Elections 2010 Wazee wetu wanatuangusha huko kijijini, Je tuwatose?

Ngonini

JF-Expert Member
Sep 1, 2010
2,023
563
Hivi majuzi nilitembelewa na mama yangu kutoka kijijini kwetu. nilitaka kujua hali ya kisiasa huko wilayani kwetu maana ni sehemu ya ngome ya Mzee Mapesa. aliniambia kuwa mchuano ni mkali mpaka kwenye udiwani. Nilifurahia maana hata serikali za vijiji vingi vinaongozwa na MAGEUZI (kama wanavyowaita wao). Kuhusu ubunge alisema Mzee wa vijicenti atapita maana watu wanachuma mno kwake. Alisema lakini kwenye jimbo la Mzee MAPESA sisiemu hawatafua dafu. Nilipomuliza Kuhusu urais yeye alisema KIGWEDE(ndivyo wanavyomwita wao).

Kuhusu namna kampeni zinavyoendeshwa, alisema wao huwa wanakusanywa kwenye vikundi ili kwenda kwenye mikutano ya sisiemu wakiwa wameahidiwa chumvi,kanga na fedha tasilimu. Mama yangu alikuwa akilalamika kuwa siku moja waliahidiwa kupewa fedha na baada ya mkutano waliambulia TSH 5000 (huku wakiwa watu zaidi ya 50)kama kikundi ili wagawane. waliishia kununua chumvi wakagawana kila mtu kiganja kimoja(Handful).

Nilichokipata kutoka maongezi na mama yangu ni uelewa mdogo wa mambo, yeye anasema "sisi hata hatujiwi kama watu wingi hivi hawamtaki KIGWEDE, sisi tunajua anakubalika tu".
Ndipo nilipomwelezea hali halisi ya watu kutaka mabadiliko. Alishangaa na kusema hata sisi tungepata mtu wakuelimisha SISIEMU tumeichoka ila hatujui cha kufanya.

Alikili kuwa ukipewa hongo na sisiemu, watakutishia mpaka utawapigia kura maana wanaogopa kuwa wanaweza kukundulika kuwa hawakuipigia sisiemu.



MIMI NAONA KUNA HAJA YA KUWAAMBIA WAZEE WETU KAMA HAWATAKI KUBADILIKA BASI NA SISI WASITEGEMEE MSAADA KUTOKA KWETU. TUNAPATA KIMSHAHARA KIDUCHU BADO TUNAGAWANA NAO ILI WAPATE CHAKULA,DAWA, ELIMU N.K WAKATI SERIKALI IMEKAA DAR NA DODOMA WAKILA KUKU BADALA YA KUWATIMIZIA HAYA WANANCHI WAKE.

WAZEE HAWA NI LAZIMA WATUELEWE MAANA SISI JAPO TUNA NAFUU KULIKO WAO, LAKINI BADO HAWATAKI KUTUELEWA. JIBU HAPA NIKUWANYIMA SERVICE ILI WATAMBUWE UMUHIMU WA KUWA NA SERIKALI INAYOWAJIBIKA.
KAMA SISIEMU INAWATISHIA NA KUKUBALIANA NAYO, BASI NA SISI TUWANYIME MISAADA YETU KAMA SISIEMU ITAWAPATIA HAYO MAHITAJI. TUKIFANYA HIVI WATABADILIKA NA NDO ITAKUWA KIFO CHA SISIEMU HUKO VIJIJINI PIA.

NILAZIMA TUONDOKE NA WAZEE WETU, HATUWAACHII SISIMU, WATATUELEWA HUKO MBELE TULIMAANISHA NIN KUWALAZIMISHA KUHAMA SISIEMU!

TUSIPOTUMIA NGUVU KAMA HII, ITATUCHUKUA MIAKA ZAIDI KUPATA USHINDI.

NAOMBA KUWASILISHA!
 
Hapana mkuu hatuna haja ya kuwatosa wazee wetu ni kuwapa elimu ya kutosha waelewe kinachoendelea!
 
hivi majuzi nilitembelewa na mama yangu kutoka kijijini kwetu. Nilitaka kujua hali ya kisiasa huko wilayani kwetu maana ni sehemu ya ngome ya mzee mapesa. Aliniambia kuwa mchuano ni mkali mpaka kwenye udiwani. Nilifurahia maana hata serikali za vijiji vingi vinaongozwa na mageuzi (kama wanavyowaita wao). Kuhusu ubunge alisema mzee wa vijicenti atapita maana watu wanachuma mno kwake. Alisema lakini kwenye jimbo la mzee mapesa sisiemu hawatafua dafu. Nilipomuliza kuhusu urais yeye alisema kigwede(ndivyo wanavyomwita wao).

Kuhusu namna kampeni zinavyoendeshwa, alisema wao huwa wanakusanywa kwenye vikundi ili kwenda kwenye mikutano ya sisiemu wakiwa wameahidiwa chumvi,kanga na fedha tasilimu. Mama yangu alikuwa akilalamika kuwa siku moja waliahidiwa kupewa fedha na baada ya mkutano waliambulia tsh 5000 (huku wakiwa watu zaidi ya 50)kama kikundi ili wagawane. Waliishia kununua chumvi wakagawana kila mtu kiganja kimoja(handful).

Nilichokipata kutoka maongezi na mama yangu ni uelewa mdogo wa mambo, yeye anasema "sisi hata hatujiwi kama watu wingi hivi hawamtaki kigwede, sisi tunajua anakubalika tu".
Ndipo nilipomwelezea hali halisi ya watu kutaka mabadiliko. Alishangaa na kusema hata sisi tungepata mtu wakuelimisha sisiemu tumeichoka ila hatujui cha kufanya.

Alikili kuwa ukipewa hongo na sisiemu, watakutishia mpaka utawapigia kura maana wanaogopa kuwa wanaweza kukundulika kuwa hawakuipigia sisiemu.



Mimi naona kuna haja ya kuwaambia wazee wetu kama hawataki kubadilika basi na sisi wasitegemee msaada kutoka kwetu. Tunapata kimshahara kiduchu bado tunagawana nao ili wapate chakula,dawa, elimu n.k wakati serikali imekaa dar na dodoma wakila kuku badala ya kuwatimizia haya wananchi wake.

Wazee hawa ni lazima watuelewe maana sisi japo tuna nafuu kuliko wao, lakini bado hawataki kutuelewa. Jibu hapa nikuwanyima service ili watambuwe umuhimu wa kuwa na serikali inayowajibika.
Kama sisiemu inawatishia na kukubaliana nayo, basi na sisi tuwanyime misaada yetu kama sisiemu itawapatia hayo mahitaji. Tukifanya hivi watabadilika na ndo itakuwa kifo cha sisiemu huko vijijini pia.

Nilazima tuondoke na wazee wetu, hatuwaachii sisimu, watatuelewa huko mbele tulimaanisha nin kuwalazimisha kuhama sisiemu!

Tusipotumia nguvu kama hii, itatuchukua miaka zaidi kupata ushindi.

Naomba kuwasilisha!

ngonini inaonekana hata wzazi wako haukuwapatia habari kuwa kigwede alikataa kuongeza mishahara ili uwezo kuwa na uwezo wa kuwaongezea kile kidogo unachowatumia. Kwa kifupi watanzania wengi hatujafanya homework zetu ili kufanikisha mageuzi. Jf ni sehemu ya kupata elimu na kubadilishana mawazo tu; tunachokipata humu tunatakiwa kukisambaza kwa wanchi wenzetu kama vile wazazi na wengineo ili kuchochea mabadiliko.
 
Wanafunzi wa vyuo waliokataliwa kurudi vyuoni watumie fursa hii kuwaelimisha wazee juu ya kiongozi bora huko vijijini wasikose yote
 
Kigwede bwana. Waendelee kuogopa tu ila mpe somo akawaelimishe na wenzake
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom