Wazazi wilaya Temeke tumewakosea nini Wizara ya elimu?

Mgodo visa

JF-Expert Member
Nov 1, 2016
3,562
3,558
Kama uzi unavyo jieleza hapo juu.
Ni masikitiko yangu (huu sasa ni mwaka wa pili) pamoja wa wazazi wengine.

Kumekuwa/Umeibuka mtindo ama utaratibu kutoka Wizara inayohusika na mambo ya Taaluma, kuwaelekeza Maafisa Elimu (W) kuhakikisha karibu 100% ya Wanafunzi wote kutoka Shule za watu binafsi ama taasisi za Kidini, walio hitimu na kufaulu mitihani yao Elimu ya Msingi, wanapelekwa (wanachaguliwa) katika Shule za Kata (Saint Kayumba)

Naandika haya, nikiwa kama mzazi na Muhanga wa maamuzi haya.

Fikiria pale Mzazi/Mlezi unapojinyima na kujipinda (kwa kulipa Mamilioni) kuhakisha mtoto (mwanafunzi) wako anapata Elimu bora na katika Shule yenye Mazingira bora, anafaulu mitihani yake kwa Alama nzuri tu (A ama B) kisha anachaguliwa kwenda katika Sekondari za Kata, kwa kweli inauma sana...!

Wanasema huu ni mpango wa makusudi kuwafanya watoto wetu (wa-kishua) waishi kama "Mashetani".

Wanasema kama Mzazi/Mlezi wake aliweza kulipa Mamilioni Miaka saba ya Msingi, atashindwa vipi kulipa Mamilioni kwa miaka minne inayofuata...!

Kumbuka Mzazi, mtoto wako anahitimu kutoka katika Shule aliyofunzwa maadili Mema (Mazuri) sasa unalazimishwa umpeleke "CHANGANYIKENI" katika Shule ambazo 90% ya wanafunzi wake wana ndoto ya kuwa kama Diamond, Manfongo, Giggy au Shilole, naomba niseme "this is unfair"..

Inapo tokea Wazazi/Walezi kuhoji utaratibu huu kwa Wakuu wa Shule, wanatupa majibu kuwa, ni lengo na matarajio ya Serikali kuwa, kujaza wanafunzi walio faulu kutoka Mashule binafsi, kutaleta mabadiriko kitaaluma, hivyo kuleta tafsiri (tumaini) kwa wananchi kuwa, sasa Shule za kata nazo ziko vizuri kushindana na Mashule binafsi kitaaluma...!

NB: Wizara inasahau kuwa huko hakuna Waalimu bora, vitendea kazi vya kutosha pia Maabara za kufundishia kwa vitendo.

Matokeo tunakwenda kuua ndoto na matarajio ya watoto wetu.

Wilaya ya TEMEKE ni Wahanga wakubwa katika hili.
 
Usemalo ni kweli kabisa mkuu..Mdogo wangu amepata jumla ya alama 234 darasa la saba na A zote tano eti kachaguliwa shule ya kata serious?
 
Iluboru,Mzumbe,kibaha,tabora boys,na nyingine za vipaji maalumu wameenda akina nani????.. Ukiona hajapangiwa shule za vipanga ujue kashazidiwa na vipanga wenzake...saiz watu wanafaulu marks za huu mpaka mwenyew nashangaa
 
Kama uzi unavyo jieleza hapo juu.
Ni masikitiko yangu (huu sasa ni mwaka wa pili) pamoja wa wazazi wengine.

Kumekuwa/Umeibuka mtindo ama utaratibu kutoka Wizara inayohusika na mambo ya Taaluma, kuwaelekeza Maafisa Elimu (W) kuhakikisha karibu 100% ya Wanafunzi wote kutoka Shule za watu binafsi ama taasisi za Kidini, walio hitimu na kufaulu mitihani yao Elimu ya Msingi, wanapelekwa (wanachaguliwa) katika Shule za Kata (Saint Kayumba)

Naandika haya, nikiwa kama mzazi na Muhanga wa maamuzi haya.

Fikiria pale Mzazi/Mlezi unapojinyima na kujipinda (kwa kulipa Mamilioni) kuhakisha mtoto (mwanafunzi) wako anapata Elimu bora na katika Shule yenye Mazingira bora, anafaulu mitihani yake kwa Alama nzuri tu (A ama B) kisha anachaguliwa kwenda katika Sekondari za Kata, kwa kweli inauma sana...!

Wanasema huu ni mpango wa makusudi kuwafanya watoto wetu (wa-kishua) waishi kama "Mashetani".

Wanasema kama Mzazi/Mlezi wake aliweza kulipa Mamilioni Miaka saba ya Msingi, atashindwa vipi kulipa Mamilioni kwa miaka minne inayofuata...!

Kumbuka Mzazi, mtoto wako anahitimu kutoka katika Shule aliyofunzwa maadili Mema (Mazuri) sasa unalazimishwa umpeleke "CHANGANYIKENI" katika Shule ambazo 90% ya wanafunzi wake wana ndoto ya kuwa kama Diamond, Manfongo, Giggy au Shilole, naomba niseme "this is unfair"..

Inapo tokea Wazazi/Walezi kuhoji utaratibu huu kwa Wakuu wa Shule, wanatupa majibu kuwa, ni lengo na matarajio ya Serikali kuwa, kujaza wanafunzi walio faulu kutoka Mashule binafsi, kutaleta mabadiriko kitaaluma, hivyo kuleta tafsiri (tumaini) kwa wananchi kuwa, sasa Shule za kata nazo ziko vizuri kushindana na Mashule binafsi kitaaluma...!

NB: Wizara inasahau kuwa huko hakuna Waalimu bora, vitendea kazi vya kutosha pia Maabara za kufundishia kwa vitendo.

Matokeo tunakwenda kuua ndoto na matarajio ya watoto wetu.

Wilaya ya TEMEKE ni Wahanga wakubwa katika hili.
Mwanao anawastan wa ngapi na anamarks ngapi..tuanzie apo kwanza unawezakuta ..izooo pugu,minaki,iluboru,Mzumbe.mnazozitaka hajafikia wastan wao
 
Iluboru,Mzumbe,kibaha,tabora boys,na nyingine za vipaji maalumu wameenda akina nani????.. Ukiona hajapangiwa shule za vipanga ujue kashazidiwa na vipanga wenzake...saiz watu wanafaulu marks za huu mpaka mwenyew nashangaa
Hizo Shule wanapelekwa wale walio faulu kwa wastani sawa na wengine, kigezo watokee tu Shule za Serikali, na hao ndio watakao kuwa na KIPAUMBELE hapo kesho katika swala zima la MIKOPO Elimu ya juu.

Ni mpango MAHASUSI umeratibiwa.
 
Mwanao anawastan wa ngapi na anamarks ngapi..tuanzie apo kwanza unawezakuta ..izooo pugu,minaki,iluboru,Mzumbe.mnazozitaka hajafikia wastan wao
Mkuu huku TMK huwa tunapigania zaidi kupata Shule moja tu ya Kibasila (achana na hizo Azania ama Forodhani)
 
Waacheni watoto wa maskini wanaopambana na changamoto za kila namna na bado wanafaulu vizuri sana ndio wapate hizo nafasi. Hao watoto wenu toka private schools mara nyingi si vipanga halisi bali ni yale mazingira ya kutafuniwa kila kitu ndo huwafanya wafaulu vizuri. Wako very dependent, socially incompetent na wana tabia mbaya za dharau, kutojali na hawana motivation toka ndani. Wakija shule nzuri za serikali wanaishia kufeli na kuchafua majina ya shule hizo. So, kama mlianza huko malizeni huko huko tukutane vyuo au highschool. Hatuwatengi ila ndo ukweli kwamba serikali haiwezi kuacha kila jema nchi hii litwaliwe na strata ya wenye vijihela mnaodhani watoto wanaosoma shule za kata wote hawana dreams
 
Waacheni watoto wa maskini wanaopambana na changamoto za kila namna na bado wanafaulu vizuri sana ndio wapate hizo nafasi. Hao watoto wenu toka private schools mara nyingi si vipanga halisi bali ni yale mazingira ya kutafuniwa kila kitu ndo huwafanya wafaulu vizuri. Wako very dependent, socially incompetent na wana tabia mbaya za dharau, kutojali na hawana motivation toka ndani. Wakija shule nzuri za serikali wanaishia kufeli na kuchafua majina ya shule hizo. So, kama mlianza huko malizeni huko huko tukutane vyuo au highschool. Hatuwatengi ila
Likes×1000
 
Waacheni watoto wa maskini wanaopambana na changamoto za kila namna na bado wanafaulu vizuri sana ndio wapate hizo nafasi. Hao watoto wenu toka private schools mara nyingi si vipanga halisi bali ni yale mazingira ya kutafuniwa kila kitu ndo huwafanya wafaulu vizuri. Wako very dependent, socially incompetent na wana tabia mbaya za dharau, kutojali na hawana motivation toka ndani. Wakija shule nzuri za serikali wanaishia kufeli na kuchafua majina ya shule hizo. So, kama mlianza huko malizeni huko huko tukutane vyuo au highschool. Hatuwatengi ila ndo ukweli kwamba serikali haiwezi kuacha kila jema nchi hii litwaliwe na strata ya wenye vijihela mnaodhani watoto wanaosoma shule za kata wote hawana dreams
Maneno ama mtazamo wako unaweza kuwa na ukweli kwa kiasi fulani, ila kumbuka, kupora ama kunyang'anya haki ya mtu (Mwanafunzi) kwa sababu ya kukomoana ama kisiasa, kweli si jambo zuri na la kushabikia hata kidogo..!

Kwa mtindo huu, Serikali itajikuta inazalisha Vilaza kila mwaka.
 
Mi wamenikwaza mwanangu kapata wastani wa A, Jumla marks 232 kati ya marks 250 halafu kapelekwa shule ya kata mbaya kuliko zote halafu ni day mbali haswaaa, wabaki tu na shule yao
 
Iluboru,Mzumbe,kibaha,tabora boys,na nyingine za vipaji maalumu wameenda akina nani????.. Ukiona hajapangiwa shule za vipanga ujue kashazidiwa na vipanga wenzake...saiz watu wanafaulu marks za huu mpaka mwenyew nashangaa
Ww sio muhanga Wa hili,acha siasa.Acha wahanga waongee
 
Back
Top Bottom