanajitosheleza kwa mambo mengi, na hivyo mataifa mengine kulazimika kujifunza lugha zao.

Mwalimu Nyerere alikipenda Kiswahili, aliipenda Tanzania, alipenda tujitegemee, lakini bado aliona umuhimu wa Tanzania kutumia lugha ya wakoloni wetu, siyo kwa sababu alikosa uzalendo au alitaka kuwaabudu wazungu. Leo hii kwa kufahamu vizuri Kiingereza, Kifaransa au Kispanish, umejirahisishia kupata maarifa mbalimbali yanayowakilishwa kwa kutumia lugua hizo. Kwa kufahamu lugha hizo, unakuwa umejirahishia kwa kiasi kikubwa kuwasiliana na sehemu kubwa sana ya Dunia.

Wachina sasa hivi wana programu madhubuti ya kukuza Kiingereza katika vyuo vyao, Waafrika Kusini wameweka mkazo mkubwa kwa lugha ya Kiingereza baada ya miaka mingi ya ubaguzi wa rangi ambapo mtu mweusi hakuruhusiwa kusoma kqenye shule zilizokuwa zinaendeaha masomo kwa lugha ya Kiingereza. Msumbiji lugha yao ya Taifa ni Kireno, lakini kwa sasa wameamua kuingiza somo la Kiingereza katika mitaala yao ili baadaye masomo yote yafundishwe kwa Kiingereza. Hiyo ipo kwa mataifa mengi kama vile Rwanda, Burundi, DRC, Brazil, Mexico, Switzerland, India, n.k.

Sidhani kama kwa kukipiga kisogo Kiingereza, tutafaidika na chochote, zaidi ya kupoteza.

Tutambue kuwa tangu enzi na enzi, kanuni ya utambuzi ni kuwa ni jukumu la maskini kujifunza kutoka kwa aliyefanikiwa, na ili ujifunze vizuri, ni lazima uifahamu lugha yake, desturi zake, na tabia zake nyingine.

Tanzania, mpaka leo, bado tunapewa msaada wa vitabu vya science na tekinolojia toka mataifa mengine, halafu eti tunafikiria tufanye mambo yetu yote kwa lugha ya Kiswahili!!

Kiswahili chenyewe, siyo kweli kuwa ndiyo lugha yetu asilia. Kiswahili kilikuja na biashara ya utumwa. Ndiyo maana kina maneno mengi ya kiarabu. Tuliamua tu, lugha hiyo iwe lugha ya pili rasmi ya Taifa letu baada ya Kiingereza ambacho ndiyo lugha rasmi ya kwanza. Tukaendelea kuiongezea maneno mpaka hapa tulipofikia. Kulikuwa na uwezekano wa kukitupa kiswahili kwa hoja kuwa ni lugha iliyoletwa na Waarabu.

Canada wanatumia English and French, wamepungukiwa nini? English na French, zote siyo lugha asilia za Wahindi wekundu.

Switzerland wanatumia French na Germany, zote siyo lugha zao za asili. Wamepungukiwa na nini?

US wanatumia English, wakati wao siyo Waingereza, wamepungukiwa nini?

Brazil, wanatumia Kireno, wakati wao siyo Wareno. Chile, Argentina, Mexico, Peru, n.k. wote wanatumia kihispania, wakati wao siyo wahispania, wamepungukiwa na nini?

Tunapoteza muda mwingi kwa mambo yasiyo na msaada kwa maendeleo ya Taifa, huku tukiacha yale yatakayowasaidia watu wetu kuondokana na umaskini. Mataifa mengi ya America Kusini, ambayo, yote hayatumii lugha zao za asili, yapo mbele kimaendeleo kuizidi Tanzania maradufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hapa hoja yako ni nini? unataka sheria ziendelee kuandikwa kwa kiingereza wakati mtumiaji wa hizo sheria hajui hiyo lugha?
Mimi nimeunga mkono sheria kuandikwa kiswahili ili wanaoandikiwa wajue kilichoandikwa.
Binafsi naona kuna kundi la wanufaika wa sheria kuandikwa kwa lugha ngeni,maana kundi la waliowengi ni raisi kupoteza haki zao mikononi wa wajuzi wa lugha hizo ngeni,mojawapo ni hizi sheria za kazi zinazowanufaisha waajili. Hata mambo muhimu kama malipo ya kviinua mgongo yakifutwa,hakuna anayejali maana hajui lugha mpaka atakapostaafu akajikuta amenyonywa ndo anaanza kupiga kelele
na kuishia kufa kwa presha.
Kama tunataka mabadiliko kwa kutumia lugha ya kigeni tufanye kama kenya na uganda.
lugha rasmi ya kufundishia mashuleni iwe kiingereza kuanzia shule za chekechea.N bahati nzuri waalimu wengi ni waalimu wa masomo ya sanaa ambayo kwa asilimia kubwa yanatumia lugha ya kiingereza.
hapo baada ya muda utakuta watu wote wanajua kiingereza barabara.
 
Jamii ya Kitanzania, kwa kiasi kikubwa, imejaa unafiki mkubwa.

Huyo Mwigulu anayetaka kuonesha kuwa Swahili to the Tanzania community is above all languages, wanawe wanasoma kwenye English medium schools, na huenda hata wengi wanaotetea kuwa tufanye kila kitu kwa Kiswahili, ndio hao ambao wanataka watoto wao wasome english medium school, na wanafarijika mioyoni mwao wanapoona watoto wao wanamudu vizuri lugha ya Kiingereza.

Kama Taifa, tunahitaji kuweka msisitizo kwenye lugha ambayo inaturahisishia maisha, inatusaidia kuchangamana na Dunia kiurahisi, kujifunza tekinolojia na science kiurahisi. Kwa nchi kama Tanzania, ambayo haiwezi kutengeneza hata baiskeli, kulazimisha kila kitu kifanyike kutumia lugha ya Kiswahili ni kuwapa ugumu watu wetu wa kujifunza, ni kuwapa ugumu watu wetu wa kuchangamana na Dunia katika nyanja mbalimbali ili tuinue uchumi wetu, ni kuwapa ugumu watu wetu wa kuuzika katika soko la ajira la kimataifa.

Usijilinganishe na mataifa makubwa ambayo kwa kiasi kikubwa wanajitosheleza kwa mambo mengi, na hivyo mataifa mengine kulazimika kujifunza lugha zao.

Mwalimu Nyerere alikipenda Kiswahili, aliipenda Tanzania, alipenda tujitegemee, lakini bado aliona umuhimu wa Tanzania kutumia lugha ya wakoloni wetu, siyo kwa sababu alikosa uzalendo au alitaka kuwaabudu wazungu. Leo hii kwa kufahamu vizuri Kiingereza, Kifaransa au Kispanish, umejirahisishia kupata maarifa mbalimbali yanayowakilishwa kwa kutumia lugua hizo. Kwa kufahamu lugha hizo, unakuwa umejirahishia kwa kiasi kikubwa kuwasiliana na sehemu kubwa sana ya Dunia.

Wachina sasa hivi wana programu madhubuti ya kukuza Kiingereza katika vyuo vyao, Waafrika Kusini wameweka mkazo mkubwa kwa lugha ya Kiingereza baada ya miaka mingi ya ubaguzi wa rangi ambapo mtu mweusi hakuruhusiwa kusoma kqenye shule zilizokuwa zinaendeaha masomo kwa lugha ya Kiingereza. Msumbiji lugha yao ya Taifa ni Kireno, lakini kwa sasa wameamua kuingiza somo la Kiingereza katika mitaala yao ili baadaye masomo yote yafundishwe kwa Kiingereza. Hiyo ipo kwa mataifa mengi kama vile Rwanda, Burundi, DRC, Brazil, Mexico, Switzerland, India, n.k.

Sidhani kama kwa kukipiga kisogo Kiingereza, tutafaidika na chochote, zaidi ya kupoteza.

Tutambue kuwa tangu enzi na enzi, kanuni ya utambuzi ni kuwa ni jukumu la maskini kujifunza kutoka kwa aliyefanikiwa, na ili ujifunze vizuri, ni lazima uifahamu lugha yake, desturi zake, na tabia zake nyingine.

Tanzania, mpaka leo, bado tunapewa msaada wa vitabu vya science na tekinolojia toka mataifa mengine, halafu eti tunafikiria tufanye mambo yetu yote kwa lugha ya Kiswahili!!

Kiswahili chenyewe, siyo kweli kuwa ndiyo lugha yetu asilia. Kiswahili kilikuja na biashara ya utumwa. Ndiyo maana kina maneno mengi ya kiarabu. Tuliamua tu, lugha hiyo iwe lugha ya pili rasmi ya Taifa letu baada ya Kiingereza ambacho ndiyo lugha rasmi ya kwanza. Tukaendelea kuiongezea maneno mpaka hapa tulipofikia. Kulikuwa na uwezekano wa kukitupa kiswahili kwa hoja kuwa ni lugha iliyoletwa na Waarabu.

Canada wanatumia English and French, wamepungukiwa nini? English na French, zote siyo lugha asilia za Wahindi wekundu.

Switzerland wanatumia French na Germany, zote siyo lugha zao za asili. Wamepungukiwa na nini?

US wanatumia English, wakati wao siyo Waingereza, wamepungukiwa nini?

Brazil, wanatumia Kireno, wakati wao siyo Wareno. Chile, Argentina, Mexico, Peru, n.k. wote wanatumia kihispania, wakati wao siyo wahispania, wamepungukiwa na nini?

Tunapoteza muda mwingi kwa mambo yasiyo na msaada kwa maendeleo ya Taifa, huku tukiacha yale yatakayowasaidia watu wetu kuondokana na umaskini. Mataifa mengi ya America Kusini, ambayo, yote hayatumii lugha zao za asili, yapo mbele kimaendeleo kuizidi Tanzania maradufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
huu ni utumwa wa fikira, inaonekana ulikuwa unanufaika sana na mfumo wa ukoloni mambo leo lkn bahati nzuri mfumo huo wa ukoloni mambo leo ndio mwisho wake ktk awamu hii ya 5,
kiswahili chetu tunu yetu.
kiswahili chetu kielelezo chetu.
kiswahili chetu uzalendo wetu.
TUMIA KISWAHILI KTK SHUGHULI ZOTE ZA UTOAJI HAKI KWA MASILAHI YA WATANZANIA.
 
usipo enzi lugha yako iko siku tutatumia lugha hata lugha ya kiarabu ktk shughuli za serikali kwa sababu tu eti kiarabu pia ni lugha ya kimataifa. Usipo kuwa na msimamo na kitu chako ukubali kuendeshwa kama gari bovu.
Lugha ya Taifa ni kielelezo cha utamaduni wa taifa letu na ni uthibitisho wa uzalendo.

kiswahili ni lugha pekee inayo kuwa kwa kasi sana...inazungumzwa na zIdi ya mataifa 10, mfano, Kenya, Burundi, Uganda, DRC Kongo, Rwanda, Malawi, Zambia, Djibuti, Somalia, Sudani, comoro, shelisheli n.k
Usikidharau kiswahili...na bado kila kukicha kinazidi kusambaaa kila kona ya dunia, nawashangaa sana wale wanao beza matumizi ya kiswahili ktk utoaji wa haki ktk mahakama zetu, Bunge n.k, wanao pinga wana maslahi binafsi na wabia wao mabeberu.
Kuzungumza Kiswahili siyo uzalendo uzalendo ni matendo ya haki kwa raia wako na siyo ubaguzi wa wazi kwa baadhi ya watu,taasisi nk.Mbona nchi za Afrika ya Kaskazini wanaongea Kiarabu na maisha yanasonga na wako vizuri tu,sema katika lugha yako unayojivunia ni kitu ulibuni kwenye hiyo lugha kama siyo waarabu ungeongea hicho Kiswahili?
 
Kuzungumza Kiswahili siyo uzalendo uzalendo ni matendo ya haki kwa raia wako na siyo ubaguzi wa wazi kwa baadhi ya watu,taasisi nk.Mbona nchi za Afrika ya Kaskazini wanaongea Kiarabu na maisha yanasonga na wako vizuri tu,sema katika lugha yako unayojivunia ni kitu ulibuni kwenye hiyo lugha kama siyo waarabu ungeongea hicho Kiswahili?
Bila Baba wa Taifa leo hii watanzania tungekuwa tunazungumza kikabila, lkn leo hii Afrika mashariki na kati tumeunganishwa na lugha ya kiswahili na kinaendelea kuenea kwa kasi ktk mataifa mbali mbali duniani, Ajabu kwa mtanzania wa kweli kukibeza na kukidharau kiswahili,
 
Bila Baba wa Taifa leo hii watanzania tungekuwa tunazungumza kikabila, lkn leo hii Afrika mashariki na kati tumeunganishwa na lugha ya kiswahili na kinaendelea kuenea kwa kasi ktk mataifa mbali mbali duniani, Ajabu kwa mtanzania wa kweli kukibeza na kukidharau kiswahili,
Baba wa Taifa au naye alijifunza kiswahili kutoka kwa wakoloni na kukiimarisha zaidi kwa ajili ya mawasiliano na waafrika wenzie Kiswahili hakikushuka mbinguni bali ni zao la waarabu na watu wa pwani.
 
Mhe. waziri wananchi wanataka Hukumu zao ziandikwe kwa lugha yao ya kiswahili sio watafsiriwe, kwani Hukumu zinapo andikwa kwa kingereza anaandikiwa nani? wakati sisi sote ni waswahili? anaye andika ni mswahili anaye andikiwa ni mswahili sasa kunaulizima gani iandikwe kwa kiingereza halafu nitagsiriwe? hiyo sio haki kabisa!
kuna wakati unatoa ushahidi kwa lugha ya kiswahili ghafla unakuta kilicho andikwa ni kiingereza hivyo unashindwa kuelewa kama kilicho andikwa ndicho ulicho kisema.
Watanzania wanataka lugha yao ya kiswahili itumike mwanzo mwisho hatutaki kuchanganyiwa.
 
Back
Top Bottom