Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Wazee wa Jimbo la Arusha Mjini Wamedai kuwa kauli ya Mbunge wao Mrisho Gambo kuwa Wamachinga Wanyanyaswa na Mgambo wa Jiji ina lengo la kuchonganisha Wafanyabiashara hao na Serikali kwani zoezi la kuhamisha wamachinga lilishirikisha pande zote wakiwemo viongozi wao.
Gambo alidai mbele ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Abdullahaman Kinana kuwa Mgambo wa Jiji wanawanyanyasa Machinga kwa kuwakamatia Biashara zao kwa kudai ya kufanyabiashara kinyume na utaratibu.
Kauli hiyo ilipingwa vikali na Wazee hao wakiongozwa na Shekh Saidi Rashid kwa kueleza kuwa Mbunge huyo afuate taratibu katika kuwasilisha hoja zake na sio kukimbilia kwa viongozi wa ngazi za juu wa Chama.
Mzee Rashid alisema Mbunge Gambo kila wakati amekuwa akikinzana na maamuzi wa watendaji wa Jiji wakiongozwa na Mkurugenzi DktJohn Pima na kueleza kuwa malalamiko ya Mbunge huyo ni ya uchonganishi na yenye hila kwa viongozi wa Jiji dhidi ya Wananchi hatua ambayo ni mbaya kama kiongozi.
Dkt Pima amekuwa akifanya mambo mengi ya Mandeleo katika Jiji la Arusha ikiwemo kuongeza Pato la Ukusanyaji wa Mapato tofauti na Awali lakini hilo halipongezwi na Gambo na amekuwa mtu wa kumchonganisha Mkurugenzi huyo na viongozi wa Juu wa Nchi hatua ambayo sio sahihi.
"Tunamwambia Gambo acha mara moja fitina,Majungu na Uchonganishi kwani Arusha ni salama na mambo yote yako sawa ikiwa ni pamoja na machinga kuwa na vibanda vya kufanyia biashara na vingine viko wazi baada ya kutosheka'' Alisema Shekh Rashid
Wazee hao wametishia kumnyima kura iwapo ataendelea na tabia yake ya kujali maslahi yake na kushindwa kushirikiana na viongozi wenzake .
Gambo alidai mbele ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Abdullahaman Kinana kuwa Mgambo wa Jiji wanawanyanyasa Machinga kwa kuwakamatia Biashara zao kwa kudai ya kufanyabiashara kinyume na utaratibu.
Kauli hiyo ilipingwa vikali na Wazee hao wakiongozwa na Shekh Saidi Rashid kwa kueleza kuwa Mbunge huyo afuate taratibu katika kuwasilisha hoja zake na sio kukimbilia kwa viongozi wa ngazi za juu wa Chama.
Mzee Rashid alisema Mbunge Gambo kila wakati amekuwa akikinzana na maamuzi wa watendaji wa Jiji wakiongozwa na Mkurugenzi DktJohn Pima na kueleza kuwa malalamiko ya Mbunge huyo ni ya uchonganishi na yenye hila kwa viongozi wa Jiji dhidi ya Wananchi hatua ambayo ni mbaya kama kiongozi.
Dkt Pima amekuwa akifanya mambo mengi ya Mandeleo katika Jiji la Arusha ikiwemo kuongeza Pato la Ukusanyaji wa Mapato tofauti na Awali lakini hilo halipongezwi na Gambo na amekuwa mtu wa kumchonganisha Mkurugenzi huyo na viongozi wa Juu wa Nchi hatua ambayo sio sahihi.
"Tunamwambia Gambo acha mara moja fitina,Majungu na Uchonganishi kwani Arusha ni salama na mambo yote yako sawa ikiwa ni pamoja na machinga kuwa na vibanda vya kufanyia biashara na vingine viko wazi baada ya kutosheka'' Alisema Shekh Rashid
Wazee hao wametishia kumnyima kura iwapo ataendelea na tabia yake ya kujali maslahi yake na kushindwa kushirikiana na viongozi wenzake .