Wawekezaji kutoka Austria wavutiwa na mazingira ya uwekezaji nchini

mamayoyo1

JF-Expert Member
Jul 25, 2018
1,011
1,019


Afisa mwandamizi wa Ubalozi wa Austria wenye makazi yake Nairobi, Kenya. Bw. Kurt Muellauer akifungua Kongamano la Biashara lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na Wenyeviwanda Tanzania (TCCIA) na Ubalozi wa Austria.

Kongamano hilo nimwendelezo wa jitihada za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambao unawakilisha pia nchini Austria na wadau mbalimbali katika kutekeleza diplomasia ya uchumi. Pamoja na mambo mengine kampuni 8 kati 16 zinatarajiwa kufanya ziara jijini Dodoma tarehe 29 Januari kwa lengo la kukutana na Mawaziri wa Kilimo; Nishati; Fedha na Mipango; Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto na Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Kongamano hilo limefanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
 
Sijaona mahali kwenye post yako panapoonyesha mtu amevutiwa na mazingira ya uwekezaji nchi hii. Na dunia hii ya leo taarifa zinapatikana kirahisi mno. Hivi kuna kampuni gani kutoka first world itakayovutiwa na mazingira yaliyowafanya wenzao wafukuzwe au walazimike kufunga biashara zao? Hata ndotoni haitatokea.

Btw: mtu akialikwa ugenini anaweza kuwa polite na politically correct kwa kutosema alichokiona. Ila mtauuona ukweli wake kwenye matendo yake.
 
Hivi wale wafanyabiashara wa Morocco, Uturuki, Israel wamesharejea tena kuwekeza?
Maana nao tuliambiwa wamevutiwa kuwakeza, lakini baada ya kusema hayo kimya kimetanda.

Vipi kuhusu kujengewa Msikiti na uwanja wa mpira wa kisasa Dodoma kutoka kwa mfalme wa Morocco kumefikia wapi? Bora kuuliza sasa ili tusijekuwa tumetapeliwa au BAKWATA wameshavuta mpunga na kuutafuna.
 
Mazingira ya uwekezaji ni magumu sana kote duniani wakati huu kwa sababu mbali mbali, kama vita iliyopo ya kati ya Jiping na Trump.

Uwekezaji utakuja kuwa mgumu sana, hasa katika nchi za mivuruganyo kama hii tuliyojiletea wenyewe.

Hao mabalozi watapata tabu sana kama waliyoagizwa yatasimamiwa ilivyoagizwa. Wachache sana watabahatika kutoboa.
 
Sijaona mahali kwenye post yako panapoonyesha mtu amevutiwa na mazingira ya uwekezaji nchi hii. Na dunia hii ya leo taarifa zinapatikana kirahisi mno. Hivi kuna kampuni gani kutoka first world itakayovutiwa na mazingira yaliyowafanya wenzao wafukuzwe au walazimike kufunga biashara zao? Hata ndotoni haitatokea.

Btw: mtu akialikwa ugenini anaweza kuwa polite na politically correct kwa kutosema alichokiona. Ila mtauuona ukweli wake kwenye matendo yake.


mmebaki wachche wenye weledi wa kuandika kiungwana hv..mie siwez kbs sasa hv..ovyo sana majitu mengine na nyuzi zao😏
 
Back
Top Bottom