Wawili wapoteza maisha kwa kukosa dawa za kulevya

Vita ndio hiyo lazima wengine wafe ili wengine wapone, mnaambiwa acheni madawa mna zani mchezo? Na bado wakibana kama mwaka hivi tutakutana mtani
 
Acha wapumzike... Hii iwe fundisho kwa wengine kutambua madawa sio mazuri,tuyaepuke.

Wewe ni matazania kama walivyo watanzania wengi majibu yenu yanafanana,wanatanzania wanajibu bila hata ya kufikiri bila hata ya kuangalia "impact" msukumo wa hili tatizo.Vifo vitazidi, familia zitaparaganyika ,nguvu kazi itapungua umasikini utazidi.

Ubora wa Binadamu unapimwa kutokana na maamuzi yake na msimamo wake hasa katika wakati mgumu.....Ni hulka ya waafrika kuwa na udhaifu wa kutoa maamuzi magumu,lakini watanzania wana udhaifu mkubwa kuliko waafrika hasa inapokuja serikali kuwaamulia raia wake, ukifanananisha waafrika wengine IQ yetu iko chini sana

Maendeleo yanaletwa na maamuzi, sisi kama nchi maendeleo yatachukua muda mwingi kutufika,maamuzi yetu yanatokana na hisia zetu sio kwa uhalisi wa jambo, tatizo hili la kuamua kwa hisia bila ya kutafakari ni tatizo la wafrka wote lakini watanzania tumezidi,nchi za wenye akili wanakuwa wanatushangaa utokana na maamuzi yetu

Wenzetu wenye akili ili kuwanausuru raia wao,kama kuna unga mkali mitaani wanatangaza kwenye radio,wametengeneza sehemu maalum kwa wateja kwenda kujidunga,wametengeneza sehemu maalumu kwa wateja kwenda kunywa dawa.

Hawa watu wanaziita nchi kama Tanzania ni nchi ya dunia ya tatu,Nchi kuitwa dunia ya tatu ina maana kuwa nchi ya dunia ya kwanza wametupita kiuchumi,kimawazo,kiakili tuko nyuma yao miaka 500.

Tumetawaliwa na chuki,viasi na uonevu hatufati yale ambayo tumeyapanga wenyewe ili yatuongoze,taifa litazidi kuingia kwenye majanga kama maamuzi yetu yatatawaliwa na chuki na visasi...
 
Kwahiyo hayo ndio mafanikio?!

Mgonjwa anapokufa ni sifa kwa daktari?.

Wataalamu wa hii Mamlaka wamepata mafunzo kweli?
Hoja hapa ni kuwa baadhi ya watumiaji wa mihadarati wamekosa dozi zao, hivyo kupelekea kuwa arosto.

Wewe useme kuwa walitakiwa kupelekwa rehab centres, tatizo huwa wanajificha na hii hupelekea kufariki au kuumia.
 
Sianga nae kaingia kwenye IGIZO naona anaanza kuuvaa uhusika vizuri kabisa,ili mambo yaende sawa ni lazima mdundo wa sebene ukate viuno ili watu wakuelewe heeeee heeee kanyaga twende kaka Sianga komaa na media tu uku unasoma script za IGIZO akikuelewa director wa IGIZO inatosha kabisa.
 
Jamani mbona Pugu kinyamwezi(Dampo Pugu kinyamwezi) wauzaji na wanunuaji mbona wanaendelea na shuguli zao zamani walikuwa wanakaa barabarani kila kiongozi akienda au akipita wanawaona na wahusika wa pale wanawajua wauzaji wote ila kwa sasa kutokana na amsha hamsha hii wamesogezwa kidogo wasikae kwenye mabanda ya mama ntilie .Nashauri makonda nenda Dampo Pugu utaona mengi na vijana wetu wanavyo halibika na unga na gongo.
 
Acha kutetea wala unga ili tu uonekane unapingana na serikali.
Mwenyekiti wenu kesho anakamatwa atalala sero siku tatu kama ni mtumiaji lazima atapata arosto kwa hizo siku tatu.
Mineno mingine inakera ila uvumilivu unahusu hapa
 
Hongera kamishna.Nadhani ni wakati muafaka sasa wa kuanza mapambano ya kweli ya mihadarati kuachana chuki binafsi na siasa za majitaka katika hili suala.
 
Nafikiri hoja ya Sianga ni kwamba, kama matokeo ya initiative ya Makonda, upatikanaji wa madawa umekuwa mgumu na waliozoea kuishi kwa hizo dawa wanakufa. Yawezekana kufikiria kuwa Sianga amefurahia vifo hivyo lakini mimi nafikiri alichofurahia ni madawa kupungua mitaani.

Serikali ingetafuta namna ya kuwa rehabilitate waathirika ili wapone waachane na madawa. Sianga pia amesema hatataja majina hadharani; hii ni message sent to 'mungu' wa Dar na wote wanaofurahia maumivu ya wengine!
Lama unadhani hii ni nzuri, then hujui ukiombacho. Vita ya kimya kimya si mpya, na halo ndipo vigogo hukwepea. Ushahidi ukikamilika ni muhimu kuwa exposed
 
Wewe ni matazania kama walivyo watanzania wengi majibu yenu yanafanana,wanatanzania wanajibu bila hata ya kufikiri bila hata ya kuangalia "impact" msukumo wa hili tatizo.Vifo vitazidi, familia zitaparaganyika ,nguvu kazi itapungua umasikini utazidi.

Ubora wa Binadamu unapimwa kutokana na maamuzi yake na msimamo wake hasa katika wakati mgumu.....Ni hulka ya waafrika kuwa na udhaifu wa kutoa maamuzi magumu,lakini watanzania wana udhaifu mkubwa kuliko waafrika hasa inapokuja serikali kuwaamulia raia wake, ukifanananisha waafrika wengine IQ yetu iko chini sana

Maendeleo yanaletwa na maamuzi, sisi kama nchi maendeleo yatachukua muda mwingi kutufika,maamuzi yetu yanatokana na hisia zetu sio kwa uhalisi wa jambo, tatizo hili la kuamua kwa hisia bila ya kutafakari ni tatizo la wafrka wote lakini watanzania tumezidi,nchi za wenye akili wanakuwa wanatushangaa utokana na maamuzi yetu

Wenzetu wenye akili ili kuwanausuru raia wao,kama kuna unga mkali mitaani wanatangaza kwenye radio,wametengeneza sehemu maalum kwa wateja kwenda kujidunga,wametengeneza sehemu maalumu kwa wateja kwenda kunywa dawa.

Hawa watu wanaziita nchi kama Tanzania ni nchi ya dunia ya tatu,Nchi kuitwa dunia ya tatu ina maana kuwa nchi ya dunia ya kwanza wametupita kiuchumi,kimawazo,kiakili tuko nyuma yao miaka 500.

Tumetawaliwa na chuki,viasi na uonevu hatufati yale ambayo tumeyapanga wenyewe ili yatuongoze,taifa litazidi kuingia kwenye majanga kama maamuzi yetu yatatawaliwa na chuki na visasi...
Usirudie kuni quote katika inshu ya ujinga kama hii... Kwahiyo unataka tuwatengenezee sehemu za kufanyia upuuzi wao. Ukishakua mtumwa wa madawa hakuna kitu. Kinga ni bora zaidi katika hili kuliko tiba. Itakuwa ngumu kutokana na mbinu zake ila hatuna budi kufuata hii njia... Uchina ambao sio dunia ya tatu unanyongwa. Kama unanufaika, mwisho umewadia. Tuwaache wa pumzike kwa amani ili iwe fundisho.
 
Wawili wapoteza maisha kwa kukosa dawa za kulevya

Sunday , 19th Feb , 2017
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Sianga amesema watu wawili wameripotiwa kupoteza maisha mkoani Mwanza kwa sababu ya kukosa dawa za kulevya mtaani kama walivyozoea.


Sianga%201.jpg

Rogers Sianga, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya

Kamishna Sianga amesema taarifa hiyo ameipata kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, hali inayomaanisha mafanikio ya mapambano ya dawa hizo, ambapo kwa sasa usambaaji wake umepungua mtaani kwa kiasi kikubwa.

"Nimeongea na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ameniambia kwamba kuna watu wwili wamefariki sababu walikuwa drug addict na sasa dawa hizo hazipo mtaani" Amesema Sianga

Sianga amesema mara baada ya kupokea kijiti cha mapambano kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mamlaka hiyo imeendelea na moto huo huo, na kwamba kwa hivi sasa timu yake hailali, ikiendelea na mapambano kila siku na kwamba hata leo, kuna mtuhumiwa mkubwa wa dawa za kulevya amekamatwa.

"Leo asubuhi tumemkamata mtuhumiwa mmoja mkubwa wa dawa kulevya, tupo naye tunaendelea kumuhoji, mengi yataibuka" amesema Kamishna Sianga

Kuhusu kuendelea kutumia mbinu iliyokuwa ikitumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam paul Makonda ya kutaja majina hadharani,, Kamishna Sianga amesema hatatumia njia hiyo kwa kuwa kutaja majina ya watu hadharani kunaweza kuiingiza serikali katika matatizo maana kuna watu wengine wanaweza kutoa majina ya watu kwa sababu ya chuki binafsi.

Amesema njia anayoitumia ni kuwakamata na kuwahoji kimyakimnya na wakishajiridhisha hatua nyingine za kisheria zinafuata.

Katika hatua nyingine, Sianga amesema Tanzania iko makini katika kuwashughulikia wahusika wakubwa wa dawa za kulevya duaniani tangu miaka mingi iliyopita, akitolea mfano mtuhumiwa mmoja wa kike ambaye ni gwiji katika biashara hiyo au 'King Pin', ambaye hivi sasa amefungwa katika magereza ya Tanzania tangu mwaka 2010

"Tulimkamata mmoja kati ya watu waliokuwa wametajwa kama king pin wa dawa hizo nchini Marekani, alikuwa ameshindikana, na huko Marekani alikuwa na kesi zaidi ya 40, lakini alikamatwa hapa na amefungwa tangu mwaka 2010, yuko gerezani nafikiri kama siyo Keko, ni Segerea". Amesema Sianga.

JPM ametumia akili nyingi sana kumchagua Sianga,kwa sababu wamasai wana utaalam wa kufatilia kimyakimya,mpaka kukutia mbaroni,kama vijana wakimasai wakimkimbiza mwizi mwenyewe ndie hukimbilia polisi mziki anaoupata!
 
Tanzania mpya bila madawa ya kulevya,Viroba,Ukimwi,Malaria, Tezi dume,Kansa ya matiti,vifo vya watoto wachanga na kina mama,makahaba,makaka poa bila kusahau rushwa n.k
 
Usirudie kuni quote katika inshu ya ujinga kama hii... Kwahiyo unataka tuwatengenezee sehemu za kufanyia upuuzi wao. Ukishakua mtumwa wa madawa hakuna kitu. Kinga ni bora zaidi katika hili kuliko tiba. Itakuwa ngumu kutokana na mbinu zake ila hatuna budi kufuata hii njia... Uchina ambao sio dunia ya tatu unanyongwa. Kama unanufaika, mwisho umewadia. Tuwaache wa pumzike kwa amani ili iwe fundisho.

Mkuu itakuwa tabu mtu kama wewe kufahamu nini nimeandika,wenye akili watafahamu nini nimeandika,wewe unaita "upuuzi" wenye akili wanaitwa "ugonjwa",kwasababu wewe tayari umeshajibu kwa kihisia kuliko uhalisia wa hili jambo

Waafrika kwasababu za udhaifu wetu wakutoweza kutoa maamuzi wagumu na ukosefu wa wakufahamu mambo yalivyo ndio maana bara letu la Afrika liko nyuma sana limepitwa na mabara yote kimaendeleo,bara la Afrika linaitwa "The dark continent",waloliita hili bara la Afrika kuwa ni bara la kiza wana maana yao.

Tanzania kuna sehemu zinaitwa "Sober house" sehemu za kuwatibu hawa wathirika wa haya madawa,bila shaka haya mawazo ya kujenga hizo sehemu yameletwa na "European" mzungu,kwani waafrika mawazo ya kutengeneza sehemu kama hizo hawawezi kuwa nayo kwani kwa wao ni "Upuuzi".....kila kitu tufikiriwe hatuwezi kufikiri wenyewe kwasabau tunashindwa kuwa na upeo wa kuona hali halisi ya matatizo.

Sasa kwa taarifa yako wenzetu wenye akili "Sober house" serikali zinawatibu wagonjwa bure sio kwa pesa kama hapa Tanzania,iwapo tu kama mgonjwa amejitolea mwenyewe

By the way,nimeku quote kwasababu nimekuona mjinga, maana yangu ilikua ni kukuelimisha,hamna fundisho litakalo patikana hapo mauti yatazidi kuwaelemea watanzania,........"our job is to wipe out the disease not the patients".....
 
Lama unadhani hii ni nzuri, then hujui ukiombacho. Vita ya kimya kimya si mpya, na halo ndipo vigogo hukwepea. Ushahidi ukikamilika ni muhimu kuwa exposed
Of course, sianga anauma na kupuliza. Vita ya kimya kimya ndo iliyoshindwa zamani!
 
Dah. Sasa hii serkali nimeichoka kwa maigizo. Khaa.
Wanataka kuwaaminisha kuwa watz vita ya madawa imefanikiwa wakati bei za unga zimepanda. Vigogo wakubwa wa unga ndyo wanapiga pesa vizur sasa.
Uki kamatwa ukatoe maelezo unga umepanda bei wap? ume tambua vip? na ni kigogo gan anae piga pesa utaweza kujibu haya mkuu?... Hapo ndo utakaa usome rangi zote
 
Hii vita inatakiwa iende hivi, sio kukurupuka tu na kutaja taja majina. Viva kamshina.
Nasema, kwa kujiamini, hii vita ikiendeshwa kimya kimya au kwa usiri, hakika haitafanikiwa, maana inatoa mwanya kwa nguvu ya pesa ya mapapa wa hiyo biashara, kuvuruga mikakati ya hiyo vita.

Kwa nini tusiamini kuwa wanaohusika na hiyo vita ndo wahusika wakuu wa biashara ya madawa ya kulevya. Ushahidi ni jinsi ukamataji wa washiriki wa biashara ya madawa ya kulevya, hasa watumiaji, ulivyopamba moto baada ya mkakati wa Makonda kuwataja baadhi tu ya wahusika hadharani.
 
Back
Top Bottom