Waziri Bashungwa awataka wamiliki wa redio kulipia muziki wanaopiga

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,811
4,533
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa amewataka wamiliki wa vyombo vya habari Tanzania kuhakikisha wanalipa tozo za muziki unaopigwa katika redio zao ili kuwawezesha wasanii kupata haki zao.

Bashungwa amesema hayo jana Ijumaa Septemba 3, 2021 wakati akizinduzi kituo kipya cha redio cha Gold FM mjini Kahama, akibainisha kuwa wasanii wanaingia gharama kubwa kutayarisha muziki lakini wanapata ujira mdogo.

Amesema, kila mmiliki wa redio hapa nchini anatakiwa kulipa kiasi cha Sh62,500 kwa mwezi bila kusukumwa na anaruhusiwa kupiga wimbo wowote ulioimbwa na wasanii wa Tanzania na kufanya hivyo ni kuwawezesha wasanii hao kupata ujira wao.

Bashungwa amesema, Serikali ni wakala wa ukusanyaji wa tozo hizo hivyo kile kinachokusanywa kila mwezi kupitia kazi za wanamuziki zinazopigwa redioni kinawasilishwa katika chama kinachosimamia haki za wasaniii (Kosota).

Pia Bashungwa amesema, Serikali imefuta tozo za kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram, YouTube na Facebook kwa watu ambao hawafanyi maudhui ya kihabari hivyo wajasirimali wanaruhusiwa kutangaza biashara zao kupitia mitandao hiyo.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda ya ziwa Francis Mihayo amesema, tozo hizo zipo kisheria na gharama zake, hivyo lazima wamiliki waweze kuzilipa fedha hizo kwani haziingii serikalini bali zinakwenda kuwalipa wale wanamuziki ambao wameshiriki katika kuimba nyimbo hizo.

Mihayo amesema, Kanda ya Ziwa kuna redio 39, ambapo Mkoa wa Mwanza pekee una Redio 15, Kagera radio 12, Shinyanga Radio tano, huku Gold Fm kikiwa kituo cha sita baada ya kufungukiwa na kwamba vituo hivyo vikilipa tozo hizo kutawanyanyua wasanii.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Festo Kiswaga amesema, atahakikisha anasimamia tozo hizo zinatolewa kwa wakati ili kuondoa migogoro isiyokuwa na tija baina ya wamiliki wa redio hizo na serikali na hakikisha wasanii wananufaika na uwepo wa radio zilizopo.
 
Hao wasanii idadi yao ni ngapi? je kama nyimbo yangu haikupgwa kbs ktk mwwz huo je nitalipwa?kma msanii nymbo zake zimepgwa mara chache tu je atalipwa sawa na yule wa zilzopigwa nying?
 
OK waweke utaratibu mzuri wa kuwalipa hao wasanii, ila nimeshangaa Waziri kutaja idadi wa redio peke yake kwa kanda ya ziwa bila kutaja na idadi ya wasanii waliopo upande huo, ni muhimu sana kupata takwimu sahihi na namna bora ya kuwapatia makusanyo hayo.

N. B. Serikali isipokuwa makini kwenye hizi tozo za vituo vya redio, wanakoelekea ni kuua kabisa mziki wa Tanzania, maana nyimbo nyingi sasa zitakazopigwa ni za nje ya Tanzania 🇹🇿. Hii kitu imeua mziki wa Kenya
 
Wanafanya hivyo wakiamini kuwa wanaboresha muziki kumbe wanauua taratibu. Muziki wa dansi umekufa na sasa mnarudi kuua muziki wa hawa vijana.

Wasanii wengi huimba wakitarajia ngoma zao zipigwe katika media mbalimbali pamoja na kupata airtime kwa ajili ya kazi zao.

Acheni vyombo vya habari vipige nyimbo za wasanii wa hapa nchini bila masharti yoyote. Wasanii wangapi watakaa kutegemea hivyo vitozo badala ya kujikita kutafuta collabo na kuupandisha muziki nje ya Tanzania.
 
Biashara ili iwe endelevu kuna kitu kinaitwa tripple "P"
1-P=product
2-P=People
3-p=puplication
Mziki bila kutangazwa watu wataujuaje ili waununue?
Nitangazie wimbo wangu kisha unilipe.,
 
Mpango ni mzuri lakini hata kama utatekelezwa sidhani kama utakuwa na tija kwa Wasanii kiasi kwamba Msanii atatamani Wimbo wake uchezwe bure kuliko hata uchezwe ili alipwe.

Pili kuna nafasi kubwa ya vituo vya redio kufanya upendeleo au rushwa kuchukuwa nafasi, kama tunavyoona kwa wanachokiita "top 10 au top twenty"...hivi nani huwa anaziamini hizo chaguzi zao za top ten/twenty?....Wabongo tunajijua bana.
 
Hii itapelekea muziki wa ndasi usipigwe na badala yake wa nje utapaa zaidi.
 
Hiv uwa wanaangalia vigezo gan kuteua mawaziri hasa wa sekta kama hizi? Sasa mmiliki wa kituo akishindwa kuilipa hiyo ela inamaana hatoruhusiwa kupiga nyimbo za bongo? Je nan atahathirika kwa hatua hyo mwenye kituo ama msanii?

Ebu wakajifikilie tena kwa huo utaratibu wao
 
Sasa kuna dalili za wasanii akanza kuombwa ela na wamiliki wa vituo vya radio ila nyimbo zao zichezwe
 
Kama ni nyimbo zitapigwa za wasanii wa nje.
Nadhani wakija kudai malipo yao itakuwa poa maana nyimbo zao zimevuka borders kutufikia.

Malipo yanaanzia kwenye kununua bando na kupakua mtandaoni. Mbona kila siku wanashindana kupata viewers, au hailipi?
 
Wanunuzi wakubwa wa hizo nyimbo ni wapenzi wa mziki nao huzinunua baada ya kuzisikia redioni. Radio kuzipiga nyimbo na hasa mpya, ni kuzitangaza. Watunzi wanalipia?
 
Back
Top Bottom