:A S-baby:Kwa mdomo wako wewe mwenyewe na bwebwe nyingi uliongelea kwa kirefu matatizo yanayoikabili TTCL na ulitamka bila kusita kuwa uongozi unachangia na ukawataja kwa vyeo nafasi mbili ndani ya TTCL ambazo ni tatizo kwa TTCL kusonga mbele na AHADI yako ya kwanza kwa wana TTCL katika mikoa karibia yote uliyotembelea ilikuwa kuwapatia CEO mpya kabla ya April walichosahau kuuliza na wewe ukasahau kutamka ni mwaka gani;April imepita mpaka leo Desemba bado kimya, Hakika umewasaliti wana TTCL.Kijana January Makamba mkumbushe ahadi aliyotoa na mwambie kuwa TTCL kuendelea kuongozwa na viongozi wasiofaa inazidi kudidima.:israel:
[h=3]Makamba afumua menejimenti TTCL[/h]
Na Mariam Mziwanda
NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameahidi kufumua uongozi uliopo katika Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kutokana na shutuma za ubadhirifu yakiwemo matumizi mabaya ya uongozi.
Makamba aliyasema hayo Dar es Salaam jana mara baada ya kupokea ripoti kutoka kwa wafanyakazi wa shirika hilo zilizoeleza vitendo viovu vinavyofanywa na viongozi wa shirika katika kuhujumu mali za umma.
Alisema kuwa, mbali na mikakati ya Serikali iliyopo kulipatia viongozi madhubuti shirika hilo pia amewasiliana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kuwachukulia hatua viongozi wanaohusika na ubadhirifu huo.
"Mimi kama raia na kiongozi nimetoa taarifa TAKUKURU tayari, imekua bahati kwangu leo nimepokea ripoti za wafanyakazi ambazo zina vielelezo vya kutosha juu ya tuhuma za viongozi ambao ni wabadhirifu na wana matumizi mabaya ya uongozi hii itarahisisha zaidi uchunguzi na sheria kuweza kutumika,"alisema.
Aliongeza kuwa, juhudi hizo zitakwenda sambamba na kuhakikisha hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamni viongozi hao zinafikiwa hivyo amewataka wafanyakazi wengine wenye vielelezo waunge mkono kwa maslahi ya taifa.
Makamba alidai kusikitishwa na udhaifu wa uongozi uliopo katika shirika hilo ambao unajieleza kuwa hakuna heshima wala staha ya shirika hivyo kufananisha mfumo wa kazi baina ya viongozi na watumishi kuwa sawa na makuli bandarini.
Alisema, Serikali ina wajibu wa kuona shirika hilo linarudi katika mfumo bora wa mashirika ya umma hivyo ni lazima mabadiliko hayo ya uongozi yaende sambamba na nafasi hizo kutangazwa ili kupata uongozi wenye sifa na imara hatimaye shirika liweze kurudisha hadhi na kuaminika.
"Kwa hali iliyopo sasa shirika ni baya na imefikia sasa haliwezi hata kukopesheka, hivyo tunatambua mtaji uliopo ni mdogo.
"Lakini kwa harufu ya ubadhirifu na matumizi mabaya ya uongozi tumesitisha hata kutoa dhamana mpaka pale litakapokaa sawa na kuweza kuamika ili liweze kukopesheka," alisema Makamba.
Alisema, mabadiliko hayo yatakwenda sambamba na Serikali kulitoa shirika hilo katika ubia na Kampuni ya Airtel ili kuongeza nguvu ya ufanisi na uhuru wa maslahi ya shirika hilo.
Makamba alieleza harakati hizo za kuondokana na ushiriki wa Airtel katika ubia na TTCL zinasubiri maamuzi ya Msajili wa Azina ili kuweza kulipa tathimini ya thamani ya ushiriki.
Pia aliitaka bodi ya shirika hilo kukutana mapema wiki hii na kutoa taarifa kwa CAG ili aweze kufanya ukaguzi wa matumizi ya fedha za shirika huku akiitaka bodi hiyo pia kuhakikisha inawapumzisha viongozi waliopo ili kuruhusu uchunguzi huru.
Makamba alimtaka Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Said Amir Said kuhakikisha hakuna mfanyakazi anayeonewa kwa utendaji wake wa kazi hasa kuwajibishwa kwa kuhamishwa kituo ili kuruhusu ubadhirifu wa mabilioni ya fedha kuendelea.
Pia alielezea kusikitishwa na hali mbaya iliyopo TTCL ya kukosa hata dola 2,000 za kuunganisha wateja huku wizi wa mikonga ya simu na mitambo ukiendelea.
Awali wafanyakazi wa shirika hilo wakiongozwa na Lucas Ishengoma walimueleza Naibu waziri huyo mchezo mchafu uliopo hasa Kanda ya Kaskazini, Dar es Salaam ambapo viongozi wamekuwa wakifanya watakavyo.
"Tunaelewa fika kuwa bajeti ya shirika letu ni sawa na mbwa asiyebweka, kwani inaongozwa na matakawa ya viongozi na sasa hivi kwa kuwa Kanda ya Kaskazini tukiongozwa na meneja tunaonekana tunafuatilia sana mapato na matumizi na tunaonekana tunakiherehere cha utendaji wa kazi.
"Tayari taarifa za meneja kuhamishiwa Mwanza tunazo ili aletwe rafiki wa mabosi, wale vizuri, lakini tunachosema tumechoka huyo mnayemleta hatumtaki kakaeni naye makao makuu,"alisema
Walisema kuwa, wakati uliopo hauna tofauti na ukoloni wa Mwarabu ndani ya shirika hilo kwani kazi ya uongozi ni kupitisha mikataba hewa ambayo haina maslahi kwa taifa huku wakiomba mapato ya mkongo wa taifa wa mawasilaino ambayo hayawafikii.
Naye Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Said Amir Said aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa mabadiliko yoyote yatakayofanywa na Serikali watayapokea hivyo ni vyema mchakato kuanza mapema.
[h=3]Makamba afumua menejimenti TTCL[/h]
Na Mariam Mziwanda
NAIBU Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ameahidi kufumua uongozi uliopo katika Shirika la Simu Tanzania (TTCL) kutokana na shutuma za ubadhirifu yakiwemo matumizi mabaya ya uongozi.
Makamba aliyasema hayo Dar es Salaam jana mara baada ya kupokea ripoti kutoka kwa wafanyakazi wa shirika hilo zilizoeleza vitendo viovu vinavyofanywa na viongozi wa shirika katika kuhujumu mali za umma.
Alisema kuwa, mbali na mikakati ya Serikali iliyopo kulipatia viongozi madhubuti shirika hilo pia amewasiliana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kuwachukulia hatua viongozi wanaohusika na ubadhirifu huo.
"Mimi kama raia na kiongozi nimetoa taarifa TAKUKURU tayari, imekua bahati kwangu leo nimepokea ripoti za wafanyakazi ambazo zina vielelezo vya kutosha juu ya tuhuma za viongozi ambao ni wabadhirifu na wana matumizi mabaya ya uongozi hii itarahisisha zaidi uchunguzi na sheria kuweza kutumika,"alisema.
Aliongeza kuwa, juhudi hizo zitakwenda sambamba na kuhakikisha hatua za kisheria ikiwemo kuwafikisha mahakamni viongozi hao zinafikiwa hivyo amewataka wafanyakazi wengine wenye vielelezo waunge mkono kwa maslahi ya taifa.
Makamba alidai kusikitishwa na udhaifu wa uongozi uliopo katika shirika hilo ambao unajieleza kuwa hakuna heshima wala staha ya shirika hivyo kufananisha mfumo wa kazi baina ya viongozi na watumishi kuwa sawa na makuli bandarini.
Alisema, Serikali ina wajibu wa kuona shirika hilo linarudi katika mfumo bora wa mashirika ya umma hivyo ni lazima mabadiliko hayo ya uongozi yaende sambamba na nafasi hizo kutangazwa ili kupata uongozi wenye sifa na imara hatimaye shirika liweze kurudisha hadhi na kuaminika.
"Kwa hali iliyopo sasa shirika ni baya na imefikia sasa haliwezi hata kukopesheka, hivyo tunatambua mtaji uliopo ni mdogo.
"Lakini kwa harufu ya ubadhirifu na matumizi mabaya ya uongozi tumesitisha hata kutoa dhamana mpaka pale litakapokaa sawa na kuweza kuamika ili liweze kukopesheka," alisema Makamba.
Alisema, mabadiliko hayo yatakwenda sambamba na Serikali kulitoa shirika hilo katika ubia na Kampuni ya Airtel ili kuongeza nguvu ya ufanisi na uhuru wa maslahi ya shirika hilo.
Makamba alieleza harakati hizo za kuondokana na ushiriki wa Airtel katika ubia na TTCL zinasubiri maamuzi ya Msajili wa Azina ili kuweza kulipa tathimini ya thamani ya ushiriki.
Pia aliitaka bodi ya shirika hilo kukutana mapema wiki hii na kutoa taarifa kwa CAG ili aweze kufanya ukaguzi wa matumizi ya fedha za shirika huku akiitaka bodi hiyo pia kuhakikisha inawapumzisha viongozi waliopo ili kuruhusu uchunguzi huru.
Makamba alimtaka Ofisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Said Amir Said kuhakikisha hakuna mfanyakazi anayeonewa kwa utendaji wake wa kazi hasa kuwajibishwa kwa kuhamishwa kituo ili kuruhusu ubadhirifu wa mabilioni ya fedha kuendelea.
Pia alielezea kusikitishwa na hali mbaya iliyopo TTCL ya kukosa hata dola 2,000 za kuunganisha wateja huku wizi wa mikonga ya simu na mitambo ukiendelea.
Awali wafanyakazi wa shirika hilo wakiongozwa na Lucas Ishengoma walimueleza Naibu waziri huyo mchezo mchafu uliopo hasa Kanda ya Kaskazini, Dar es Salaam ambapo viongozi wamekuwa wakifanya watakavyo.
"Tunaelewa fika kuwa bajeti ya shirika letu ni sawa na mbwa asiyebweka, kwani inaongozwa na matakawa ya viongozi na sasa hivi kwa kuwa Kanda ya Kaskazini tukiongozwa na meneja tunaonekana tunafuatilia sana mapato na matumizi na tunaonekana tunakiherehere cha utendaji wa kazi.
"Tayari taarifa za meneja kuhamishiwa Mwanza tunazo ili aletwe rafiki wa mabosi, wale vizuri, lakini tunachosema tumechoka huyo mnayemleta hatumtaki kakaeni naye makao makuu,"alisema
Walisema kuwa, wakati uliopo hauna tofauti na ukoloni wa Mwarabu ndani ya shirika hilo kwani kazi ya uongozi ni kupitisha mikataba hewa ambayo haina maslahi kwa taifa huku wakiomba mapato ya mkongo wa taifa wa mawasilaino ambayo hayawafikii.
Naye Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Said Amir Said aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa mabadiliko yoyote yatakayofanywa na Serikali watayapokea hivyo ni vyema mchakato kuanza mapema.
| ||
|