Wazee wa Jadi na Machifu Wapeni Kauri Mafisadi Waludishe Mapesa Ya Umma!!!!

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Nimevutiwa na tamko la Machifu wa Mbeya dhidi ya tukio la mauaji la Mwenyekiti wa CCM,wa Wilaya.Huku ndani ya JF kuna thread Mchambuzi nilichangia kama wiki mbili zilizopita nikasema kama Wazee wa Jadi na Machifu wakiamka wakatoa matamko dhidi ya matukio ambayo yamekuwa yakiendelea kwa Watanzania kama UFISADI au MAADILI hakika tutaona maajabu kuwa yatoweka kwa ajabu sana.

Watanzania wengi wanaheshimu JADI sana kuliko dini zao, hivyo kitendo cha jamii husika kama ilivyotokea Mbeya, wale Machifu wa eneo husika wakiamka wakawaita walengwa wa Jamii ya kwao ambao wanajulikana kwa matendo yao ya KIFISADI kwenye jamii na wakapewa tamko la Machifu na Wazee wa Jadi hakika tutashangaa yatakayotokea.

Tumeona tamko la Wanambeya na matokeo yake!!!!Ebu Wana JF baadhi tunawafahamu wazee na Machifu ebu waamsheni waamke kukemea Maadili na kuwahimiza mafisadi kuludisha Pesa walizokwiba, wazilejeshe zijenge shule na hospital nina imani sana na kauri za wazee na Machifu kuwa ndani ya wiki kila FISADI atakuwa ameludisha Pesa hizo na watu hawataamini!!!!
 
Back
Top Bottom