Phdum
JF-Expert Member
- Apr 15, 2019
- 810
- 1,667
Vijana wa kileo hatuna kabisa desturi ya kukaa na wazee ili tupate madini waliyonayo. nakuhakikishia hawa wazee wanajua masuala mengi sana kuhusu maisha na vitu vingi walivyokuwa wanaona sio sahihi ila sisi vijana wa kileo tunaona ni sahihi huku tukisema ndio utandawazi.
Sikia hii. Uliwahi kusikia au unafahamu ule usemi usemao "mwanamke mwenye mimba hana ujanja"? Mimi ni miongoni mwa watu waliokuwa wanasikia tu huo msemo ila sikuwahi fahamu kuwa inamaanisha nini.
Jana nilibahatika kukaa na bibi moja nikamuuliza kuhusiana na hii kauli kwamba kwanini mwanamke mwenye mimba hana ujanja.
Kwa maelezo yake ni kwamba mwanamke mwenye mimba akichanganya damu yaani kushiriki na wanaume/mwanamme mwingine ambaye sio mhusika wa mimba siku ya kujifungua atakuwa katika hatari ya kupatwa na mambo makuu mawili
Moja: ni kupata kifafa cha mimba na hata kumpelekea kupoteza maisha yake na hata maisha ya mwanaye pia nikajagundua kuwa siku hizi nasikia vifafa vya mimba vimeongezeka labda chanzo ni hii japo kitaalam kuna chanzo chake ila hawa wazee wetu walikuwa wanaamini kifafa cha mimba hutokana na kuchanganya wanaume wakati wa mimba.
Jambo la pili: walikuwa wanaamini kuwa ukichanganya wanaume ukiwa na mimba siku ya kujifungua utapata sana shida. Unaweza kumaliza siku hata mbili bila kujifungua mpaka aje mtaalamu na kukuuliza kama umechanganya wanaume na ukikubali tu anafanya yake ndio utaweza kujifungua vizuri. hapa napo nikapata ukakasi kuwa au hata hivi vioperation vya kila siku kwa wake zetu hili linaweza kuwa ni chanzo japo wataalam wa afya nao wana sababu zao za kiafya zinazosababisha upasuaji kuongozeka kwa wingi. Maana siku hizi unakuta mwanamke mjamzito lakini mechi za ugenini wanapiga kama kawa.
Karibu na wewe mdau utoe nondo uliopata kutoka kwa hawa wazee wetu
Sikia hii. Uliwahi kusikia au unafahamu ule usemi usemao "mwanamke mwenye mimba hana ujanja"? Mimi ni miongoni mwa watu waliokuwa wanasikia tu huo msemo ila sikuwahi fahamu kuwa inamaanisha nini.
Jana nilibahatika kukaa na bibi moja nikamuuliza kuhusiana na hii kauli kwamba kwanini mwanamke mwenye mimba hana ujanja.
Kwa maelezo yake ni kwamba mwanamke mwenye mimba akichanganya damu yaani kushiriki na wanaume/mwanamme mwingine ambaye sio mhusika wa mimba siku ya kujifungua atakuwa katika hatari ya kupatwa na mambo makuu mawili
Moja: ni kupata kifafa cha mimba na hata kumpelekea kupoteza maisha yake na hata maisha ya mwanaye pia nikajagundua kuwa siku hizi nasikia vifafa vya mimba vimeongezeka labda chanzo ni hii japo kitaalam kuna chanzo chake ila hawa wazee wetu walikuwa wanaamini kifafa cha mimba hutokana na kuchanganya wanaume wakati wa mimba.
Jambo la pili: walikuwa wanaamini kuwa ukichanganya wanaume ukiwa na mimba siku ya kujifungua utapata sana shida. Unaweza kumaliza siku hata mbili bila kujifungua mpaka aje mtaalamu na kukuuliza kama umechanganya wanaume na ukikubali tu anafanya yake ndio utaweza kujifungua vizuri. hapa napo nikapata ukakasi kuwa au hata hivi vioperation vya kila siku kwa wake zetu hili linaweza kuwa ni chanzo japo wataalam wa afya nao wana sababu zao za kiafya zinazosababisha upasuaji kuongozeka kwa wingi. Maana siku hizi unakuta mwanamke mjamzito lakini mechi za ugenini wanapiga kama kawa.
Karibu na wewe mdau utoe nondo uliopata kutoka kwa hawa wazee wetu