Wayajua Mema yaliyoasisiwa na JK 2005 hadi 2010!

Bill

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
8,272
8,484
Hakika JK rais wetu mpendwa atakumbukwa kwa mengi moja wapo ni haya...

Mwanzilishi wa Siasa za Kimtandao
Mwanzilishi wa Siasa za Maji taka
Mwanzilishi wa Safari nyingi za nje
Mwanzilishi wa Siasa za makundi ndani ya CCM
Mwanzilishi wa mdororo wa umaarufu wa CCM
Mwanzilishi wa mbinu za ushindi wa uchakachuaji matokeo
Mwanzilishi wa siasa za kifamilia
Mwanzilsihi wa chuo kikuu cha Dodoma
Mwanzilishi wa maisha ya kufikirika (Maisha bora kwa kila mTZ)
Mwanzilishi wa kesi za ufisadi (kuwapeleka watuhumiwa mahakamani)
nk.

Ongeza mengine unayoyajua.........
 
mwendelezaji wa mapinduzi ya peoples choice
mwanzilishi wa mijadala ya udini
mwendelezaji wa ufisadi wa kufa mtu
mfumuko wa bei na maisha magumu
mwendelezaji wa matabaka wenye nacho na wasionacho
ubaguzi elimu ya juuuuuuuuuu
 
  • Kiongozi wa kwanza kufanya maajabu ya kuahidi bajaji 400 kwa wajawzito vijijini badala ya ambulance!
  • Kiongozi wa Kwanza kuwakilisha bajeti feki kwa wahisani badala ya iliyopitishwa na bunge
  • Kiongozi wa kwanza kuahidi Tembo na Swala barabara ya rami kuzunguka mlima kirimanjaro badala ya kuwajengea wananchi wa Kigoma hasa kibondo
  • Kiongozi wa kwanza kukiri wazi kuwa aliamini kuwa kujenga Dodoma University ni mpaka wafadhili matokeo yake anatoka kuomba misaada anakuta Ben keshongea na NSSF,PPF,LAPF nae kubaki midomo wazi
  • kiongozi wa kwanza kuchakachuliwa mafuta ya magari ya msafara wake
  • Kiongozi wa kwanza kuahidi barabara ya angani akiamini kupunguza misongomano dar es salaam.
Wengine twende kazi........
 
Nimwanzilishi pia wa maraisi wetu wajao kutunukiwa digree nyingi za jukwaani.
 
Kiongozi wa kwanza kupiga mieleka hadharani

Kiongozi wa kwanza kudanganywa mara nyingi na wasaidizi wake na akaendelea kuwachekea,

Kiongozi wa kwanza kuchuja damu mara nyingi bila kushitukiwa...................
 
  • Kiongozi wa kwanza kuahidi nyingi ambazo kama kila miaka mitano tungekuwa tunafanya hayo nchi ingekuwa hii zaidi ya Marekani
  • Kiongozi wa kwanza kuahidi Int. Airport Kigoma aka kijijini wakati wananchi hata luxury buses kama Kilimanjaro, Dar Express hawazijua kwa sababu hakuna hata barabara. Na wao kubaki wakimshangaa kwa hawana hata pesa ya kupandia ndege
  • kiongozi wa kwanza kuamua kujenga bandari Bagamoyo, Airport bagamoyo, Barabara Bagamoyo pembezoni mwa bahari hadi Tanga, Kuanzisha special economic Zone Bagamoyo yaani kila kitu bagamoyo
 
Kiongozi wa kwanza kupiga mieleka hadharani

Kiongozi wa kwanza kudanganywa mara nyingi na wasaidizi wake na akaendelea kuwachekea,

Kiongozi wa kwanza kuchuja damu mara nyingi bila kushitukiwa...................

Du kaka, hii kali... tena hivyo. Haya twendelee
 
Kiongozi wa kwanza kuchanganyiwa ma ded wa ngorongoro na morogoro

kiongozi wa kwanza kuchomekewa kifungu cha sheria za uchaguzi afu ye akasaini kwa mbembwe mbele ya waandishi wa habari.
 
Kila awamu ina nafasi ya uanzilishi wa jambo sio serikali ya mkwere tu. serikali zingine Je zilianzisha nini?
 
Back
Top Bottom