Wazazi 17,000 kuanza kusakwa watoto kukacha kidato cha kwanza

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Serikali ya Mkoa wa Mtwara imesema itaanza kuwasaka wazazi ambao watoto wao wameshindwa kuripoti shuleni kuanza kidato cha kwanza mwaka huu.

Wanafunzi hao wa kidato cha kwanza wameshindwa kuripoti shuleni, huku idadi ya waliofaulu ni zaidi ya 20,000, hivyo serikali kuagiza wazazi wote waliogoma kupeleka watoto shuleni kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa, alitoa agizo hilo baada ya kufanya ziara katika Manispaa ya Mtwara Mikindani na kukuta wanafunzi wa kidato cha kwanza zaidi ya 3,000 hawajaripoti shuleni.

Amesema matarajio ya mkoa ni watoto 20,400 na ndiyo waliyofaulu mtihani wa darasa la saba na kutakiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.

Alisema hali hiyo haiwezi kuvumiliwa na kusisitiza kuwa tangu shule zifunguliwe zaidi ya wiki tatu, lakini wanafunzi wa kidato cha kwanza walioripoti shule maudhurio hayaridhishi.

Alisema asilimia 75 ya wanafunzi hao hawajaripoti shule na kusisitiza ifikapo Jumatatu ijayo, wazazi wote waliogoma kupeleka watoto shule sheria ichukue mkondo wake dhidi yao, huku akisisitiza nia ya serikali ya kutoa elimu bure ni kuona kila Mtanzania anapata elimu ya msingi na sekondari.

Byakanwa ameshawaagiza wa vijiji, vitongoji na mitaa kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi kuhakikisha wazazi hao wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Kwa upande wake Ofisa Elimu wa Mkoa wa Mtwara, Germana Mng’aho, alisema takwimu zilizokusanywa na ofisi ya elimu mkoa inaonyesha kuwa hadi Januari 17, mwaka huu watoto walioripoti shule hasa sekondari ni wachache.

Alisema ofisi yake imejipanga kutoa ushirikiano ili kuhakikisha mchakato wa kuwafatilia watoto wote waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza, lakini hawajaripoti unafanikiwa.

Chanzo: IPP Media
 
SI WACHUKUE batch ya pili hao wengine waliogoma waachane nao

Hilo zoezi kwa mikoa mingine ni gumu sababu wengi wakifaulu hawaripoti kidato cha kwanza shule za serikali huenda shule za private kule waonekana watoro kumbe wamekwenda zao shule za private
 
Na Mwandishi wetu Mihambwe

Mkuu wa Mkoa Mtwara, Mhe. Gelasius Byakanwa amewaagiza Watendaji Kata na Vijiji kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani Wazazi na Walezi wote ambao hawajawapeleka Watoto shule mpaka sasa ambao wanaostahili kuanza darasa la kwanza na wale waliofaulu kidato cha kwanza.

Mhe. Byakanwa ameyasema hayo kwenye ziara ya siku aliyoifanya kwenye Tarafa ya Mihambwe ambapo alikuwa akikagua hali ya kuripoti Wanafunzi kidato cha kwanza pamoja na kukagua ujenzi wa miradi ya kimaendeleo kama vile Madarasa, Maabara pamoja na vyoo.

"Nawaagiza Watendaji Kata na Vijiji kuwakamata na kuwapeleka Mahakamani Wazazi na Walezi wote ambao wamekaidi utekelezaji wa kuwapeleka shule Watoto wao. Watakaokaidi kukamatwa Watendaji nijulisheni haraka, nitawashughulikia mwenyewe." Alisisitiza Mhe. Byakanwa.

Kwenye upande wa ujenzi wa miradi ya maendeleo, Mhe. Byakanwa ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo na kuvutiwa zaidi na utekelezaji wa kampeni aliyoianzisha ya ujenzi wa vyoo kwenye shule.

*"Nilikuwa naona mitandaoni leo nimejionea mwenyewe, nakupongeza sana Afisa Tarafa Mihambwe Shilatu kwa kazi nzuri unayoifanya ya kusimamia miradi ya kimaendeleo. Nimevutiwa zaidi na namna ulivyosimamia kampeni ya shule ni choo, kote nilipopita nimeona kazi kubwa iliyofanyika. Hongera sana Shilatu."* Alisema Mhe. Byakanwa alipokuwa akizungumza na Wazazi na Wananchi waliojitokeza Shule ya msingi Chikongo kilichopo Kijiji cha Chikongo kata ya Mkoreha wakati akihitimisha ziara yake ya siku moja alipotembelea Tarafa ya Mihambwe.

IMG_20200128_133152_316.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
SI WACHUKUE batch ya pili hao wengine waliogoma waachane nao

Hilo zoezi kwa mikoa mingine ni gumu sababu wengi wakifaulu hawaripoti kidato cha kwanza shule za serikali huenda shule za private kule waonekana watoro kumbe wamekwenda zao shule za private
Sio Kweli unachozungumza kwa mkoa wa mtwara. Wengi hawaendi izo private school

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom