Wazidi kupoteza maisha

kbm

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
5,222
1,670
Waliopata kikombe cha Babu wa Loliondo wazidi kupoteza maisha. Utafiti uliofanyika wa idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Ukimwi ktk Wilaya na Mkoa wa Geita inasemekana imeongezeka kufuatia hatua ya baadhi ya wagonjwa kuacha kutumia dawa za kupunguza makali ya virusi. Mratibu wa Ukimwi ktk Kitengo cha Matibabu ktk Wilaya ya Geita, amesema watu waliamini kuwa babu alikuwa na dawa ya kutibu ugonjwa wa Ukimwi licha ya kutambua kuwa HAKUNA DAWA ILIYOTHIBITISHWA NA WATALAAMU. Source by Mwananchi - jumatatu.
 
Kuna uthibitisho kuwa walikunywa kikombe cha babu?
Yeye kama mtaalam anachukua hatua gani kuhakikisha watu hawafi? Kwa nafasi yake ya uratibu itakua vyema akifanya juhudi kupunguza hivyo vifo, na si kuutangzia umma kuwa watu wanakufa kwa sababu ya kikombe cha babu, halafu akishatangaza ndo hawafi? Afanye kazi yake
 
Wiseboy umenena! Afanye kazi yake ya kuhakikisha vifo hivyo havitokei kwa kuchukulia kikombe cha babu kama changamogo ingine katika kupiga vita janga hilo.
 
Kuna uthibitisho kuwa walikunywa kikombe cha babu?
Yeye kama mtaalam anachukua hatua gani kuhakikisha watu hawafi? Kwa nafasi yake ya uratibu itakua vyema akifanya juhudi kupunguza hivyo vifo, na si kuutangzia umma kuwa watu wanakufa kwa sababu ya kikombe cha babu, halafu akishatangaza ndo hawafi? Afanye kazi yake

Kwa hiyo hakuna haja ya kutangaza jambo lolote? Maana yeye kama mratibu anatoa sababu za wagonjwa kufariki sasa ulitaka yeye ndio awanyweshe hizo dawa? Sio siri babu wa Loliondo ni janga na anakesi za mauaji sema tu hii sirikale yetu imeenda Gamboshi!
 
Kuna uthibitisho kuwa walikunywa kikombe cha babu?
Yeye kama mtaalam anachukua hatua gani kuhakikisha watu hawafi? Kwa nafasi yake ya uratibu itakua vyema akifanya juhudi kupunguza hivyo vifo, na si kuutangzia umma kuwa watu wanakufa kwa sababu ya kikombe cha babu, halafu akishatangaza ndo hawafi? Afanye kazi yake

Hivi unafahamu maana ya utafiti? ushawahi kufanya au kusoma ripoti yoyote ya utafiti?
Mwandishi wa habari kalenga upande mmoja tu wa utafiti, nao ni madhara...pengine katika hiyo habari mwandishi kaeleza na njia za kufuatwa kurekebisha tatizo(sijasoma gazeti), ila nina uhakika katika ripoti ya utafiti jambo hilo litakuwepo tu maana ndio "format" ya utafiti inapaswa kuwa.
 
..., kwa ujumla serikali ndiyo wakubebeshwa lawama' tangia mwanzo walikuwa wanajua kuwa uganga wa tiba za mitishamba haukubaliki bila ya kufanyiwa utafiti na taasisi husika kisheria, na wakati mwingine serikali yetu ilimuunga mkono babu kwa njia moja au nyingine, kwa kutengeneza miundombinu n.k, na bilasha walijua kuwa jambo hili nila ki-Imani, ni kwa nini hawakuchukua hatua mapema, na kuwaacha waathilika wakiacha matumizi ya ARV, wakati serikali imetumia mabilioni ya kodi kugarimia ununuzi wa dawa hizo. Na sasa wanakuja na kauli za kutolea taarifa madhara ya kikombe cha babu. Hii inanikumbusha DECI.
 
Back
Top Bottom