Waziri azifunga leseni za Madereva wa Mabasi 10 kwa kuendesha speed 125 kwa saa. Aagiza washtakiwe

Ifike mahali tujue kwamba tunahitaji barabara mpya sio mara ya kwanza kusikia dereva wanafungiwa leseni, lakini bado ajali zipo.
Barabara zetu zimetengenezwa kurusuhu gari kutoka point A kufika B kwa mwendo ambao hauzidi 80km/hr
Haya magari huko duniani wanapotengeneza yanaletwa na speed zaidi ya 80 hivo kutokana na kwao kua na miundombinu bora wanadhani na kwetu ni hivo hivo

Either serikali itoe order magari ya kuja tanzania yawe na speed mwisho 80 au ni wakati wa kufikiria kuanza kutengeneza barabara mpya kuepusha mambo ya ajali na bus kuvuka speed elekezi
 
Nikuulize
Kwani Magari yao ni ya abiria? We pimbi kweli! Sheria ya usalama imeelekeza magari ya abiria speed mwisho 80km na ambayo siyo ya abilia yanaruhusiwa kuzidisha ambapo siyo makazi!

Waziri kasimamia sheria siyo maoni yake
Nikuulize, kama kisheria speed mwisho 80km/hr mfano dar Arusha ni almost 600km then ukigawa hapo unapata masaa 7.5 ikimaanisha ukitoka dar saa 12asubuh unapaswa ufike saa 8 mchana jijin Arusha. Kwann magari bado yanazuiliwa kufika mda huo mpaka at least ifike saa 10 jion na kuendelea? Hili likoje? Ufafanuzi tafadhali
 
Nikuulize

Nikuulize, kama kisheria speed mwisho 80km/hr mfano dar Arusha ni almost 600km then ukigawa hapo unapata masaa 7.5 ikimaanisha ukitoka dar saa 12asubuh unapaswa ufike saa 8 mchana jijin Arusha. Kwann magari bado yanazuiliwa kufika mda huo mpaka at least ifike saa 10 jion na kuendelea? Hili likoje? Ufafanuzi tafadhali
Hiyo speed 80km utaenda kama risasi, hakuna matuta, hakuna kona, hauchimbi dawa au unamaanisha utapaa kama ndege?
Mda huo ulifanyiwa uchunguzi kwa kuzingatia hayo kwanza kuwa muelewa
 
Hiyo speed 80km utaenda kama risasi, hakuna matuta, hakuna kona, hauchimbi dawa au unamaanisha utapaa kama ndege?
Mda huo ulifanyiwa uchunguzi kwa kuzingatia hayo kwanza kuwa muelewa
Issue ya speed 80km/ hr utaenda kama risas au la sio hoja ya msingi ndugu, jiulize je sheria hiyo iliwekwa na wahusika wakat barabara hazikua na bumps? Issue ya kuchimba sio hoja ya utetez wako cz uchimbaji dawa upo kweny utaratib wa kupita hotelin kula na kuchimba dawa. Kwa hoja yako hapo juu ndugu siwez kua muelewa mpaka unijib hili swal
 
Ik
Issue ya speed 80km/ hr utaenda kama risas au la sio hoja ya msingi ndugu, jiulize je sheria hiyo iliwekwa na wahusika wakat barabara hazikua na bumps? Issue ya kuchimba sio hoja ya utetez wako cz uchimbaji dawa upo kweny utaratib wa kupita hotelin kula na kuchimba dawa. Kwa hoja yako hapo juu ndugu siwez kua muelewa mpaka unijib hili swal
Nikujibu nini sasa! Nimekwambia hiyo speed 80km huwezi itembelea constant kama risas, kuna maeneo utatakiwa utembee 50km au 30km,
Ndiyo mabasi wakapewa kitabu ili wasiwahi kufika kabla ya huo mda ili kuwa discourage wasione umhimu wa kwenda mbio!
 
Safi sana. Ajali isikie kwa mwenzio, Siku ukipoteza mpendwa wako wa karibu ndio utajua umuhimu wa kuwajibisha madereva wanaokiuka sheria.

Ajali zembe zinazuilika.
 
Watanzania hatuwezi kiendelea lwa ub standards hizi, kuna mabasi yanajulikana kwa kiendeshwa ovyo na kukimbia zaidi ya spidi ilitowekwa kisheria na hayafuati wala kujali alama za barabarani lakini kwenye hiyo orodha ya waziri hayapo, hiyo ni joke. Mabasi kma Sauli, Allys na Kisbo yalipaswa kuwemo kwenye hiyo orodha
 
Watanzania hatuwezi kiendelea lwa ub standards hizi, kuna mabasi yanajulikana kwa kiendeshwa ovyo na kukimbia zaidi ya spidi ilitowekwa kisheria na hayafuati wala kujali alama za barabarani lakini kwenye hiyo orodha ya waziri hayapo, hiyo ni joke. Mabasi kma Sauli, Allys na Kisbo yalipaswa kuwemo kwenye hiyo orodha
Tatizo ni madereva na si mabasi. Dereva ndiye anayeendesha gari kwa mwendokasi. Ndio maana nyundo imeangukia kwao.
 
Safi sana ndugu Waziri mwenye dhamana ya usalama barabarani.

Hii imekaa vizuri . Tena iwe endelevu kama ulivyosema.

Kazeni buti.
 
Sheria za barabarani zinaruhusu speed kiasi gani kwa mabasi ya abiria? Maana lazima kutii sheria bila shurti. Ajari nyingi zimekuwa na madhara makubwa kwa watu na mali pia. Hawa madereva wengi akili zao ziko kwenye sehemu isiyojulikana
 
Wanajifanya wanapenda wananchi huku magari yao yakienda zaidi ya speed 200 KPH
Kuna mabasi yanamilikiwa na mzito mmoja wa TCRA yanakwenda mwendo hatari na king'amuzi kinasoma yameoverspeed lakini hayakamatwi, naona double standards
 
Tena hawa kuna wakati walipewa onyo maybe wamejirekebisha
Waziri kasema hawa ni sugu. Pamoja na kuonywa mara kadhaa, na kupigwa faini, wamekuwa wakaidi. Ndio maana wamefikia maamuzi hayo.
 
Kwani Magari yao ni ya abiria? We pimbi kweli! Sheria ya usalama imeelekeza magari ya abiria speed mwisho 80km na ambayo siyo ya abilia yanaruhusiwa kuzidisha ambapo siyo makazi!

Waziri kasimamia sheria siyo maoni yake
Wow! kumbe tuna sheria nzuri kabisa,tatizo kuzisimamia,hao sio kufungiwa wasiruhusiwe tena kuendesha magari ya abiria mabasi
 
Kuendesha 125km/h sio tatizo . Tatizo haswa ni:

1. Je barabara zetu zina ubora wa kuhimiri hiyo speed ya 125
2. Je vyombo kama mabasi hayo viko roadworthy kuwepo barabarani?
3. Je kuna vifaa gani zaidi ya vitochi vya polisi vinavo zuia watu kuendesha mwendo hatarishi?

Ni nini serikali inafanya ili kuwawezesha madereza kutii sheria barabari, speed governors hazitoshi, vipi kuhusu traffic speed camera -Kwa nini zisifungwe huko barabarani? driving licences kuwa na points kwa kila kosa kabla ya kuwa revoked?

Waziri hawezi tu kuwafungia watu kufanya kazi maana watashindwa kuishi, na Judge makini hawezi kuwa- deprive haki yao ya kuishi kwa kukosa kazi au kipato na atawapa adhabu mbadara na wataendelea na kazi yao ya kuendesha mabasi. Kosa ni kwa serikali kutoweka namna bora ya kuzuia mwendo hatarishi kwa kuweka vifaa vinavyo wafanya watu wajue kwamba ni hatari- mfano- compursory awareness course kwa madreva wa mabasi kila mwaka, kufunga average speed cameras huko mabarabarani ( sio vitochi), kuhakikisha road worthiness ya vyombo na ubora wa njia za magari na mambo mengineyo ambayo wenzetu wanafanya huko duniani.
Mbona unachanga madesa? Kuendesha 125km/h siyo tatizo wakati hapo hapo unahoji kama barabara zetu zinahimili? Wewe unaona zinahimili?
 
Hili jambo limetokeaje kama tunaambiwa mabasi yote yako na speed governor kufikia 80kph??

Kama wameharibu hivyo vifaa basi wanaweza kushtakiwa. Kama mabasi hayo hayakuwa na hivyo vifaa, mwenye mabasi ashtakiwe na kulipishwa faini.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom