Waziri Bashe tusaidie, ASA wametudhulumu fedha wakulima

TENGEFU

Senior Member
Jan 25, 2017
138
206
Sisi ni wakulima tunaozalisha kwa mkataba kwa makubaliano na wakala wa mbegu za serikali yaani agricultural seed agency (ASA) yenye makao yake mjini Morogoro na matawi mikoani. Msimu wa kilimo wa mwaka 2021 tulifanikiwa kuzalisha mbegu na kuwauzia ASA kwa mujibu wa mkataba. Katika hali ya kawaida tulitakiwa kuwa tumelipwa hela zetu by December 2021.

Ilipofika November 2021 wakulima wote baada ya kukabidhi mbegu tuliandika barua ya kuomba malipo kama ilivyo kawaida. Leo ni mwishoni mwa January 2022 ASA wamenyamaza kimya na hawataki kutulipa malipo yetu ya mamilioni ya shilingi. Tunapofuatilia kwa maafisa wakuu akiwemo mkurugenzi wa Uzalishaji Dr. Justin Ringo na engineer Sumuni wanatupa majibu ya mitaani mfano. Hela itawekwa tu. Tunapofuatilia malipo kwa simu hawa hawa akina Ringo na Sumuni wamekuwa hawapokei wala kujibu simu zetu na hawaleti mrejesho ni kwa nini hatupewi fedha zetu.

Wengi wetu tumekopa hadi Milioni 20 kupata mkopo wa kuzalisha kwa ajili ya ASA na tumeanza kuuza baadhi ya mali zetu kulipa madeni kwa sababu tulitegemea malipo ya kazi yetu yangetuwezesha kulipa madeni.

Mh Bashe naomba utusaidie ili tuweze kulipwa hela zetu na hii taasisi ambayo ni ya serikali

NB: Msimu wa kilimo unaanza maeneo mengi na ni hakika sisi tunaozalisha kwa ajili ya ASA ni dhahiri hatutaweza kuingia mkataba maana mtaji wetu umeshikiliwa na hawa ASA bila maelezo yoyote.

Tafadhali tusaidieni ili turudi tena kuzalisha

NB: ASA ni taasisi ya serikali iliyoko ndani ya Wizara ya Kilimo na makao yake makuu ni Morogoro
 
Je serikali inayohamasisha secta binafsi inaweza ikaruhusu haya mambo kwenye taasisi yake kudhulumu walipa kodi wake
 
Nini kimetokea ASA mbona wanakatisha tamaa wakulima
Nimevumilia, nimefuatilia, nimedanganywa na hao hao ma Dokta wa ASA lakini hadi sas hamna malipo na hawataki kuelewa kuwa tumekopa hela
 
Kitu kibaya zaidi ASA hawasemi kwa nini hawatulipi fedha zetu
 
Hii ni sabotage kufifisha juhudi za sekta binafsi kushirikiana na serikali
 
Watu binafsi wametumia mitaji yao kuzalisha lakini taasisi ya serikali inawadhulumu?
 
Hii haina tofauti na hosegirl kunywa maziwa ya mtoto. Serikali inatakiwa iwashughulikie viongozi wa ASA na ikiwezekana iwaondoe
 
Tuliingia kufanya kazi na serikali tukijua hakuna ubabaishaji kabisa lakini ninachokiona hapa ni maafisa waliowekwa kusimamia hii Taasisi wakitoa majibu ya kihuni kwa wakulima(wawekezaji) bila kueleza kwa nini mpaka sasa wakulima hawalipwi ili hali walishachukua mbegu
 
Kinahoutuuma kwanini hawatuambii tatizo ni kitu gani wamebakia kunyamaza kimya kihuni?
 
Move ya serikali ni kuhamasisha kilimo kwa kutumia mbegeu bora . Na kama hii imetokea ni kweli wapo watu waliopewa dhamana na serikali kusimamia huu mchakato lakini kwa hili ni dhahiri wanafanya hujuma kwa maslahi yao binafsi
 
Nimeulizia nimeambiwa serikali ime inject hela nyingi ASA kwa ajili ya ku promote utumiaji wa mbegu bora. fedha hizi pia zilitakiwa zinunue mbegu wanazozalisha wakulima walioko katika mkataba na ASA. Kama wakulima wazalishaji hawajalipwa hadi leo kuna tatizo katika uongozi wa ngazi ya juu wa ASA.
 
Kama maafisa tena wenye PhD wanapigiwa simu hawatoi official statement huo ni uhuni na wanatakiwa wawajibishwe maana hili suala kuja huku limewafika shingoni wahusika
 
Tuliingia kufanya kazi na serikali tukijua hakuna ubabaishaji kabisa lakini ninachokiona hapa ni maafisa waliowekwa kusimamia hii Taasisi wakitoa majibu ya kihuni kwa wakulima(wawekezaji) bila kueleza kwa nini mpaka sasa wakulima hawalipwi ili hali walishachukua mbegu
Mkuu nenda kule Instagram kaandike ujumbe kisha mtag plus kama watumia twitter. Au nikupe namba ya mmoja wa mawaziri kisha muombe namba ya Bashe.
 
Back
Top Bottom