Natanguliza shukrani zangu kwa JamiiForums kwa kazi nzuri mnayoifanya. Yaani mpaka nje ya nchi Watanzania na wasiokuwa utawakuta wanasoma na kutoa maoni katika mtandao huu maarufu. Hongereni sana.
Sasa nije kwenye mada yangu. Sisi Wazanzibari tupo vizuri sana tena sana katika lugha zetu mbili kuliko ndugu zetu wa bara ambao huchanganya na lafudhi ya kikwao. Kuthibitisha hayo sikiliza hotuba ya madam (mama) president (rais) Samia Suluhu Hassan aliyoitoa Umoja wa Mataifa kwa lugha safi, nadhifu, matamshi sahihi kabisa ukizima tv (luninga) yako na ukamsikiliza utasema ni Muingereza halisi. Hiyo ni kwa lugha ya Kiingereza.
Ukija kwenye lugha ya Kiswahili ukamsiliza mwenyekiti wa baraza la wazee la Chadema majuzi tu alikuwa anahutubia wazee wenzie lakini Kiswahili kilikuwa safi, fasaha, sanifu na kinaeleweka kirahisi sana.
Sasa njoo kwa mheshimiwa Polepole, yeye naye alikuwa akizungumza mada zake kwa Kiswahili lakini kichekesho neno magharibi limemshinda kabisa anatamka mangaribi, isitoshe lafudhi yake imeingiliana na ya kikwao. Nawaomba wabara mjifundishe lugha hizi mbili mkishindwa muongee kikwenu.
Sasa nije kwenye mada yangu. Sisi Wazanzibari tupo vizuri sana tena sana katika lugha zetu mbili kuliko ndugu zetu wa bara ambao huchanganya na lafudhi ya kikwao. Kuthibitisha hayo sikiliza hotuba ya madam (mama) president (rais) Samia Suluhu Hassan aliyoitoa Umoja wa Mataifa kwa lugha safi, nadhifu, matamshi sahihi kabisa ukizima tv (luninga) yako na ukamsikiliza utasema ni Muingereza halisi. Hiyo ni kwa lugha ya Kiingereza.
Ukija kwenye lugha ya Kiswahili ukamsiliza mwenyekiti wa baraza la wazee la Chadema majuzi tu alikuwa anahutubia wazee wenzie lakini Kiswahili kilikuwa safi, fasaha, sanifu na kinaeleweka kirahisi sana.
Sasa njoo kwa mheshimiwa Polepole, yeye naye alikuwa akizungumza mada zake kwa Kiswahili lakini kichekesho neno magharibi limemshinda kabisa anatamka mangaribi, isitoshe lafudhi yake imeingiliana na ya kikwao. Nawaomba wabara mjifundishe lugha hizi mbili mkishindwa muongee kikwenu.