Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,778
- 59,133
- Thread starter
- #41
Asante sana Mtende kwa mchango wako. Umegusia vitu vya msingi sana.Kiukweli vifo vya hao watoto viliniumiza sana, nilijikuta nina maswali mengi sana kichwani
Sijawahi kuwaza kuwapeleka wanangu boarding hata siku moja, pamoja na changamoto za wasaidizi wa kazi, wakati mwingine inafika wakati unakata tamaa kabisa lakini ni bora kusacrifice kazi yangu for the sake of the kids na sio kuwapeleka boarding
Kwa umri huo ni muda ambao watoto bado wanahitaji foundation kubwa sana kutoka kwa wazazi wote wawili, wanahitaji pia upendo na ukaribu na mzazi na pia inasaidia hata kujenga bond kati ya mzazi na mtoto
Ni umri ambao mtoto yupo katika stage ya kujifunza, kwa hiyo mengi anayojifunza anaangalia kutoka kwa walezi na hapa ndio mantiki ya wazazi inapokuja...naamini kila mzazi kuna namna ambayo anatamani amlee mtoto/watoto wake na kuna makuzi ambayo hatamani kumuona mtoto wake ameyapata especially baqdhi ya tabia ambazo baadae zinaweza kusababisha mtoto kuwa kiumbe wa hovyo, kwa hiyo umri huu ni wa kumtengeneza sana mtoto
Nawaza tu hao wanaokua boarding, wanajifunza mengi sana mazuri na mabaya, wanajifunza kutoka kwenye backgroubd za kila aina maaana kuna mchanganyiko wa watu wengi, sijui hata kama kuna ile upendo ambao angetakiwa kuupata kwa mzazi, wakati mwingine mtoto hata anapokua na jambo, sijui huwa anamweleza nani, either mwalimu au wanafunzi wengine?
Mimi nadhani serikali ingebadilisha tu huu utaratibu wa watoto wa shule za msingi kukaa boarding na sheria iwekwe ili wazazi waweze kuwajibika katika malezi ya watoto la sivyo tutatengeneza taifa lenye watu wa hovyo, irresponsible citizens kwa sababu wamekua katika mazingira ambayo wazazi wao hawakua respinsible kwenye malezi yao na hakujifunza kutoka kwao
Mzazi anapata kabisa usingizi mtoto wake wa miaka 4 yupo boarding, hujui amekula, ameoga, anajisikiaje, tena mama ameingia leba kabisaa
Ukweli ni kwamba our society is more dysfunctional than we would like to admit. Kuna umuhimu wa serikali pamoja na taasisi nyinginezo kutoa elimu kuhusu hasara za muda mrefu zinazoweza kusababishwa na "sifa" tunazokimbilia sasa hivi, pia kushinikiza uwajibikaji wa wazazi kwa watoto. Haya ndo maswala wataalam wa maswala ya kijamii wanatakiwa kuzungumzia but hola😏
I hope baadhi ya wazazi watafunguka macho ama kupunguza ubinafsi kadri kutokana na taarifa kama hizi.