Waziri Bashe: Hatujapokea taarifa rasmi kutoka Kenya kuhusu kuzuiwa mahindi yetu ila magari yetu yamezuiwa!

Hatua stahiki ni kuhakikisha kuwa mazao yetu hayana sumu. Tunatakiwa kuwashukuru wakenya maana hayo mahindi hata sisi tunauziwa. Serikali inatakiwa kuanzisha utaratibu wa ku monitor mazao yetu kabla hayajaingia kwenye masoko ya ndani na nje. Hii sio mara ya kwanza kugundua kuwa watu wako tayari kuhatarisha maisha ya wenzao kwa tamaa za faida ya haraka haraka. Kuku wanalishwa dawa za ajabu ili wawe wakubwa, pombe zinachanganywa na uchafu wa kila namna ili zivutie wateja, samaki kuvuliwa kwa sumu na baruti n.k.

Hii tabia ya kila wakati kujiona sisi ni victims inatugharimu sana.

Amandla....
Asante. Umeelezea vizuri sana. Lakini utawala wa sasa hawana weledi kama huu. Sana sana utasikia wamezuia ndege au bidhaa za Kenya.
 
Badala ya kuwasiliana na waziri mwenzake kwa upande wa Kenya anatuletea habari hizi.

Sasa anaposema hawajapokea taarifa rasmi inatusaidia nini sisi Watanzania?

..Nia yetu ni kuuza mahindi Kenya na Waziri hatakiwi kuzubaa-zubaa ktk kulipatia ufumbuzi suala hili.
Atakuwa hana namba za simu za Wazuri mwenzie
 
Bashe unasubiri taarifa gani mkuu? Wakenya kuwakomesha inapaswa kuwatandika kipigo ambacho watokaa tena kutuchokoza.
 
..time is money. muda aliotumia kupiga blah-blah angeweza kuwasiliana na mamlaka za Kenya na kulipatia uvumbuzi suala hili.

Protocol haimpi ruhusa ya kuisemea inchi/serikali yetu moja kwa moja nje ya mipaka(.
 
Protocol haimpi ruhusa ya kuisemea inchi/serikali yetu moja kwa moja nje ya mipaka(.

..hatakiwi kusema-sema mbele ya camera za waandishi wa habari.

..anatakiwa aanzishe majadiliano/mazungumzo itakayopelekea mahindi ya Tz kuendelea kuuzwa Kenya.

..time is money.
 
Sijui tunakwama wapi!! Mahindi yanapimwa na shirika na viwango KEBS hapo hapo mpakani. Yakikutwa na unyevunyevu hayaruhusiwi kuingia! Hakuna ban ya kuingiza mahindi so waziri mdogo atasubiri sana na hatasikia chochote!!

Tunapenda sana kulazimisha mambo. Kama tulivokuwa tunataka madereva wetu wasipimwe korona na waingie wakati hata wakenye wanaoingia tu wanapimwa!!

Tukaushe mahindi!!
 
Dogo[bashe] anaenda kutembelea mpaka wa namanga, badala ya kuwasiliana na viongozi wenzake kwa upande wa Kenya.

Ndio hapo sasa
Sa sijui wale madereva ndio wana mamlaka au! Tunataka watu wa kupiga kazi kutupa matokeo sio waziri naye hajui eti hajaambiwa acha akae hivyo hivyo
 
Badala ya kuwasiliana na waziri mwenzake kwa upande wa Kenya anatuletea habari hizi.

Sasa anaposema hawajapokea taarifa rasmi inatusaidia nini sisi Watanzania?

..Nia yetu ni kuuza mahindi Kenya na Waziri hatakiwi kuzubaa-zubaa ktk kulipatia ufumbuzi suala hili.
Akili ni mali ..... ......
 
Watanzania tumejengewa dhana zo hovyo sana,na hii kwasababu
hatuna exposure na hatupendi kusoma ,yani huwa tunadhani tulivyonavyo sisi wengine hawana na kama wanavyo basi vyakwetu ni bora na vingi zaidi ukilinganisha na kokote duniani.

Ukweli ni kwamba tuko kawaida Sana tusiji over rate.Madini kama dhahabu tulionayo huwezi linganisha hata kwa robo na dhahabu ya south Africa.

Gas hii tulionayo ifahamike Urusi ni miongoni mwa nchi zilizobarikiwa gas nyingi duniani.

Sasa unajigamba habari ya mahindi ambayo mmarekani ndio mkulima no moja wa mahindi duniani na huyalima kwaajili ya mifugo.

Tuache ubabe wakijinga kwani kwakufanya hivyo tunaumiza sana wakulima.
Mkuu kabla ya mitandao na Tv za kuyajua hayo unayosema, tulilishwa nyimbo tulizoambiwa ni za kizalendo zenye kusifia neema ya nchi...tukajua sisi ndio namba moja duniani.
 
Watanzania mnaoshabikia Kenya si muhame, muende uko Kenya mnayoishabikia.
Hameni mtuondokee msitujazie nchi, tunaonekana weengi kumbe mengine ni matahiira tu mashabiki ya Kenya.
 
Aliyekupa amekupa tu hata mkitia kila aina ya figisu hamtaweza kwa sababu aliyetubariki ni Mungu mwenyewe

Tuna madini
Tuna ardhi nzuri na tunalima sana tu
Tuna vivutio vya utalii kama vyote
Mungu ametuweka kijiografia kwenye eneo nzuri kuwahudumia nchi zilizoko mbali na bahari
Yaani sijui niseme nini
RAISI MAKINI TUNAE

Hebu mtuheshimu tu hizi figisu hazisaidii jamani ni Mungu huyu ambaye ametupatia vitu vyote hivyo
Lakini kimaendeleo Kenya imewapita, mnakwama wapi au mlinyimwa akili?
 
Back
Top Bottom