Wazanzibari wapanga kufanya mandamano 1/4/2011 kisa wamechoshwa na Muungano

Status
Not open for further replies.

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
Sauti:Kongomano la katiba – 05 March 2011 | MZALENDO.NET
Wananchi, wazalendo, wapenda amani, maendeleo na utaifa wa nchi yetu ya Zanzibar.
Kufuatia mjadala wa Katiba Mpya unavyoendelea, mengi yamefichuliwa dhidi ya muungano wetu uliodumu kwa miaka 47. Pamoja na nia njema wakati wa kuasisiwa muungano wanchi mbili, Tanganyika na Zanzibar, kiukweli sasa hivi hali haiku hivyo.
Tumeshuhudia wanansheria wetu, mara kwa mara, wamekuwa wakitoa dosari zao zinazoonyesha kupotea kwa nia njema iliyokusudiwa. Miongozi mwao ni pamoja na kutamka bayana kuwa muungano huu kisheria haipo tena, kilichobaki ni kinadharia tu.
Hivyo basi, ni wakati wetu sote kwa pamoja kuungana katika kudai haki yetu kama raia watiifu kwa taifa letu pamoja na kudai haki za nchi yetu iliyopoteza haki zake kwa kufanya maandamano ya amani.
Madhumuni ya maandamano.
- Kudai muungano ujadiliwe upya na pande zote.
- Kuunga mkono matamko yanayotolewa na wanasheria wetu kwenye mjadala wa katiba.
- Kutoa muamsho kwa jamii na wananchi juu ya kutetea haki za nchi na taifa letu – Zanzibar.
Petition itakuwa na ujumbe ambao ni open letter itakayo beba ujumbe mmoja wa madai yetu kwa sehemu zote zitakazofanyika maandamano.
Siku ya Maandamano.
Maandamano yamepangwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 1/04/2011. Ijumaa ni siku ya mwisho wa wiki, itakuwa muafaka kwa Wazanzbibar wengi kuweza kushiriki. Vilevile itakuwa ni wiki nne kabla kufanyika sherehe za Muungano hapo 26/04/2011. Wale walioko makazini tunaomba waombe likizo zao mapema ili waweze kushiriki.
Eneo la Maandamano.
Maandamano yatafanyika ulimwengu mzima.
Kitovu cha maandamano haya kitakuwa ni ndani ya Zanzibar, ambapo Petition ya madai yetu itawasilishwa kwa Waziri wa Sheria na Katiba na Mwanasheria Mkuu wa SMZ.
Kwa wale walioko Tanzania Bara, wao watawasilisha Petition yao kwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa nchi nyengine dunia, Wazanzibar na Watanzania kwa jumla, watafanya maandamano kwa kila nchi yenye ubalozi wa Tanzania. Petition zitawasilishwa kwa mabalozi wa nchi husika ili kuziwasilisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambae wakati huohuo anakuwa Rais wa Shughuli za Serikali ya Tanganyika pamoja na Rais wa Zanzibar.
Yanayohitajika
Tunaomba ushirikiano kutoka kwa Wazanzibar wote ulimwenguni kufanikisha shughuli hii. Tunahitaji mawakala wa kusimamia kutoka kila nchi husika. Hii itasaidia kufikisha ujumbe kule tunakokusudia.
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nami kupitia email yangu ashakh@mzalendo.net
NOTE: Msisitizo unatiliwa kuwa haya ni maandamano ya amani, kwa lengo la kudai haki zetu.
 
mmmhhhh! Sio mchezo. Presha kila upande au ni watu tu kutafuta umaarufu!!!???
 
Wengine tunaandamana maisha magumu na ufisadi, wenzetu wanajadili Muungano tu.....

Hao ma Bwana zao huko Muscut wanaandamana kudai utawala bora.

Wao mchawi wao ni Muungano. Kaazi kwelikweli.

Wakivunja Muungano, NTAPIKA PILAU la NGUVU kusherehekea UKOMBOZI wa kwanza wa Tanganyika.

Ntasubiri wakianza kuzichapa Unguja na Pemba na mwisho Waarabu na Waswahili....... Hapo watakuja na kupiga magoti Tanganyika iwasaidie. Dawa hapo ni kuwaambia kuwa sasa MNAKUWA ki-MKOA na si Nchi.

LOOSER.
 
Mtammaliza JK mwaka huu jamani! Ngoja tuone kama maandamano hayo nako atadai kwamba yanahatarisha utulivu na amani!
 
Wengine tunaandamana maisha magumu na ufisadi, wenzetu wanajadili Muungano tu.....

Hao ma Bwana zao huko Muscut wanaandamana kudai utawala bora.

Wao mchawi wao ni Muungano. Kaazi kwelikweli.

Wakivunja Muungano, NTAPIKA PILAU la NGUVU kusherehekea UKOMBOZI wa kwanza wa Tanganyika.

Ntasubiri wakianza kuzichapa Unguja na Pemba na mwisho Waarabu na Waswahili....... Hapo watakuja na kupiga magoti Tanganyika iwasaidie. Dawa hapo ni kuwaambia kuwa sasa MNAKUWA ki-MKOA na si Nchi.

LOOSER.
TANGANYIKA nimekosa nini hata watu wangu wa tanganyika hawanidai wala hawanihitaji ?
 
Mbona wamepanga tarehe mbaya hii, au....??. Hivi 1/4 siyo ile siku ya kuingizana mjini?

Halafu eneo la Maandamano: Maandamano yatafanyika ulimwengu mzima.
Sijui taarifa za kiintelijensia za IGP Mwema atazidhibiti vipi zikipatikana.

Mabalaa yote yanamwangukia JK.
Kufa kwa CCM, kufa kwa Muungano, kufa kwa mfumo wa Mafisadi nk
 
abdulahsaf

Mumeshapata "kibali cha polisi"?

Na intelijensia inasemaje?

Mukifanikiwa ni jambo zuri...sio kupigishana kelele, kejeli na matusi kwenye mitandao.

All the best to all of you. Mukipata Zanzibar yenu, tutapata Tanganyika yetu.
 
Mataarisho yapoo na yanaendelea,haya sio maandamano ya siasa na ya wananchi wote kwa ujumla zanzibar,,,,,mungu akipenda yatakuwa ya amani,,,yatafanyika kila pembe ya dunia,siku ni nzuri sana wala sio mbaya kabisaa muda muafaka, Pia kuna hati za muungano feki tutaziorezesha kila Office ya UNITED Nation,,,,,tutazisambaza kila kona ya dunia.. tunaomba ushikiano wenu....mi pia naunga mkono,
 
Wengine tunaandamana maisha magumu na ufisadi, wenzetu wanajadili Muungano tu.....

Hao ma Bwana zao huko Muscut wanaandamana kudai utawala bora.

Wao mchawi wao ni Muungano. Kaazi kwelikweli.

Wakivunja Muungano, NTAPIKA PILAU la NGUVU kusherehekea UKOMBOZI wa kwanza wa Tanganyika.

Ntasubiri wakianza kuzichapa Unguja na Pemba na mwisho Waarabu na Waswahili....... Hapo watakuja na kupiga magoti Tanganyika iwasaidie. Dawa hapo ni kuwaambia kuwa sasa MNAKUWA ki-MKOA na si Nchi.

LOOSER.

Mkuu .
Kwanza, Si jambo jema kuwatukana watu wazima wenzako.

Pili mchango wako umejaa utata mwingi...unaitaka Tanganyika lakini unawaita "looser"

Utapika pilau lakini unawakejeli kuwambia waandamane kupinga ufisadi badala ya Muungano.

Unawambia wana "bwana zao mascut"...jamani lugha gani hii....
Tuwatie nguvu watende kwa vitendo ili tupate yetu au huitaki?

By the way tutakutana nao kwenye EAC, kama ndugu na washirika wa zamani. and life will go on!
 
Mkwere anashughuli mwaka huu, Bara maandamano ya ukali wa maisha, Znz maandamano ya kuhusu muungano kweli mkwere na ccm yake atapona hapo? Tunachohitaji ni Tanganyika yetu iwe na Maendeleo sio ufisadi mungu tujaale tupate uhuru kujitoa kwenye ukoloni wa ccm
 
Mataarisho yapoo na yanaendelea,haya sio maandamano ya siasa na ya wananchi wote kwa ujumla zanzibar,,,,,mungu akipenda yatakuwa ya amani,,,yatafanyika kila pembe ya dunia,siku ni nzuri sana wala sio mbaya kabisaa muda muafaka, Pia kuna hati za muungano feki tutaziorezesha kila Office ya UNITED Nation,,,,,tutazisambaza kila kona ya dunia.. tunaomba ushikiano wenu....mi pia naunga mkono,

ha ha haa! Wewe na wenzio wenye mawazo kama yako nyote punguani. Andamaneni, nadhani mnatuchokoza watanganyika. Siku mzuka ukipanda tunawafutilia mbali. Hamna chochote mnachochangia Tanganyika zaidi ya kutuongezea umasikini. Sikia, mdai kujitenga ndio itakua safi. LOOSER !
 
Wengine tunaandamana maisha magumu na ufisadi, wenzetu wanajadili Muungano tu.....

Hao ma Bwana zao huko Muscut wanaandamana kudai utawala bora.

Wao mchawi wao ni Muungano. Kaazi kwelikweli.

Wakivunja Muungano, NTAPIKA PILAU la NGUVU kusherehekea UKOMBOZI wa kwanza wa Tanganyika.

Ntasubiri wakianza kuzichapa Unguja na Pemba na mwisho Waarabu na Waswahili....... Hapo watakuja na kupiga magoti Tanganyika iwasaidie. Dawa hapo ni kuwaambia kuwa sasa MNAKUWA ki-MKOA na si Nchi.

LOOSER.

Kashindwa baba yako nyerere kuifanya mkoa kafanya kila juhudi lakini wapiiiiiiiiiiiii. yagujuu haitokuwa mkoa mungu yupo sio asumaniii
 
nikisema buriani muungano .... nani atakayelia akikumbuka favour za muungano....?
 
ha ha haa! Wewe na wenzio wenye mawazo kama yako nyote punguani. Andamaneni, nadhani mnatuchokoza watanganyika. Siku mzuka ukipanda tunawafutilia mbali. Hamna chochote mnachochangia Tanganyika zaidi ya kutuongezea umasikini. Sikia, mdai kujitenga ndio itakua safi. LOOSER !
Mkuu.
Hawa si wa kuwafutilia mbali..ni kuwaacha kwa amani waende kivyao ili sisi tupate urahisi wa kukabiliana na hili janga la kujitakia la umasikini.

Wewe na sikonge ni marafiki?

Mkuu. Punguza ghadhabu...munkari, jazba... kama ndio itakuwa safi waende basi tusiwatusi. EAC itatuunganisha tena nao.
 
Bora wapewe uhuru wao wanaotaka watuachie tanganyika yetu! Wakirudi tena unakuwa mkoa cyo nchi tena. Nchi ina wabunge wengi maraisi wa2 lakini watu hata mil 2 hawafiki wachache kuliko jimbo moja la bongo.
 
Wengine tunaandamana maisha magumu na ufisadi, wenzetu wanajadili Muungano tu.....

Hao ma Bwana zao huko Muscut wanaandamana kudai utawala bora.

Wao mchawi wao ni Muungano. Kaazi kwelikweli.

Wakivunja Muungano, NTAPIKA PILAU la NGUVU kusherehekea UKOMBOZI wa kwanza wa Tanganyika.

Ntasubiri wakianza kuzichapa Unguja na Pemba na mwisho Waarabu na Waswahili....... Hapo watakuja na kupiga magoti Tanganyika iwasaidie. Dawa hapo ni kuwaambia kuwa sasa MNAKUWA ki-MKOA na si Nchi.

LOOSER.
hakika nenda sikonge ukarine asali,unasubiri wazenj waikomboe zenj nawe upike pilau,hakika wewe nidhaifu unataka utafuniwe umeze,wenzio wako duniani wewe upo ulimwenguni,nirahisi wao walioko nje kufikisha ujumbe kuliko hapa tz media inabana,mkuu wazenj wameamka zamani wakati sisi wadanganyika bado tumelala fofofo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom