Wazazi hasa wa kike tuwe makini na wasichana wa kazi

jje's

JF-Expert Member
Sep 3, 2014
10,752
16,364
Kuna story moja ya kweli kabisa binti wa kazi/beki tatu alikuwa anamnywesha mtoto wa bosi wake viroba. Ni hivi mabosi ni wafanyakazi hivyo binti alikuwa akibaki home na mtoto peke yake.

Baada ya muda alipata rafiki wa kiume na wakaanza relationship. Kwa kuwa mtoto alikuwa ni kikwazo aliamua awe ananunua viroba (pombe) ili awe anachanganya na maziwa mtoto anywe alewe alale.

Majirani waligunduga tabia aya binti huyo ya kumuacha mtoto ndani kila siku na kwenda kwa wanaume wakaamua kumweleza mama wa mtoto ambaye aliamua kuweka mtego.

Aliaga kama kawaida anaenda kazini na baada ya muda alirudi na kukuta binti akimpa maziwa mtoto aliomba amsaidie kumnywesha mtoto maziwa ndipo alipogundua kuwa kuna tofauti kwani kila akimnywesha maziwa mtoto anakunja uso, akacheki ka yana moto sana lakini wapi ile aliposogolea kidogo akakutana na harufu ya viroba.

Ilibidi achukue hatua ya kumpiga sana binti ndipo alipotoa siri kuwa huwa hufanya hivyo ili mtoto alale naye afanye mambo yake na alielekezwa na mpenzi wake. Cha kusikitisha hapa sio kiroba bali alipojaribu kumpeleka mtoto hospitali kucheki afya yake aliaambiwa ubongo wa mtoto umeshaharibika.

Hivyo nawasihi wazazi wote kike/kiume tuwe makini sana na beki tatu na tupende kufuatilia maendeleo ya watoto wetu.

Tumefika mahali tunajisahau kabisa majukumu yetu na kuwaachia mabeki tatu bila kujua madhara yake.

Wote kwa pamoja tuchukue hatua na tutekeleze haya.
 
Kwa staili hii watakuja kuwanyea hata mdomoni wawadanganye ni keki Hawa sio watu
 
Kwa staili hii watakuja kuwanyea hata mdomoni wawadanganye ni keki Hawa sio watu
hiyo inaweza ikawa ishatokea ni kwa vile tu hatujaona au kusikia.
Tunachotakiwa kuchukua tahadhari tuwapende mabeki tatu kama watoto wetu wa kuwazaa. tukifanya hivyo hata kama anashawishiwa kumdhuru ule upendo wetu kwao unachukua nafas na wanaghairi walichokuwa wanadhamiria kufanya.
 
Kweli tuwe makini tuangalie msichana tunae mwajiri na mahusiano pande zote ni muhimu.
 
hiyo inaweza ikawa ishatokea ni kwa vile tu hatujaona au kusikia.
Tunachotakiwa kuchukua tahadhari tuwapende mabeki tatu kama watoto wetu wa kuwazaa. tukifanya hivyo hata kama anashawishiwa kumdhuru ule upendo wetu kwao unachukua nafas na wanaghairi walichokuwa wanadhamiria kufanya.
Hamna mkuu kwa matukio ambayo wafanya kaz wa ndani wanayoyafanya uwaga ni ya kinyama sana ssa cjui huwa wanalipiza kisasi hata celew japo ckatai kuna baadhi wana roho ya utu
 
Kweli tuwe makini tuangalie msichana tunae mwajiri na mahusiano pande zote ni muhimu.
Tatizo kwa watu ambao mke na mume wote wanafanya kazi ni ngumu sana kukaa na msichana wakamtathmini. Maana unapata msichana leo jioni kesho unamwachia nyumba.
 
Jje's ww ndio umeongea point, utakuta mtu kamleta mtoto wa watu kuja kumtunzia familia kwa maana ya watoto na nyumba na mambo mbalimbali ya home, lkn cha ajabu anasahau kuwa hilo jukum ni kubwa mno na inapaswa wewe kama bosi umjali pia.

Asee kutunza watoto na shughuri nyingine za domestic si kazi rahisi inahitaji upendo, uhuru, heshima n.k. Sasa bosi anamfanya beki tatu kama mbwa wake anategemea nini
kwa watoto wako.

Naona wengi mnachangia kwa hasira bila kuangalia tatizo ni ninina mkatimiza wajibu wenu, la sivyo watoto hata unga watapewa.
 
Tatizo kwa watu ambao mke na mume wote wanafanya kazi ni ngumu sana kukaa na msichana wakamtathmini. Maana unapata msichana leo jioni kesho unamwachia nyumba.
Ni changamoto kwakweli,tunahangaika kutafuta pesa ili familia zetu ziwe katika hali nzuri lakini wakati huo tunasahau au kuzidiwa kwenye mihangaiko yetu.

Na bila kubalance kotekote upande mmoja lazima upwaye haswa hili la familia. Mume na mke ni wajibu kuweka mambo sawa kuhakikisha familia inakaa vema
 
Back
Top Bottom