Wazazi wa lulu wanahusika katika haya mazito yaliyomkuta lulu

JATELO1

JF-Expert Member
Oct 31, 2011
1,230
301
Mimi naamini kabisa kwamba Lulu siyo wa kulaumiwa kwa haya yanayomkuta sasa na badala yake WAZAZI WAKE kama anao ndiyo watu wa kwanza wa kulaumiwa kwa huyu mtoto-Lulu. Wazazi wa Lulu hawakuwa wazazi wazuri kwa mtoto wao, kwani uhuru alioachiwa huyu mtoto mpaka sasa haya makubwa yanamkuta ni mbaya sana na ndiyo umesababisha huyu mtoto AKAKUBUHU katika matendo na tabia chafu katika jamii. Wewe huyo mtoto kwa umri wake inasemekana ameshakuwa na uhusiano wa kimapenzi na watu mbalimbali wasiopungua 10 mpaka sasa, je hiyo kitu yake bado ina LADHA? hakika hiyo kitu yawezekana sasa haina ladha tena, na si ajabu viungo vingine navyo tayari havina usalama kwasasa kwani wanaume wa DSM wana maana? utafikiri wote wametokea Tanga, Zanzibar na Mombasa au Uarabuni wakati kuna wengine wabara kama mimi.


Huyo mtoto (Lulu) yaliyomkuta ni matokeo mabaya ya malezi ya watoto wa siku hizi kwa kisingizio cha uhuru na utandawazi. Nani kasema utandawazi haina rules and regulations? ndiyo maana sisi watanzania hasa viongozi wetu wamelazimika kuuza kila kitu kwa kisingizio cha Utandawazi bila kujali checks and balance ambazo kila nchi inatumia hasa pale inaporuhusu Foreign Direct Investment (FDI). Na kwa mantiki hiyo hiyo ya Utandawazi hata watoto wetu siku hizi hatuoni haja ya kuwakanya na kuwaelekeza yaliyo mazuri kwa ajili ya future zao. Ndiyo maana watoto wetu wanaanza ule mchezo mapema na matokeo yake huo mchezo unakuwa kama maji na damu katika viuongo vya mwanadamu.

Ndugu wana-JF; nasema haya siyo kwamba nafurahia yaliyomkuta huyu Lulu na hata Marehemu Kanumba, HAPANA naumia sana hasa ninapofikiria kwamba huyu mtoto Lulu kwa umri wake na yaliyomkuta, ni hakika NAFSI YAKE ITAMSUTA katika maisha yake yote hata kama ataachiwa huru katika kesi. Nasema hivi kwasababu huyu mtoto kwa yaliyomkuta sasa ya kuhusishwa na mauaji ya Kanumba na yale yote hasa ufuska ambao amekuwa akijishughulisha nao hata sasa amekuwa mzoefu ktk umri wa miaka 18 tu; ni HAKIKA NI MZIGO MZITO SANA UTAKAOMUUMIZA HUYU MTOTO. Je, tutegemee huyu binti arudi shule na kuweza kusoma kweli? Je huyu binti hizi picha za matukio mengi ya ajabu kama ya kunywa pombe na kuvaa nguo za kuvutia biashara zitaweza kumfanya aweze kuwa na mazingira chanya kwa ajili ya kusoma? itakuwa kazi ngumu sana.

Ndiyo maana mimi nawatupia lawama wazazi wake kwa kuchangia kumharibu binti yao, kwani hata mavazi anayovaa huyu mtoto siyo ya heshima hata kidogo na wazazi wake wanamwona na kila leo anatolewa kwenye magazeti akifanya mambo ya ajabu. Wewe mtot yule anatoka nyumbani kwao mapaja yote yako wazi akiulizwa eti yeye nguo ndefu zinamwasha, je hapa kuna ukweli gani? Je kama nguo ndefu zinamwasha na matiti mbona yako nje? Je na tumbo na kitovu? Hakika wazazi na familia yake yote wanawajibika kwa haya yanayomkuta Lulu sasa.

Naomba nimalizie kwa kuuliza maswali haya ili nisaidiwe majibu?
1. Je Lulu ana wazazi wake wote (baba na mama)?
2. Je, huko gerezani/police oysterbay kuna member yeyote amemwona? kama ndiyo, je mavazi gani amevaa huko? nauliza hili kwasababu ya aina ya mavazi anayovaa huyu mtoto ktk jamii.

Nawakilisha kwa ajili ya majadiliano. Pia ipo siku nitaandika kuhusu madhara yanayowakuta watoto ambao wazazi wao wanawapeleka nchi za nje hasa Ulaya na Marekani kusoma undergraduate degree wakati bado wako kwenye umri wa kutoweza kufanya maamuzi wao wenyewe kuhusu mambo mbalimbali.

RDI.
 
Ni suala la jamii kwa ujumla. Wazazi wa Lulu ni sehemu ya jamii inayobomoka kimaadili. Je wanaotembea na watoto wa shule wako sawa? Mind you wako wengi sana. Jamii ibadilike.
 
Back
Top Bottom