Wazazi kuweni makini na bodaboda wanaowapelekea watoto wenu shule

Fall Army Worm

JF-Expert Member
Jan 8, 2015
19,317
14,233
Poleni na majukumu yenu ya kulijenga Taifa Wazazi wenzangu!

Kama mada inavyojieleza, kuna huu utaratibu wa Wazazi kuwatumia Boda boda kuwapeleka Watoto wenu shule asubuhi na kisha jioni kuwarudisha nyumbani. Ndugu zangu muwe makini nao katika suala zima la usalama hasa namna ya uendeshaji wa pikipiki hata kama mnawaamini lkn chunguzeni spidi yao.

Leo asubuhi nimeona jamaa wawili Bodaboda wakiwapeleka Watoto shule kwa spidi kali, huyu wa kwanza amembeba mtoto wa kike, umri kama miaka mitano amevaa hijabu amempakiza nyuma, spidi anayoenda nayo kwakweli sijapendezewa nayo. Wa pili amebeba mtoto wa kiume, huyu amempakia mtoto kwenye mbele ya tanki la pikipiki na anakimbia sana hivyo anaua Mapafu ya yule mtoto. Kwakweli nimemhurumia sana yule mtoto.

Kwahiyo wazazi wenzangu kazi kwenu, usipomlinda mtoto wako nani wa kumthamini??.
 
Kuna sheria ilitungwa kuwalinda watoto na usafiri wa bodaboda. Sijui hata kama iko enforced au imeishia tu kwenye makaratasi.

Jirani yangu ana kisichana kibonge kweli; saa 11 asb kuna bodaboda inamfuata na kumrudisha jioni kizani. Huwa nashindwa kuelewa kama mzazi unawezaje kumwamini mtu kwa kiwango hicho kwa mwanao hususan binti unayempenda? Yaani hainiingii akilini kabisa!

Shule za boarding zimesaidia sana tulio wengi!
 
Inatakiwa Asubuhi unakamata Binti yako unaweka Begani unampeleka shule huku ukimpigia story zenye akili kisha unarudi ukikimbia mchakamchaka..... Jioni Mama atakwenda kumrudisha ama uende mwenyewe......mtoto wa kike anapaswa kulindwa kwa manufaa ya vizazi vijavyo

Binti kama huyo hawezi kukuletea mkwe legelege usiyefanana nae.
 
Hili ni tatizo la Serikali ingeondoa ushuru kwenye school van magari ya shule, ili bei ya kusafirisha watoto wa shule ipungue sana. Wazazi wengi wanapenda watoto wao wapande magari ya shule ila hawana pesa ya ada tena na ya usafiri.
 
40 Reactions
Reply
Back
Top Bottom