Wazazi wote Tanzania shime tuungane na walimu.

manuu

JF-Expert Member
Apr 23, 2009
4,064
10,723
Hivi ukiwa kama mzazi mwenye mtoto anaesoma katika shule ambazo walimu wamegoma,Unampango gani juu ya swala hili la watoto wetu kwenda shule asubuhi na kurudi nyumbani bila kufundishwa?
Nadhani kila mmoja wetu atakuwa anahusika kwa namna moja ama nyingine kwani kama si mtoto wako ni dada ako,kaka ako.shangazi ako yupo katika shule hizi.

Nafikiri umefika wakati watanzania tuwache woga na tuweze kuiwajibisha serikali yetu pale inapobidi kwa vitendo siyo kwa kuonyesha hasira zetu kwenye keyborad tu hapa then kila mtu anakwenda kwake kulala.
Taifa linaendeshwa kama hakuna msomi hata mmoja ama kama hakuna mtu mwenye uwelewa wa kuona hali ilipofika ni mbaya na inahitaji jitahadi zangu mimi na wewe kuweza kupambana na hili.

TUWACHE WOGA NCHI YETU INAELEKEA KORONGONI TUAMKE WOTE TUIKOMBOE NCHI YETU.

Hapa tumekubaliana tupo kama wazazi 20 tunakwenda kwa mkuu wa mkoa tunataka atupe muafaka wa watoto wetu na ikibidi tutashawishi wananchi wenye uchungu na taifa hili tufanye maandamano ya amani kuonyesha kutokuridhika nahili.

Juzi NSSF,PPF hadi miaka 50,Leo watoto wetu hawapati haki yao ya msingi kabisa.

NA TUPO TU, TUNASUBIRI MUUJIZA KUTOKA MBINGUNI AMA?
 
Ngoja tumsikie Mr Dhaifu leo ataongelea nini kwenye ngonjela yake, kweli inauma sana.Sijui tunajenga taifa gani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom