Wakuu poleni na mapumziko ya sikukuu ya mapinduzi ya Zanzibar.
Jana kwenye taarifa ya habari ya ITV saa mbili usiku nilimuona Waziri wa Nishati na Madini Bw. William Ngeleja akifungua mradi wa maji ambao upo katika mgodi wa GGM.
Katika maelezo yao (Mkurugenzi wa wilaya ya Geita na mwakilishi wa GGM) walidai kuwa pindi utakapokamilika, mradi huo wa maji utakuwa na uwezo wa kutoa mita za ujazo 500 kwa siku ambapo mgodi wa Geita utakuwa unatumia mita za ujazo 300 na kiwango kitakachobaki (mita za ujazo 200) watapelekewa wananchi wa Geita.
Gharama ya mradi huo ni sh. 15bn ambapo GGM watatoa 6bn na kiasi kitakachobaki 9bn kitagharamiwa na serikali.
Nilijaribu kufanya analysis ndogo ya haraka haraka ambapo niligundua kuwa:
1. GGM watatumia 60% ya maji yote yatakayozalishwa na wananchi wa Geita watapelekewa 40% ya kiasi kinachobaki (hatukuelezwa kama mita za ujazo 200 ndiyo mahitaji ya wananchi wa Geita kwa siku).
2. Katika kuchangia, GGM wao watachangia 40% wakati serikali kwa niaba ya wananchi wake itachangia 60% ya mradi wote.
Swali linakuja:
Inakuwaje mgodi ambao utatumia maji zaidi ya mara moja na nusu ya wananchi uchangie mradi huo mara moja na nusu chini ya kiwango ambacho serikali itachanga?
Nilitarajia kuwa mtu anayetumia zaidi ndiye anastahili kulipa zaidi, lakini vilevile nilitarajia kuwa hii ilikuwa nafasi nzuri kwa mgodi kurudisha japo kiasi kidogo cha faida yao kwa wananchi.
Napata picha (na hii ni kwa mtu yeyote mwenye akili) kwamba mradi huo ni kwa manufaa ya mgodi isipokuwa kuna hila imefanyika ili serikali igharamie mradi huo kwa manufaa ya GGM.
IWAPI SASA FAIDA YA UWEKEZAJI KATIKA MIGODI KAMA KILA KITU TUNAWAGHARAMIA KILA KITU HALI WAO HAWALIPI CHOCHOTE SERIKALINI?
Zinduka!.
Jana kwenye taarifa ya habari ya ITV saa mbili usiku nilimuona Waziri wa Nishati na Madini Bw. William Ngeleja akifungua mradi wa maji ambao upo katika mgodi wa GGM.
Katika maelezo yao (Mkurugenzi wa wilaya ya Geita na mwakilishi wa GGM) walidai kuwa pindi utakapokamilika, mradi huo wa maji utakuwa na uwezo wa kutoa mita za ujazo 500 kwa siku ambapo mgodi wa Geita utakuwa unatumia mita za ujazo 300 na kiwango kitakachobaki (mita za ujazo 200) watapelekewa wananchi wa Geita.
Gharama ya mradi huo ni sh. 15bn ambapo GGM watatoa 6bn na kiasi kitakachobaki 9bn kitagharamiwa na serikali.
Nilijaribu kufanya analysis ndogo ya haraka haraka ambapo niligundua kuwa:
1. GGM watatumia 60% ya maji yote yatakayozalishwa na wananchi wa Geita watapelekewa 40% ya kiasi kinachobaki (hatukuelezwa kama mita za ujazo 200 ndiyo mahitaji ya wananchi wa Geita kwa siku).
2. Katika kuchangia, GGM wao watachangia 40% wakati serikali kwa niaba ya wananchi wake itachangia 60% ya mradi wote.
Swali linakuja:
Inakuwaje mgodi ambao utatumia maji zaidi ya mara moja na nusu ya wananchi uchangie mradi huo mara moja na nusu chini ya kiwango ambacho serikali itachanga?
Nilitarajia kuwa mtu anayetumia zaidi ndiye anastahili kulipa zaidi, lakini vilevile nilitarajia kuwa hii ilikuwa nafasi nzuri kwa mgodi kurudisha japo kiasi kidogo cha faida yao kwa wananchi.
Napata picha (na hii ni kwa mtu yeyote mwenye akili) kwamba mradi huo ni kwa manufaa ya mgodi isipokuwa kuna hila imefanyika ili serikali igharamie mradi huo kwa manufaa ya GGM.
IWAPI SASA FAIDA YA UWEKEZAJI KATIKA MIGODI KAMA KILA KITU TUNAWAGHARAMIA KILA KITU HALI WAO HAWALIPI CHOCHOTE SERIKALINI?
Zinduka!.