Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka Wazazi kuwasimamia watoto katika matumizi ya vifaa vya kielektroniki ili kuwaepusha kujiingiza katika vitendo vya ngono na ukatili mwingine mitandaoni
”Watoto wanafikia hatua kutaka kujiua kwasababu wanakutana na Watu mitandaoni wanawasema vibaya”
Ummy ameyasema hayo Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishiwa June 16 kila mwaka
”Watoto wanatumia vifaa vya kielektroniki ikiwemo simu na kompyuta kujifunzia, ni vizuri wazingatie matumizi sahihi ya vifaa hivyo ili kuepusha kufanyiwa vitendo vya kikatili”
“Katika eneo la malezi ya Watoto wetu bado kuna changamoto kubwa ya matumizi ya mitandao tuhakikishe tunawasimamia Watoto wetu wasijiingize katika masuala yasiyofaa katika mitandao hiyo, Watoto wakiwa nyumbani katika kipindi hiki wajiepushe kwenda kwenye maeneo yatakayohatarisha usalama wao, ikiwa pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kushawishiwa kufanya ngono na hata kupata maambukizi ya corona”-
UMMY
”Watoto wanafikia hatua kutaka kujiua kwasababu wanakutana na Watu mitandaoni wanawasema vibaya”
Ummy ameyasema hayo Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yanayoadhimishiwa June 16 kila mwaka
”Watoto wanatumia vifaa vya kielektroniki ikiwemo simu na kompyuta kujifunzia, ni vizuri wazingatie matumizi sahihi ya vifaa hivyo ili kuepusha kufanyiwa vitendo vya kikatili”
“Katika eneo la malezi ya Watoto wetu bado kuna changamoto kubwa ya matumizi ya mitandao tuhakikishe tunawasimamia Watoto wetu wasijiingize katika masuala yasiyofaa katika mitandao hiyo, Watoto wakiwa nyumbani katika kipindi hiki wajiepushe kwenda kwenye maeneo yatakayohatarisha usalama wao, ikiwa pamoja na kubakwa, kulawitiwa, kushawishiwa kufanya ngono na hata kupata maambukizi ya corona”-
UMMY