Wazazi/Walezi: Makuzi na malezi ya watoto

naina19

JF-Expert Member
Oct 8, 2019
294
510
Habari za leo wakuu

Natumaini ni furaha ya kila mzazi au mlezi mwenye nia njema kumuona mtoto anakua katika kile anachokiamini.

Kwa nchi nyingi za kiafrika na Tanzania ikiwemo kumekuwa na desturi, mazoea au tabia ya kuwekeza mafunzo mengi, ulinzi, ukaribu kwa mtoto wa kike zaidi ya mtoto wa kiume.

Kwa miaka mingi sasa pia kumekuwa na mashirika pamoja na uhamasishaji mkubwa katika kumsaidia mtoto wa kike na wanawake huku mtoto wa kiume akiachwa akue akijifunza kwa jamii inayomzunguka tu bila kujali kama anapata kinachotakiwa na kwa usahihi.

Wazazi tunachokifanya kwa mabinti zetu sio kibaya ila tujue tunatengeneza gap kubwa kati yao na vijana wetu wa kiume. Tunakuwa na idadi kubwa ya mabinti wanaoelewa majukumu yao kijamii na vijana wa kiume wasioelewa majukumu yao japo yale ya asili.

Nadhani huu ni muda sahihi kwetu wazazi na jamii kwa ujumla ikiwepo taasisi mbalimbali (haswa zile za dini na elimu) kuliangalia hili upya kwani kwa kufanya hivyo inaweza kusaidia kupunguza matatizo mengi sana yanayoweza kutokea baadae haswa pale vijana wanapokuja kuingia kwenye majukumu ya ndoa.
 
Mkuu kuna vitu vingi tunakosea. Tunaweza kuona tunamsaidia mtoto wa kike lakini tukawa tunamwondoa mtoto wa kiume kwenye nafasi yake.
Halafu mbeleni asipojua anatakiwa kufanya nini tunalaumu.
Tuangalie tunapokosea na tusahihishe kabla hapajaharibika
 
Mkuu kuna vitu vingi tunakosea. Tunaweza kuona tunamsaidia mtoto wa kike lakini tukawa tunamwondoa mtoto wa kiume kwenye nafasi yake.
Halafu mbeleni asipojua anatakiwa kufanya nini tunalaumu.
Tuangalie tunapokosea na tusahihishe kabla hapajaharibika
Upo very collect.
Ni wazi jamii yetu, inahitaji nguvu ya ziada kwa lengo wa kuijenga tena upya.

Binafsi nafarijika sana, ninapoona mwanamama kama wewe...unaweza ukasimama kidete na kuongea hayo. Ilihali kundi kubwa la jamii zetu, limelala usingizi mzito, kwenye kitanda cha utandawazi.

Hakika unastaili pongezi kwa hili, hongera sana mama. Naomba tuendelee kuwa pamoja, ili tukomboe jamii zetu.....kutoka katika huu utandawazi haribifu.

Asante sana.
 
Upo very collect.
Ni wazi jamii yetu, inahitaji nguvu ya ziada kwa lengo wa kuijenga tena upya.

Binafsi nafarijika sana, ninapoona mwanamama kama wewe...unaweza ukasimama kidete na kuongea hayo. Ilihali kundi kubwa la jamii zetu, limelala usingizi mzito, kwenye kitanda cha utandawazi.

Hakika unastaili pongezi kwa hili, hongera sana mama. Naomba tuendelee kuwa pamoja, ili tukomboe jamii zetu.....kutoka katika huu utandawazi haribifu.

Asante sana.
Pamoja mkuu
 
Back
Top Bottom