Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,187
- 670
naam ni kweli wataendelea au wakitishwa watanyauka? na nnaamini baada ya muafaka tutasikia mengi
SMZ yaigomea EWURA
na Waandishi Wetu, Zanzibar
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imegoma kutumia viwango vipya vya umeme vilivyotangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kwa kuwa taasisi hiyo haina mamlaka ya kuipangia bei.
Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansur Yussuf Himid, alieleza hayo jana alipokuwa akijibu maswali ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika kikao kinachoendelea mjini Zanzibar.
Katika kikao hicho, Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini, Ali Abdallah Ali (CCM), aliitaka serikali kueleza sababu ya EWURA kupanga kiwango kikubwa cha umeme kama hicho.
Waziri Mansour alisema Zanzibar imeamua kukataa kutumia viwango vilivyotangazwa na taasisi hiyo kwa vile vitaathiri uchumi wa Zanzibar na wananchi wake.
Alieleza kwa mujibu wa sheria taasisi hiyo inapaswa kupanga viwango vya Tanzania Bara na si kwa upande wa Zanzibar, kwa vile jambo hilo lilipaswa kufanywa na TANESCO kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).
Alisema mashirika hayo ya umeme yana mkataba wa huduma tangu Zanzibar kuanza kupokea umeme wa gridi ya taifa kutoka Morogoro, ambao unapita chini ya bahari.
EWURA hawana mamlaka ya kuipandishia umeme Zanzibar, ndio maana hatujaafikiana katika suala la kutumia viwango vipya, alisema Waziri Mansour.
Alieleza kiwango cha bei ya umeme kilichotangazwa na EWURA cha asilimia 168 kimevunja rekodi na kingeathiri wananchi wa Zanzibar na uchumi wake.
Waziri Mansour alisema ni jambo la kushangaza wakati Zanzibar imepandishiwa kiwango hicho, upande wa Tanzania Bara ulipandishiwa kwa asilimia 21.7.
Alisema kwa msingi huo, Zanzibar kuanzia Machi mwaka huu imekuwa ikitumia kiwango cha asilimia 21.7, badala ya kiwango cha asilimia 168, kwa kuwa suala hilo hadi sasa halijapata muafaka.
Waziri huyo alisema kutokana na uzito wa jambo hilo, hivi sasa Zanzibar imeamua kulipeleka katika mazungumzo ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi, ili kulinda maslahi ya wananchi wa Zanzibar na uchumi wa visiwani.
Kutokana na maelezo hayo, Mwakilishi wa Viti Maalum, Najma Khalfan (CUF) alitaka kujua mikakati ya serikali kuwa na umeme wa kujitegemea.
Waziri huyo alisema, mikakati tayari imekwishaanza kuchukuliwa, ikiwemo kufuta sheria ya ukiritimba ili kukaribisha wawekezaji katika sekta ya nishati Zanzibar.
Alisema hadi sasa kuna kampuni mbili, ikiwemo ya SDE ya Israel na Gold Solar Wind Management ya Ujerumani ambazo zimeonyesha nia ya kuwekeza katika sekta ya nishati ya umeme.
Waziri Mansour alisema SDE kutoka Israel inataka kuwekeza umeme wa mawimbi ya bahari (Wave Power) wakati kampuni ya Kijerumani wanataka kuwekeza umeme wa nguvu za jua kwa kuanzia na kuazalisha KWh 300,000 katika Kisiwa cha Pemba.
Hata hivyo, alisema kwa kuwa umeme huo kiwango chake ni kidogo utatoa huduma katika visiwa vidogo vidogo vilivyomo Zanzibar.
Zanzibar imekuwa ikipokea umeme kutoka Tanzania Bara tangu serikali ya awamu ya pili chini ya Rais mstaafu Aboud Jumbe Mwinyi, ambapo sasa inatumia kiasi cha shilingi milioni 900 kila mwezi kununua megawati 42 kwa matumizi ya Kisiwa cha Unguja, ambapo kwa upande wa Pemba wamekuwa wakitumia umeme unaozalishwa na vinu vilivyomo kisiwani humo.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wanaendelea kujadili muswada wa sheria ya kulinda haki za Tasnia na Mali za Ubunifu Zanzibar, uliowasilishwa na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba na Utawala Bora, Ramadhan Abdallah Shaaban.
source tanzania daima
SMZ yaigomea EWURA
na Waandishi Wetu, Zanzibar
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imegoma kutumia viwango vipya vya umeme vilivyotangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) kwa kuwa taasisi hiyo haina mamlaka ya kuipangia bei.
Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansur Yussuf Himid, alieleza hayo jana alipokuwa akijibu maswali ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika kikao kinachoendelea mjini Zanzibar.
Katika kikao hicho, Mwakilishi wa Jimbo la Mfenesini, Ali Abdallah Ali (CCM), aliitaka serikali kueleza sababu ya EWURA kupanga kiwango kikubwa cha umeme kama hicho.
Waziri Mansour alisema Zanzibar imeamua kukataa kutumia viwango vilivyotangazwa na taasisi hiyo kwa vile vitaathiri uchumi wa Zanzibar na wananchi wake.
Alieleza kwa mujibu wa sheria taasisi hiyo inapaswa kupanga viwango vya Tanzania Bara na si kwa upande wa Zanzibar, kwa vile jambo hilo lilipaswa kufanywa na TANESCO kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO).
Alisema mashirika hayo ya umeme yana mkataba wa huduma tangu Zanzibar kuanza kupokea umeme wa gridi ya taifa kutoka Morogoro, ambao unapita chini ya bahari.
EWURA hawana mamlaka ya kuipandishia umeme Zanzibar, ndio maana hatujaafikiana katika suala la kutumia viwango vipya, alisema Waziri Mansour.
Alieleza kiwango cha bei ya umeme kilichotangazwa na EWURA cha asilimia 168 kimevunja rekodi na kingeathiri wananchi wa Zanzibar na uchumi wake.
Waziri Mansour alisema ni jambo la kushangaza wakati Zanzibar imepandishiwa kiwango hicho, upande wa Tanzania Bara ulipandishiwa kwa asilimia 21.7.
Alisema kwa msingi huo, Zanzibar kuanzia Machi mwaka huu imekuwa ikitumia kiwango cha asilimia 21.7, badala ya kiwango cha asilimia 168, kwa kuwa suala hilo hadi sasa halijapata muafaka.
Waziri huyo alisema kutokana na uzito wa jambo hilo, hivi sasa Zanzibar imeamua kulipeleka katika mazungumzo ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi, ili kulinda maslahi ya wananchi wa Zanzibar na uchumi wa visiwani.
Kutokana na maelezo hayo, Mwakilishi wa Viti Maalum, Najma Khalfan (CUF) alitaka kujua mikakati ya serikali kuwa na umeme wa kujitegemea.
Waziri huyo alisema, mikakati tayari imekwishaanza kuchukuliwa, ikiwemo kufuta sheria ya ukiritimba ili kukaribisha wawekezaji katika sekta ya nishati Zanzibar.
Alisema hadi sasa kuna kampuni mbili, ikiwemo ya SDE ya Israel na Gold Solar Wind Management ya Ujerumani ambazo zimeonyesha nia ya kuwekeza katika sekta ya nishati ya umeme.
Waziri Mansour alisema SDE kutoka Israel inataka kuwekeza umeme wa mawimbi ya bahari (Wave Power) wakati kampuni ya Kijerumani wanataka kuwekeza umeme wa nguvu za jua kwa kuanzia na kuazalisha KWh 300,000 katika Kisiwa cha Pemba.
Hata hivyo, alisema kwa kuwa umeme huo kiwango chake ni kidogo utatoa huduma katika visiwa vidogo vidogo vilivyomo Zanzibar.
Zanzibar imekuwa ikipokea umeme kutoka Tanzania Bara tangu serikali ya awamu ya pili chini ya Rais mstaafu Aboud Jumbe Mwinyi, ambapo sasa inatumia kiasi cha shilingi milioni 900 kila mwezi kununua megawati 42 kwa matumizi ya Kisiwa cha Unguja, ambapo kwa upande wa Pemba wamekuwa wakitumia umeme unaozalishwa na vinu vilivyomo kisiwani humo.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar wanaendelea kujadili muswada wa sheria ya kulinda haki za Tasnia na Mali za Ubunifu Zanzibar, uliowasilishwa na Waziri wa Nchi Afisi ya Rais Katiba na Utawala Bora, Ramadhan Abdallah Shaaban.
source tanzania daima