Wazazi msiwaambukize watoto wenu chuki dhidi ya wazazi wenzenu?

Lizzy, mimi naona wakati mwingi hii mbinu ya Mtorii inasaidia. Kuna dada namfahamu, pamoja na kuolewa, lakini hataki baba mtoto wake (ambaye ameshaoa) amchukue mtoto si kwa kusalimia wala nini. Na madai yake hataki mtoto wake akaishi na mama wa kambo. SIna tatizo na argument yake, lakini anafikia to the extent ya kumwambia baba mtoto kama anamtaka mtoto kumsalimia basi amchukue azunguke naye tuu, na siyo kumpeleka kwake jioni arudishwe. Watu wakamshika masikio mwanaume wakamwambia mtoto hagombaniwi, muda muafaka ukifika atakutafuta tu, cha msingi wewe kama ni ada lipa shuleni na achana na kukimbizana na mambo ya mtoto. Na kweli, imemletea amani mwanaume coz sasa hivi yeye ndiye anatumiwa ujumbe kuwa mtoto aje likizo? Kwa sababu hamna mtu wa kuendekeza drama alizokuwa anaziibua pale linapogusiwa suala la mtoto.

Kwa mtazamo wangu mie, hizi purukushani za wazazi wenza mwisho wake ni watoto ndio wanaoumia, coz ukimkuta baba kichaa anasusa kabisa hata kuhudumia huyo mtoto. Labda ukikuta na mama mtu anaweza kumhudumia mwenyewe.

Alitumia akili kwa kutotaka mashindano na mama mtu....ila hiyo ya kukataa mtoto alelewe na mama wa kambo hata mimi naisupport sana.Mtu uko hai mwanao analelewa na mtu mwingine...na ukifa je?!
 
Alitumia akili kwa kutotaka mashindano na mama mtu....ila hiyo ya kukataa mtoto alelewe na mama wa kambo hata mimi naisupport sana.Mtu uko hai mwanao analelewa na mtu mwingine...na ukifa je?!

Sawa, but not always. Unaweza kuzuia sana mtoto asilelewe NA mama wa kambo, but sio kulelewa KWA mama wa kambo. Fikiria circumstance kuwa wewe mama mtoto uko katika zingira (kazi, masomo, kwa mume mwingine) ambalo kwa vyovyote vile haliwezi kusuport basic needs za mtoto, kama kwa mama yake wa kambo?!
 
Sawa, but not always. Unaweza kuzuia sana mtoto asilelewe NA mama wa kambo, but sio kulelewa KWA mama wa kambo. Fikiria circumstance kuwa wewe mama mtoto uko katika zingira (kazi, masomo, kwa mume mwingine) ambalo kwa vyovyote vile haliwezi kusuport basic needs za mtoto, kama kwa mama yake wa kambo?!

We unabisha kwa maneno tu na sio kwasababu siku moja unaeeza ukajikuta unatakiwa kufanya maamuzi magumu sana....assuming you are not a woman/mother!
 
Watoto wenyewe pia huwa wana kawaida ya kumchukia mzazi wao asiyeishi nae, na huwa wanajiuliza maswali mengi sanasana, kwanza wenzao wakienda beach wako na baba na mama kwa nini sisi, vikao vya shule ni mama, mbona wenzetu wanakuja baba zao?

Usiku tupo na mama na mama ndiye anayehakikisha tumelala salama huyu baba yuko wapi? Chuki inaanzia hapo sasa bila mama kutia neno, mie nimeshuhudia mtoto wa dada wa shosti angu baba yake akienda kuwatembelea anajifungia mlango chumbani kabisa, na mama ake hadi anamchapa atoke akamsalimie baba yake lakini mtoto hataki kabisa.

Na huyu kafundishwa na nani? vitu vingine ni nature tu.
 
Alitumia akili kwa kutotaka mashindano na mama mtu....ila hiyo ya kukataa mtoto alelewe na mama wa kambo hata mimi naisupport sana.Mtu uko hai mwanao analelewa na mtu mwingine...na ukifa je?!

Tatizo huwa linakuja kwa malezi ya mtoto mwenyewe, kwa sababu kama hao angalau baba anakazana mwanae asome shule nzuri. Sasa huyo dada naye ameshaolewa na watoto wake kwa mumewe wanasoma shule za kawaida tu. Huoni hapo inaleta gap ya hao watoto wenyewe? Na umpate mume muelewa, akiwa nae hamne hamne hamchelewi kuzuliana ugomvi wenyewe kwa wenyewe kisa mtoto!
 
Back
Top Bottom