Wazazi wanajitoa sana kuhajikisha watoto wanapata mahitaji yao ya kila siku

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Ninakumbuka miaka ya 1980 enzi zile Afrika ya Kusini siasa za ubaguzi wa rangi zimetamalaki. Nchi nyingi zilijitenga na Afrika ya Kusini, passport ya Tanzania iliandikwa kabisa hairuhusu mmiliki kuingia nchi hiyo

Jirani yetu Baba yao alifanikiwa kupata kazi Afrika ya Kusini kwenye migodi ya madini. Yule mzee alirudi kwa kujificha na alikaa wiki si zaidi ya wiki mbili. Aliondoka usiku

Familia yake waliweza kujenga nyumba yenye hadhi. Watoto walivaa raba mtoni na ada za shule walipata. Lakini kukua bila malezi ya baba nayo ni changamoto

wazazi wakisha pata watoto, wanajitoa sana kuhakikisha watoto wanapata mahitaji yao, ikiwemo kutengana na familia kwa muda mrefu
 
Hoja inakuwa je familia inatambua kujitoa huko? Watoto wakiwa wakubwa wanaelewa na kuthamini kuhitoa huko kwa wazazi kwamba ilikuwa kwa faida yao?
Mama huwa anakumbukwa siku zote ila baba kutokana na harakati za ujana, mazuri yake huwa yanamezwa na mabaya yake ila umuhimu wake unaonekana pale anapofariki mapema huku familia inamuhitaji kulipa hadi school fees
 
Hoja inakuwa je familia inatambua kujitoa huko? Watoto wakiwa wakubwa wanaelewa na kuthamini kuhitoa huko kwa wazazi kwamba ilikuwa kwa faida yao?
Hata siku moja! Watoto watalaumu baba kuwa aliwatupa hasa akirudi amekongoroka kwa vumbi la mgodi na hana pesa maana alikuwa anazituma nyumbani
 
Sasa hapo usiombee baba na mama wakatengana then
Ukakuta mama ni bichwa box
Ataanza kuwalisha sumu watoto kuwa baba yao ni mtu mbaya aliwa telekeza na kila aina ya uongo "

Wakati kumbe baba yao alipitia magumu mengi sana ili kuhakikisha watoto wanapata mahitaji yote ya msingi na yalazima
 
Mzee unahangaika ughaibuni huko kwenye migodi kifo njenje ili mradi watoto wale wavae ,mama apendeze Mara kifusi kiwafukie mkae chini siku tatu mle mijusi tu na maji machafu


Halafu mtoto unakua kabisa unakuja kusema "ni nani kama mama "
 
Wazazi hupambana hta ikiwa watoto ni kumi, balaa linageuka pale mzazi ikitokea ameishiwa au amefilisika lakini alifanikiwa kusomesha ajabu watoto wrote hao huwa wanashindwa kumhudumia mzazi mmoja tu
 
Back
Top Bottom