Wazanzibari hawataki muungano wanawafukuza wabara visiwani kwao

mafwili

Member
Nov 22, 2010
9
1
salaam ndugu wapendwa.

matukio ya hivi karibuni juu ya mjadala wa kujadili rasimu ya mapendekezo ya katiba ya Tanzania yaliibua na kuweka hadharani hisia za wenzetu katika muungano huu wa Tanzania.

wakati wa mjadala uliofanyika katika hotel ya Bwawani mjini Unguja wanzabari walionekana kuwa waliandaliwa na kujiandaa kwa hoja yao mbele ya mheshimiwa JOHN SITTA aliyekuwa ndiye mwendesha mada.

wakiwa na mabango yao walitamka hadharani kuwa wamechoshwa na muungano na kuwataka wabunge wao waliokuwa bungeni wakati huo warejee visiwani wadai talaka yao.

kana kwamba haitoshi wakachana hata kilichoitwa rasimu ya katiba.lakini hoja yao ikagusa kuwa Muungano wa Zanzibar na nani wakati serikali ya Tanganyika haipo wakati wao wana serikali yao kamili tena na wimbo wa taifa lao,bendera yao,Bunge lao (baraza la wawakilishi), Rais wao nk huku upande wa pili hakuna rais wao,hakuna bendera yao, hakuna wimbo wao,hakuna bunge lao,Hakuna hata identity yao vyote vilifutwa ili kuungana na upande wa pili.(niliona hii ni hoja ya msingi sana)

Hivi juzi tu tumesikia kwenye taarifa za habari kuwa kundi la watu limechoma biashara za Wa bara na kuwaambia waende kwao kwani wamewachoka na muungano wao. jambo hili sio dogo hata kufumbiwa macho.

chokochoko hizi zitaendelea kutuumiza watu wa bara mpaka lini huku sisi tukiwakumbatia ndugu zetu katika lundo la ardhi na mali tele ya Tanganyika? matusi haya mpaka lini.Mbona sisi tunawakaribisha na kimiliki majumba, mashamba,makambuni majumba ya kupangisha nk.

Ukiwa huu wa kutokuwa na serikali yetu ya Tanganyika tukawa na msemaji wa watanganyika utaisha lini?

Siyo serikali ya Muungano wala ya visiwani iliyotoa tamko kulaani vitendo hivyo vya kibaguzi hata kama watasema hawana ushahidi wa hayo yaliyotokea maeneo ya mashamba huko unguja je? yaliyotokea zanzibar mjini mbele ya runinga zao mbona wameyafumbia macho?

Mnataka watanganyika waingie mitaani kudai haki yao? angalieni yanayotokea uarabuni kwani vifaru na majeshi yameshindwa kuzima moto wa wananchi, kwa hiyo viongozi wetu msilale mpaka watu wakaamka wenyewe.

tutachekesha sana tuking'ang'ania muungano wa Afrika Mashariki huku tuna shindwa kuweka sawa haya ya nchi mbili ambazo leo tunasema tuna miaka 47 huku upande mmoja tukinyanyasana.

Mzee Mafwili mimi nataka kusikia kauli ya Serikali juu ya uchafu huu

wasaalam
 
Moto wa Watanganyika ndio utakaowaamsha hao wakubwa ili waibembeleze Zanzibar kama kawaida yao, mimi naenda chagua kabisa duka namanga, manake moto hauko mbali kwa wapemba
 
Kwa hiyo kwa wapemba kuwepo kwa maduka ya wabara huko pemba+unguja ndo muungano?, je kuwepo kwa wazanzibari huko mombasa, nairobi, maputo pemba, shelisheli, comoro ni kwasababu zanzibar imeungana na miji/nchi hizo?, hivi hizi nchi zote ambazo wapemba wanaishi na kufanya biashara kwa raha zao zikiamua kuwafukuza kama wanavyo wafukuza watanganyika itakuwaje?-hili ni tatizo la kujaza ilmu ahera zaidi huku ukiwa duniani na kuiacha elimi dunia.
 
nyinyi wazanzibari mkiguswa mnadeka kama mashoga, utamaduni wenu.
achia ya moto wa juzi, leo biashara zingine zimefungwa bila sababu yoyote na maafsa wa wilaya, na kuwanyang'anya leseni zao, ni Rastaurant mbili za kitalii huko huko kazkazini Unguja...
na hao watetewe na nani? Watanganyika hawana kwao?
Watanganyika tuwahi maduka Namanga za Kariakoo, lakini za Namanga ndo dili!!!! mimi nawahi.
 
Niwekee moja nami naenda chagua nyumba Msasani
nyinyi wazanzibari mkiguswa mnadeka kama mashoga, utamaduni wenu.
achia ya moto wa juzi, leo biashara zingine zimefungwa bila sababu yoyote na maafsa wa wilaya, na kuwanyang'anya leseni zao, ni Rastaurant mbili za kitalii huko huko kazkazini Unguja...
na hao watetewe na nani? Watanganyika hawana kwao?
Watanganyika tuwahi maduka Namanga za Kariakoo, lakini za Namanga ndo dili!!!! mimi nawahi.
 
Fidah hussein,Salim bakhresa,zakharia,Abdallah Malick(cool blue,tembo tiles,safari cargo),Mo Dewji ni wazanzibar hawa watu na wao tuchome biashara zao? Wazanzibar fikilieni mara mbili acheni ulevi wa madaraka,tukikinukisha huku bara sijui mtakimbilia wapi?
 
Moto wa Watanganyika ndio utakaowaamsha hao wakubwa ili waibembeleze Zanzibar kama kawaida yao, mimi naenda chagua kabisa duka namanga, manake moto hauko mbali kwa wapemba

Na sisi tuandae mikakati ya kuwatimua kutoka kwetu Tanganyika. Imefika wakati wa Wtanganyika kujiuliza - hivi katika Muungano, Tanganyika tunafaidika vipi? Mana kwa hali ya sasa ni "Chao ni chao, chetu ni chao"

Nafikiri kuna watu wanawadanganya wenzetu wa Zanzibar kuwa wakitibagua watakuwa salama. Il;i mradi wao wameanza, sisi tumalizie!
 
Viongozi wetu hawana hata ubavu wa kutuliza nguvu ya wananchi. huu ndio udini ndani ya ccm unatisha.
 
Acheni kupotosha, hakuna mtu aliefukuzwa Zanzibar,, kama una ndugu yako mpigie simu umuulize,, ukifuata magazeti utapata taabu sana.
 
Halafu Mbaya zaidi hata hao walioko huku bara wakineemeka na kuinjoy bado hawaoni mazuri wanayotendewa wanazidi kulaani muungano ama kweli hili suala si la kisiasa bali ni la kidini zaidi kwani sielewi wanadhulumiwa kitu gani?
Hapa kuna shinikizo toka mahala fulani iwe isiwe.Na watambue kuwa suala la muungano halina haja ya kujadiliwa kwani maamuzi yalishapangwa ni sawasawa na kutafuta solution kwa suala ambalo limeshakuwa solved.
Nyerere na Karume hawakuwa wajinga sasa sisi tunachokonoa kitu gani kipya.Mimi naamini kabisa wazanzibar asili yao ni bara na huu ni ukweli usiopingika abadan! hawakuumbwa wala kuexist from nowhere isipokuwa bara na inawezekana kabisa historically zanzibar,pemba na Tanganyika zilikuwa ni nchi moja kabla hazijatenganishwa na maji ambayo baadae kadiri tunavyozidi kuishi yatavimeza visiwa hivi.
Wanasayansi wameshatuambia kuna 'global warming' ambayo baadhi ya effects zake ni kuongezeka kwa vina vya bahari yaani bahari kumega sehemu ya ardhi,sasa hawa watu katika vizazi vijavyo watakimbilia wapi nchi ya karibu?Uarabuni au wapi?Laiti kama mngekuwa na uwezo wa kuangalia mbali na wala si hapa wala msingepoteza muda.
Kwa nini basi mafia hawadai kuwa nao ni nchi?
Binafsi mimi suala hili kwangu nilisikiapo huona kichefuchefu na ninawaonea huruma sana watu wanahangaika sana, wanaendesha makongamano, wanaanzisha mihadhara,yote ni kupoteza muda na kupandikiza chuki katika jamii ambayo umoja ndio kitu pekee kilichowaunganisha.
%wise hivi kuna mtu asiyefahamu kuwa visiwani mnafaidika zaidi na muungano kulikoni wa bara?acheni hizo bana.
 
Hawa ni mambwiga sana .

Yanajifanya hayataki muungano lakini toka wamekinukisha huko zenji wengi wao wanakimbilia huku bara sasa najiuliza wao hawataki muungano wamekinukisha kwao halafu wanatimukia huku je wanafuata nin? Sasa??
 
Hawa ni mambwiga sana .

Yanajifanya hayataki muungano lakini toka wamekinukisha huko zenji wengi wao wanakimbilia huku bara sasa najiuliza wao hawataki muungano wamekinukisha kwao halafu wanatimukia huku je wanafuata nin? Sasa??

Ugonjwa wa kutaka kufanyiwa kila kitu unawasumbua. Usikute hawa wanatumiwa tu Kwa sababu za kijinga. Sasa wao wanafikiri muungano ukivunjika ule mpaka mpya Wa bahari utakuwa wa kwao?
 
Back
Top Bottom