Felixonfellix
JF-Expert Member
- Feb 16, 2010
- 1,672
- 182
Tushirikiane kumshauri mtu huyu jamani:
Naomba ndugu muniombee niko kwenye majaribu makubwa hadi inafika wakati najisikia sina hata nguvu ya kuomba. Mara kwa mara huwa najiuliza kama kweli Mungu yuko karibu nami. Lakini naamini siku moja Mungu atanikumbuka.
Cha kwanza naomba muniombee, wazazi wangu wanataka ku-divorce, yaani baba yangu alishatuacha nyumbani mimi na wadogo zangu na mama yangu. Sasa wazazi hawasikilizani na wanataka ku-divorce. Mimi nimejaribu kuwaombea muda mrefu na kuwashauri lakini hawanisikii, nami kwa hivyo nimeshachoka na sijui nifanye nini.
Kingine mnaonaje nikiwashauri wazazi wangu kuachana, kweli nitakuwa nimefanya dhambi? Sijui cha kufanya, lakini neno la Mungu linasema kama kilichounganishwa na Mungu mwanadamu asikitenganishe. Naomba mnisaidie hapo!
Cha tatu naomba mnisaidie kuomba ili nipate mume mwema kutoka kwa Mungu kwa sababu mara nyingi naogopaga nasema labda sitakuja kuolewa. Sababu ni kuwa mambo ninayoyaona kwa wazazi wangu yananiogopesha sana hadi nakata tamaa, najiuliza hivi nikipata mume ambaye hatusikilizani hali itakuwa ya namna gani?.
Jamani nawaombeni mnisadie sana kwa maombi na ushauri.
Naitwa -------------- na nina miaka 25.
Mungu awabariki sana!
Naomba ndugu muniombee niko kwenye majaribu makubwa hadi inafika wakati najisikia sina hata nguvu ya kuomba. Mara kwa mara huwa najiuliza kama kweli Mungu yuko karibu nami. Lakini naamini siku moja Mungu atanikumbuka.
Cha kwanza naomba muniombee, wazazi wangu wanataka ku-divorce, yaani baba yangu alishatuacha nyumbani mimi na wadogo zangu na mama yangu. Sasa wazazi hawasikilizani na wanataka ku-divorce. Mimi nimejaribu kuwaombea muda mrefu na kuwashauri lakini hawanisikii, nami kwa hivyo nimeshachoka na sijui nifanye nini.
Kingine mnaonaje nikiwashauri wazazi wangu kuachana, kweli nitakuwa nimefanya dhambi? Sijui cha kufanya, lakini neno la Mungu linasema kama kilichounganishwa na Mungu mwanadamu asikitenganishe. Naomba mnisaidie hapo!
Cha tatu naomba mnisaidie kuomba ili nipate mume mwema kutoka kwa Mungu kwa sababu mara nyingi naogopaga nasema labda sitakuja kuolewa. Sababu ni kuwa mambo ninayoyaona kwa wazazi wangu yananiogopesha sana hadi nakata tamaa, najiuliza hivi nikipata mume ambaye hatusikilizani hali itakuwa ya namna gani?.
Jamani nawaombeni mnisadie sana kwa maombi na ushauri.
Naitwa -------------- na nina miaka 25.
Mungu awabariki sana!