abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Sauti:Kongomano la katiba – 05 March 2011 | MZALENDO.NET
Wananchi, wazalendo, wapenda amani, maendeleo na utaifa wa nchi yetu ya Zanzibar.
Kufuatia mjadala wa Katiba Mpya unavyoendelea, mengi yamefichuliwa dhidi ya muungano wetu uliodumu kwa miaka 47. Pamoja na nia njema wakati wa kuasisiwa muungano wanchi mbili, Tanganyika na Zanzibar, kiukweli sasa hivi hali haiku hivyo.
Tumeshuhudia wanansheria wetu, mara kwa mara, wamekuwa wakitoa dosari zao zinazoonyesha kupotea kwa nia njema iliyokusudiwa. Miongozi mwao ni pamoja na kutamka bayana kuwa muungano huu kisheria haipo tena, kilichobaki ni kinadharia tu.
Hivyo basi, ni wakati wetu sote kwa pamoja kuungana katika kudai haki yetu kama raia watiifu kwa taifa letu pamoja na kudai haki za nchi yetu iliyopoteza haki zake kwa kufanya maandamano ya amani.
Madhumuni ya maandamano.
- Kudai muungano ujadiliwe upya na pande zote.
- Kuunga mkono matamko yanayotolewa na wanasheria wetu kwenye mjadala wa katiba.
- Kutoa muamsho kwa jamii na wananchi juu ya kutetea haki za nchi na taifa letu Zanzibar.
Petition itakuwa na ujumbe ambao ni open letter itakayo beba ujumbe mmoja wa madai yetu kwa sehemu zote zitakazofanyika maandamano.
Siku ya Maandamano.
Maandamano yamepangwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 1/04/2011. Ijumaa ni siku ya mwisho wa wiki, itakuwa muafaka kwa Wazanzbibar wengi kuweza kushiriki. Vilevile itakuwa ni wiki nne kabla kufanyika sherehe za Muungano hapo 26/04/2011. Wale walioko makazini tunaomba waombe likizo zao mapema ili waweze kushiriki.
Eneo la Maandamano.
Maandamano yatafanyika ulimwengu mzima.
Kitovu cha maandamano haya kitakuwa ni ndani ya Zanzibar, ambapo Petition ya madai yetu itawasilishwa kwa Waziri wa Sheria na Katiba na Mwanasheria Mkuu wa SMZ.
Kwa wale walioko Tanzania Bara, wao watawasilisha Petition yao kwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa nchi nyengine dunia, Wazanzibar na Watanzania kwa jumla, watafanya maandamano kwa kila nchi yenye ubalozi wa Tanzania. Petition zitawasilishwa kwa mabalozi wa nchi husika ili kuziwasilisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambae wakati huohuo anakuwa Rais wa Shughuli za Serikali ya Tanganyika pamoja na Rais wa Zanzibar.
Yanayohitajika
Tunaomba ushirikiano kutoka kwa Wazanzibar wote ulimwenguni kufanikisha shughuli hii. Tunahitaji mawakala wa kusimamia kutoka kila nchi husika. Hii itasaidia kufikisha ujumbe kule tunakokusudia.
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nami kupitia email yangu ashakh@mzalendo.net
NOTE: Msisitizo unatiliwa kuwa haya ni maandamano ya amani, kwa lengo la kudai haki zetu.
Wananchi, wazalendo, wapenda amani, maendeleo na utaifa wa nchi yetu ya Zanzibar.
Kufuatia mjadala wa Katiba Mpya unavyoendelea, mengi yamefichuliwa dhidi ya muungano wetu uliodumu kwa miaka 47. Pamoja na nia njema wakati wa kuasisiwa muungano wanchi mbili, Tanganyika na Zanzibar, kiukweli sasa hivi hali haiku hivyo.
Tumeshuhudia wanansheria wetu, mara kwa mara, wamekuwa wakitoa dosari zao zinazoonyesha kupotea kwa nia njema iliyokusudiwa. Miongozi mwao ni pamoja na kutamka bayana kuwa muungano huu kisheria haipo tena, kilichobaki ni kinadharia tu.
Hivyo basi, ni wakati wetu sote kwa pamoja kuungana katika kudai haki yetu kama raia watiifu kwa taifa letu pamoja na kudai haki za nchi yetu iliyopoteza haki zake kwa kufanya maandamano ya amani.
Madhumuni ya maandamano.
- Kudai muungano ujadiliwe upya na pande zote.
- Kuunga mkono matamko yanayotolewa na wanasheria wetu kwenye mjadala wa katiba.
- Kutoa muamsho kwa jamii na wananchi juu ya kutetea haki za nchi na taifa letu Zanzibar.
Petition itakuwa na ujumbe ambao ni open letter itakayo beba ujumbe mmoja wa madai yetu kwa sehemu zote zitakazofanyika maandamano.
Siku ya Maandamano.
Maandamano yamepangwa kufanyika siku ya Ijumaa tarehe 1/04/2011. Ijumaa ni siku ya mwisho wa wiki, itakuwa muafaka kwa Wazanzbibar wengi kuweza kushiriki. Vilevile itakuwa ni wiki nne kabla kufanyika sherehe za Muungano hapo 26/04/2011. Wale walioko makazini tunaomba waombe likizo zao mapema ili waweze kushiriki.
Eneo la Maandamano.
Maandamano yatafanyika ulimwengu mzima.
Kitovu cha maandamano haya kitakuwa ni ndani ya Zanzibar, ambapo Petition ya madai yetu itawasilishwa kwa Waziri wa Sheria na Katiba na Mwanasheria Mkuu wa SMZ.
Kwa wale walioko Tanzania Bara, wao watawasilisha Petition yao kwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa nchi nyengine dunia, Wazanzibar na Watanzania kwa jumla, watafanya maandamano kwa kila nchi yenye ubalozi wa Tanzania. Petition zitawasilishwa kwa mabalozi wa nchi husika ili kuziwasilisha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambae wakati huohuo anakuwa Rais wa Shughuli za Serikali ya Tanganyika pamoja na Rais wa Zanzibar.
Yanayohitajika
Tunaomba ushirikiano kutoka kwa Wazanzibar wote ulimwenguni kufanikisha shughuli hii. Tunahitaji mawakala wa kusimamia kutoka kila nchi husika. Hii itasaidia kufikisha ujumbe kule tunakokusudia.
Kwa maelezo zaidi tafadhali wasiliana nami kupitia email yangu ashakh@mzalendo.net
NOTE: Msisitizo unatiliwa kuwa haya ni maandamano ya amani, kwa lengo la kudai haki zetu.