Wazee wa Mtama washindwa kuzuia hisia zao kwa Rais Magufuli

WAZEE WA MTAMA WASHINDWA KUZUIA HISIA ZAO KWA RAIS MAGUFULI

22 Februari, 2020

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dkt. Bashiru Ally akiendelea na ziara yake Mkoani Mtwara kuelekea jimbo la Ndanda kupitia jimbo la Mtama, wazee wameshindwa kuzuia hisia zao kwa Rais Magufuli kwa kuonesha nia ya kutaka kumchangia gharama za fomu za Urais mwaka 2020.

Akieleza kwa niaba ya wazee hao, Mbunge wa jimbo la Mtama Ndg. Nape Mosses Nnaye, ameleeza kuwa wazee wapo tayari na wamejipanga kumchangia gharama za fomu za Urais ili kuonesha mapenzi yao kwake kutokana na namna anavyowajali wazee na wananchi kwa ujumla, hivyo wanasubiri kibali kwa Katibu Mkuu.

Wameyasema hayo asubuhi ya leo tarehe 22 Februari, 2020 katika ufunguzi wa shina la Wakereketwa la Kambarage jimboni Mtama.

Katibu Mkuu pamoja na mambo mengine, akifafanua uamuzi huo wa wazee, ameeleza kuwa, nia yao ni njema na imekuwa matamanio ya wazee wengi kufanya hivyo kama wao wa Mtama, amepokea nia yao njema lakini kikubwa wao waendelee kumuombea Mhe. Rais afya njema ili awatumikie zaidi bila kuchoka.

Katibu Mkuu yupo Mkoani Mtwara kwa ziara ya kikazi ya siku tatu, yenye lengo la kuendelea kukirejesha Chama kwa wanachama

Imetolelewa na;
Said Said Nguya
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)


Sent using Jamii Forums mobile app
Nape’s another bloody sycophant!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom