Wazazi wangu wanataka kuachana, nifanyeje?

Felixonfellix

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
1,672
182
Tushirikiane kumshauri mtu huyu jamani:


Naomba ndugu muniombee niko kwenye majaribu makubwa hadi inafika wakati najisikia sina hata nguvu ya kuomba. Mara kwa mara huwa najiuliza kama kweli Mungu yuko karibu nami. Lakini naamini siku moja Mungu atanikumbuka.

Cha kwanza naomba muniombee, wazazi wangu wanataka ku-divorce, yaani baba yangu alishatuacha nyumbani mimi na wadogo zangu na mama yangu. Sasa wazazi hawasikilizani na wanataka ku-divorce. Mimi nimejaribu kuwaombea muda mrefu na kuwashauri lakini hawanisikii, nami kwa hivyo nimeshachoka na sijui nifanye nini.

Kingine mnaonaje nikiwashauri wazazi wangu kuachana, kweli nitakuwa nimefanya dhambi? Sijui cha kufanya, lakini neno la Mungu linasema kama kilichounganishwa na Mungu mwanadamu asikitenganishe. Naomba mnisaidie hapo!

Cha tatu naomba mnisaidie kuomba ili nipate mume mwema kutoka kwa Mungu kwa sababu mara nyingi naogopaga nasema labda sitakuja kuolewa. Sababu ni kuwa mambo ninayoyaona kwa wazazi wangu yananiogopesha sana hadi nakata tamaa, najiuliza hivi nikipata mume ambaye hatusikilizani hali itakuwa ya namna gani?.
Jamani nawaombeni mnisadie sana kwa maombi na ushauri.
Naitwa -------------- na nina miaka 25.
Mungu awabariki sana!
 
duh kwa hii story! we ni kama dada angu, lakin ye hayupo jeief. . . .au
ok, ni mapito tu, endelea kusali sana, MUNGU anakusikia na anajua anachofanya! Pia huo mwenendo wa wazaz usikufanye wewe ukate tamaa, kila mtu ana njia yake utapata mume mzuri na mtaelewana. . .!
 
Pheeewwww! Mambo ya wazazi mdogo wangu ni magumu sana. Yalinitokea mimi miaka michache iliyopita tena wakiwa watu wazima kweli na wajukuu! Baba akasambaratisha mji mama akakimbilia kwaoooo miaka 2. Kila nilipofuatwa nilisema siingilii, hiyo ni ndoa yao kama wameamua kujitesa na kujiaibisha na kufanya nyumbani pasiwe mahali pa sie kufurahia kuwatembelea ni wao. Nilikaa kimya kabisa! Sikuingilia hata kidogo hata mama aliponipigia simu mara moja moja kutoa mashitaka, nilimsikiliza kwa makini kweli but baada ya kukata simu sikufanya lolote zaidi ya kuwaombea tu. Na baba aliponipigia simu kutoa mashitaka kuhusu mama nilimsikiliza kwa makini kweli, lakini baada ya kukata simu nilikaa kimyaaa!

Walipochoka kutesana na kucheza hiyo sinema yao ya uzeeni mama alirudi kwake na yupo hadi sasa. Siwezi kusema mambo yametengemaa kama zamani lakini wanaelewana na mji upo tena.

Hizo tabia za baba zetu ni kweli huwa zinatutisha sana kuolewa na mfano mimi, sikuwataka tena watu wa kutoka kwetu. Nilijiambia nafsi yangu, watakuwa kama baba yangu.... (mnisamehe wababa nasema ukweli toka moyoni). Sasa mdogo wangu, wewe muombe Mungu akusaidie, usimuone baba kama ndiye mkosaji sana, sometimes sisi tulifikia mahali tukamuona baba kama ana nafuu kuliko mama, na wakati mwingine tuliona kama baba mkosaji sana. Kwa hivyo, nakushauri kumwomba Mungu akupe mume mzuri atakayekupenda na kukufurahisha maisha yako yote na atakayejali familia, na wewe jiombee uje uwe mke mwema maana tunaomba waume wazuri na wema je, sisi wenyewe tukoje? Omba baraka za Mungu, na utaolewa tu ukikaa mkao wa kuolewa, usijifungie baraka ya ndoa.

Barikiwa.
 
Kingine mnaonaje nikiwashauri wazazi wangu kuachana, kweli nitakuwa nimefanya dhambi? Sijui cha kufanya, lakini neno la Mungu linasema kama kilicho tenganishwa na Mungu mwanadamu asikitenganishe.

Hapo kwenye Bold nyekundu sijaelewa kabisa......... hata sijui muandishi alikuwa na maana gani
 
Pheeewwww! Mambo ya wazazi mdogo wangu ni magumu sana. Yalinitokea mimi miaka michache iliyopita tena wakiwa watu wazima kweli na wajukuu! Baba akasambaratisha mji mama akakimbilia kwaoooo miaka 2. Kila nilipofuatwa nilisema siingilii, hiyo ni ndoa yao kama wameamua kujitesa na kujiaibisha na kufanya nyumbani pasiwe mahali pa sie kufurahia kuwatembelea ni wao. Nilikaa kimya kabisa! Sikuingilia hata kidogo hata mama aliponipigia simu mara moja moja kutoa mashitaka, nilimsikiliza kwa makini kweli but baada ya kukata simu sikufanya lolote zaidi ya kuwaombea tu. Na baba aliponipigia simu kutoa mashitaka kuhusu mama nilimsikiliza kwa makini kweli, lakini baada ya kukata simu nilikaa kimyaaa!

Walipochoka kutesana na kucheza hiyo sinema yao ya uzeeni mama alirudi kwake na yupo hadi sasa. Siwezi kusema mambo yametengemaa kama zamani lakini wanaelewana na mji upo tena.

Hizo tabia za baba zetu ni kweli huwa zinatutisha sana kuolewa na mfano mimi, sikuwataka tena watu wa kutoka kwetu. Nilijiambia nafsi yangu, watakuwa kama baba yangu.... (mnisamehe wababa nasema ukweli toka moyoni). Sasa mdogo wangu, wewe muombe Mungu akusaidie, usimuone baba kama ndiye mkosaji sana, sometimes sisi tulifikia mahali tukamuona baba kama ana nafuu kuliko mama, na wakati mwingine tuliona kama baba mkosaji sana. Kwa hivyo, nakushauri kumwomba Mungu akupe mume mzuri atakayekupenda na kukufurahisha maisha yako yote na atakayejali familia, na wewe jiombee uje uwe mke mwema maana tunaomba waume wazuri na wema je, sisi wenyewe tukoje? Omba baraka za Mungu, na utaolewa tu ukikaa mkao wa kuolewa, usijifungie baraka ya ndoa.

Barikiwa.
Well said penye red, Mungu anasikiliza maombi. Mimi binafsi nimepewa mwanamke wa ndoto zangu baada ya maombi ninaye kwa miaka minane sasa. Nikisafiri au yeye akisafiri kwa siku chache tuu maisha yangu huwa magumu sana, sembuse kuachana!!!!!!!!!!!
 
baba kwa muda huu anapuyanga nje, mama naye anapuyanga nje, mwisho wote wataleta maradhi ndani. kama ni makosa ya kusameheana na wafanye hivyo kama ni magumu wewe waache si kila mtu ana akili zake.

kuhusu wewe wala usijali MUNGU alishakupangia maisha yako toka dunia inaumbwa ni wewe kumkumbusha tu kwa njia ya maombi.
 
Ugomvi wa baba na mama achana nao usiuingilie kabisa hujui baba yako alicho mfanyia mama yako na wala haujui mama alichomfanyia baba na wala uctake kujua kwasababu unaweza usitamani hata kuingia kwenye ndoa
 
Jitahidi uwe kiungo kipatanishi kati ya baba na mama. Piga magoti ukasali, ikiwezeka ufunge kwa ajili ya hilo.
 
Wengi tumepitia kwa hayo maisha.. Hakuna anayependa..kuona wazazi wakigombana ..lakini hakuna jinsi kwani wao ni wanadamu....

Ushauri wangu.. Uchukua worse scenario (yaani wazazi wanaachana) na uifanyie kazi..Yaani nyinyi watoto mtayumba vipi kiuchumi, masomo etc.. (hasa kama binafsi bado hujaanza kujitegemea) Washirikishe wakubwa na kuhakikisha mnapata haki zenu kama watoto ..hasa matunzo..

Siri ya mafanikio yako 1. "usijihusishe kabisa wala kushiriki ugomvi wa wazazi".. 2. Kwa sababu wewe ni binti..kumbuka wanaume wote sio kama yule usiyempenda.
 
Pheeewwww! Mambo ya wazazi mdogo wangu ni magumu sana. Yalinitokea mimi miaka michache iliyopita tena wakiwa watu wazima kweli na wajukuu! Baba akasambaratisha mji mama akakimbilia kwaoooo miaka 2. Kila nilipofuatwa nilisema siingilii, hiyo ni ndoa yao kama wameamua kujitesa na kujiaibisha na kufanya nyumbani pasiwe mahali pa sie kufurahia kuwatembelea ni wao. Nilikaa kimya kabisa! Sikuingilia hata kidogo hata mama aliponipigia simu mara moja moja kutoa mashitaka, nilimsikiliza kwa makini kweli but baada ya kukata simu sikufanya lolote zaidi ya kuwaombea tu. Na baba aliponipigia simu kutoa mashitaka kuhusu mama nilimsikiliza kwa makini kweli, lakini baada ya kukata simu nilikaa kimyaaa!

Walipochoka kutesana na kucheza hiyo sinema yao ya uzeeni mama alirudi kwake na yupo hadi sasa. Siwezi kusema mambo yametengemaa kama zamani lakini wanaelewana na mji upo tena.

Hizo tabia za baba zetu ni kweli huwa zinatutisha sana kuolewa na mfano mimi, sikuwataka tena watu wa kutoka kwetu. Nilijiambia nafsi yangu, watakuwa kama baba yangu.... (mnisamehe wababa nasema ukweli toka moyoni). Sasa mdogo wangu, wewe muombe Mungu akusaidie, usimuone baba kama ndiye mkosaji sana, sometimes sisi tulifikia mahali tukamuona baba kama ana nafuu kuliko mama, na wakati mwingine tuliona kama baba mkosaji sana. Kwa hivyo, nakushauri kumwomba Mungu akupe mume mzuri atakayekupenda na kukufurahisha maisha yako yote na atakayejali familia, na wewe jiombee uje uwe mke mwema maana tunaomba waume wazuri na wema je, sisi wenyewe tukoje? Omba baraka za Mungu, na utaolewa tu ukikaa mkao wa kuolewa, usijifungie baraka ya ndoa.

Barikiwa.

Ushauri ulompa ni mzuri kazi kwake kuufuata ili siku moja ujetimiza malengo yako yakuunganisha wazazi wako pamoja na kupata mume mwema. Pia na wewe jitahidi uwe mwema sio ukute mambo yako sio alafu unataka mume mwema. God bless u na akuongoze ktk kukabiliana na mtihani huu mgumu
 
Hapo kwenye Bold nyekundu sijaelewa kabisa......... hata sijui muandishi alikuwa na maana gani

hiyo ni comfusition kidogo nadhani alikuwa akimaanisha ALICHOUNGANISHA MUNGU MWANADAMU HAWEZI TENGANISHA
 
Mungu akutie nguvu ili uweze kuendelea kuwaombea wazazi. Hizo ni hila za shetani kusambaratisha ndoa ili na familia nzima isambaratike. Pia epuka kujinenea mabaya (Mf. Hivi nitakuja kuoelwa kweli?) Kumbuka kinywa huumba. Mungu akutie nguvu.
 
Kuna ndoa moja ilikua na mgogoro wa miaka nenda miaka rudi Mungu anisamehe walipoachana nilishukuru sababu hiyo ndio ilikuwa wish yangu. Nilikua na wasiwasi huenda mmoja wao anaweza muua mwenzake siku moja kwa hasira/wivu wa kimapenzi ama mmoja wapo anaweza kujiua kwa frustration. Wameachana lakini sasa roho inaniuma jinsi kila mmoja wao anavoishi maisha ya upweke na kuhangaika. But naona hii ni afadhali kuliko kipindi walipokua wakiwa pamoja
 
Back
Top Bottom