Wazazi wameniharibia maisha nazidi kulaani

OME123

JF-Expert Member
Oct 4, 2010
1,498
605
Wazazi wangu hawataki nioe mchagaa wakati ndo nampenda,wanataka nioe tofauti na mchagaa (mmarangu)wakati nampenda sana huyu msichana kwani anasifa zote za kuwa mke.Na ukizingatia umri wangu wa kuoa na sifa zote za kuwa na familia ndo imetimia
 
Mpendwa kuna mambo mawili
1. Uliza kwa nini wanamkataa. Wazazi ni Mungu wa pili. Huwa wanaona mbali. Ukishajua pima.
2. Kama sababu zao hazina msingi mzuri, basi funga na kuomba wamkubali. Maana hata Biblia inasema mengine hayawezekaniki pasipo kufunga na kuomba.
 
mkuu lazimisha ila jua likukutokea ujue namna ya kusimama mwenyewe.. pili waulize kwa nini hawataki mchaga.. ila hutupendi ujinga wakulundikana ndani bila sababu hasa kama huna la kufanya.. karibu marangu mkuu sisi wanawake wazuri tunafaa kuwa mke
 
Ukilazimisha kuoa huyo utaweshangaa wazazi watatumia changamoto utazokumbana nazo wakuprove kwamba ulikosea kuchagua na uliambiwa hukisikia.Wakati ki uhalisia maisha ya ndo yanachangamoto zake haijalishi umeoa kabila gani.
 
Wanakukataza kumuoa sababu wanamjua vizuri yeye pamoja na ukoo wao au wanakukataza tu basi kwa sababu ya dhana kuwa wachaga sio wa kuoa?

Maisha yamebadilika sana kaka, siku hizi kila kabila lina mshamba, lina vilaza, lina wachawi, lina wajanja, lina wife material........ ni more individual siku hizi kuliko ile nadharia ya kuaminishana kuwa baadhi ya makabila hayafai kuoa na mengine yanafaa.

Sikiliza moyo wako full stop, tusitishane bana
 
Mpendwa kuna mambo mawili
1. Uliza kwa nini wanamkataa. Wazazi ni Mungu wa pili. Huwa wanaona mbali. Ukishajua pima.
2. Kama sababu zao hazina msingi mzuri, basi funga na kuomba wamkubali. Maana hata Biblia inasema mengine hayawezekaniki pasipo kufunga na kuomba.
hakuna mungu wa pili bali mungu ni mmoja aliye pekee isipokuwa tumeambia tuwatii wazazi
 
Unalalamika kuambiwa usimwoe mchaga wakati hata nikipewa bure mchaga, niongezewe pembe za faru John, na kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa taanesko bado ntamkataa huyo mchaga na vyote walivyoniongezea.
 
ngoja niseme kitu humu jf kuna wazaz madingi kabisa hiv inakuaje kila kitu unataka useme ndo kijana wako afate maana wamekuwa wa kwanza kuharibu future za watoto wao na kuanza kukimbilia kwa waganga kwa hili wazaz mbadilike tena sana mwingine unakuta hana uwezo kabisa lakin ni mtoto wake mwenyew anashindwa kumsaidia ila akisikia fulani hana oa au kuolewa mbio kutoa mchango ata kama laki moja na hali tuliyonayo hii ya mpito wew mzaz unakuta umesoma udaktar unalazimisha na mwanao awe daktali uku ukijua kipaji cha mtoto wako ni fasion u miss na usanii ama mambo ya biashara unajua jiulize wewe mzaz baba ako alikuwa daktali kama wewe si alikuwa mkulima tu pale uyole miaka 60 blood ful wazee msiojielewa na hakuna laana ya mbaya kwenu.....
 
nimesoma comment zenu kwa kweli hata nikioa kabila lingine amani ya moyo sitokuwa nayo milele.huyo mchagaa ndo nampenda.japo wao wamesema kma nitamuoa mke wa pili ni sawa.mi ni msukuma wa Mwanza.Nae binti amekataa suala la kuolewa mke wa pili
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom