salaam ndugu wapendwa.
matukio ya hivi karibuni juu ya mjadala wa kujadili rasimu ya mapendekezo ya katiba ya Tanzania yaliibua na kuweka hadharani hisia za wenzetu katika muungano huu wa Tanzania.
wakati wa mjadala uliofanyika katika hotel ya Bwawani mjini Unguja wanzabari walionekana kuwa waliandaliwa na kujiandaa kwa hoja yao mbele ya mheshimiwa JOHN SITTA aliyekuwa ndiye mwendesha mada.
wakiwa na mabango yao walitamka hadharani kuwa wamechoshwa na muungano na kuwataka wabunge wao waliokuwa bungeni wakati huo warejee visiwani wadai talaka yao.
kana kwamba haitoshi wakachana hata kilichoitwa rasimu ya katiba.lakini hoja yao ikagusa kuwa Muungano wa Zanzibar na nani wakati serikali ya Tanganyika haipo wakati wao wana serikali yao kamili tena na wimbo wa taifa lao,bendera yao,Bunge lao (baraza la wawakilishi), Rais wao nk huku upande wa pili hakuna rais wao,hakuna bendera yao, hakuna wimbo wao,hakuna bunge lao,Hakuna hata identity yao vyote vilifutwa ili kuungana na upande wa pili.(niliona hii ni hoja ya msingi sana)
Hivi juzi tu tumesikia kwenye taarifa za habari kuwa kundi la watu limechoma biashara za Wa bara na kuwaambia waende kwao kwani wamewachoka na muungano wao. jambo hili sio dogo hata kufumbiwa macho.
chokochoko hizi zitaendelea kutuumiza watu wa bara mpaka lini huku sisi tukiwakumbatia ndugu zetu katika lundo la ardhi na mali tele ya Tanganyika? matusi haya mpaka lini.Mbona sisi tunawakaribisha na kimiliki majumba, mashamba,makambuni majumba ya kupangisha nk.
Ukiwa huu wa kutokuwa na serikali yetu ya Tanganyika tukawa na msemaji wa watanganyika utaisha lini?
Siyo serikali ya Muungano wala ya visiwani iliyotoa tamko kulaani vitendo hivyo vya kibaguzi hata kama watasema hawana ushahidi wa hayo yaliyotokea maeneo ya mashamba huko unguja je? yaliyotokea zanzibar mjini mbele ya runinga zao mbona wameyafumbia macho?
Mnataka watanganyika waingie mitaani kudai haki yao? angalieni yanayotokea uarabuni kwani vifaru na majeshi yameshindwa kuzima moto wa wananchi, kwa hiyo viongozi wetu msilale mpaka watu wakaamka wenyewe.
tutachekesha sana tuking'ang'ania muungano wa Afrika Mashariki huku tuna shindwa kuweka sawa haya ya nchi mbili ambazo leo tunasema tuna miaka 47 huku upande mmoja tukinyanyasana.
Mzee Mafwili mimi nataka kusikia kauli ya Serikali juu ya uchafu huu
wasaalam
matukio ya hivi karibuni juu ya mjadala wa kujadili rasimu ya mapendekezo ya katiba ya Tanzania yaliibua na kuweka hadharani hisia za wenzetu katika muungano huu wa Tanzania.
wakati wa mjadala uliofanyika katika hotel ya Bwawani mjini Unguja wanzabari walionekana kuwa waliandaliwa na kujiandaa kwa hoja yao mbele ya mheshimiwa JOHN SITTA aliyekuwa ndiye mwendesha mada.
wakiwa na mabango yao walitamka hadharani kuwa wamechoshwa na muungano na kuwataka wabunge wao waliokuwa bungeni wakati huo warejee visiwani wadai talaka yao.
kana kwamba haitoshi wakachana hata kilichoitwa rasimu ya katiba.lakini hoja yao ikagusa kuwa Muungano wa Zanzibar na nani wakati serikali ya Tanganyika haipo wakati wao wana serikali yao kamili tena na wimbo wa taifa lao,bendera yao,Bunge lao (baraza la wawakilishi), Rais wao nk huku upande wa pili hakuna rais wao,hakuna bendera yao, hakuna wimbo wao,hakuna bunge lao,Hakuna hata identity yao vyote vilifutwa ili kuungana na upande wa pili.(niliona hii ni hoja ya msingi sana)
Hivi juzi tu tumesikia kwenye taarifa za habari kuwa kundi la watu limechoma biashara za Wa bara na kuwaambia waende kwao kwani wamewachoka na muungano wao. jambo hili sio dogo hata kufumbiwa macho.
chokochoko hizi zitaendelea kutuumiza watu wa bara mpaka lini huku sisi tukiwakumbatia ndugu zetu katika lundo la ardhi na mali tele ya Tanganyika? matusi haya mpaka lini.Mbona sisi tunawakaribisha na kimiliki majumba, mashamba,makambuni majumba ya kupangisha nk.
Ukiwa huu wa kutokuwa na serikali yetu ya Tanganyika tukawa na msemaji wa watanganyika utaisha lini?
Siyo serikali ya Muungano wala ya visiwani iliyotoa tamko kulaani vitendo hivyo vya kibaguzi hata kama watasema hawana ushahidi wa hayo yaliyotokea maeneo ya mashamba huko unguja je? yaliyotokea zanzibar mjini mbele ya runinga zao mbona wameyafumbia macho?
Mnataka watanganyika waingie mitaani kudai haki yao? angalieni yanayotokea uarabuni kwani vifaru na majeshi yameshindwa kuzima moto wa wananchi, kwa hiyo viongozi wetu msilale mpaka watu wakaamka wenyewe.
tutachekesha sana tuking'ang'ania muungano wa Afrika Mashariki huku tuna shindwa kuweka sawa haya ya nchi mbili ambazo leo tunasema tuna miaka 47 huku upande mmoja tukinyanyasana.
Mzee Mafwili mimi nataka kusikia kauli ya Serikali juu ya uchafu huu
wasaalam