wawakilishi wa TANZANIA NA MALAWI kukutana MZUZU tarehe August 20 2012

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,573
Malawi and Tanzania representatives are scheduled to meet in Mzuzu on August 20 2012 ;


Malawi wana hoja 3 za msingi.

.1. Anglo-Germany treaty 1890 Boundary inayoonesha Tanganyika mpk hupo kwenye beach (coast)

2. Sababu za Kamuzu banda ; kudai Mbeya na Nyasa ni mali ya Malawi

3. Zoezi ili lilikuwepo kitambo kwanini baada ya kuchaguliwa raisi mwanamke ndo Tanzania inapeleka majeshi na si kipindi cha mihula ya viongozi wanaume?
 
Tunataka tujue timu itakayounda jopo la Tanzania. Mimi sitaki AG Werema awemo huyu ni kiazi mkubwa.

Jopo la Tanzania lipitie kwa umakini evidence ambazo Malawi wanadai zinahalalisha ziwa lote kuwa ni lao. From there Tanzania wajenge hoja zao.
 
Tangu kabla ya uhuru, mpaka huu una migogoro. Tusirukie kuamua na kuhukumu malawi kama wana makosa, tunatakiwa kuwa makini katika jambo hili. Tusikimbilie vita, sio suluhisho, ingawa ikibidi, haitakuwa na jinsi.
 
Unajua nimetoka angalia google map apa yaan moz vs malawi mpaka ni katikati ya ziwa ila ukija kwa Tz mpaka ni kwa lake shore huu uwandawazimu Sisi tutatumia kigezo cha UN Convention 1982 mpaka ni 12 NAutical Miles from the lake shore bothways which is the same to lake victoria and Tanganyika why this common sense is not common to Malawians.

Na uyo anaesema kwa nini sasa ivi hujui uchokozi waliuanza wao kwa kuanza utafiti unakuja mpaka manda litui itungi port Kwenye ilo jopo angalau kuwe na mtu mmoja au wawili wanaotoka maeneo ya kyela na ileje bse wanajua uchungu wa kupokwa ilo ziwa. Na ilo jopo likishindwa kukubaliana kuwa mpaka ni katikati ya ziwa wabaki uko uko ili tukiingia kijeshi adi Mzuzu ndo warudi na wanajeshi baada ya kumsimika raisi mpya wa Malawi.
 
wewe ni mmalawi.....umetuvamia JF...... nini kigezo cha hitimisho lako hili.

Tafuta ukweli utaelewa. Mimi ni mtanzania kama wewe na nilikuwa na mawazo kama wewe, lakini baada ya kupata ukweli sina budi kukubaliana nao.
 
LAKENYASA.jpg
 
Angalieni mipaka inavyoonesha. Ziwa nyasa liko Malawi na Msumbiji lakini si Tanzania.
 
point ya tatu...seriously??

Not seriaous..... Ni nani alijua Malawi itapata Rais mwanamke? Kampuni zinazotafiti Ziwa Nyasa ziliingia mkataba wakati wa rais mwanamume ( Bingu wa Mutharika) wakati wa mvutano na vikao. Kwa sasa kutokea vita sio suala la Rais mwanamke bali ni suala la kushindwa kufikia muafaka.
 
Tafuta ukweli utaelewa. Mimi ni mtanzania kama wewe na nilikuwa na mawazo kama wewe, lakini baada ya kupata ukweli sina budi kukubaliana nao.

eleza ukweli ulioutafuta tukusikie.... acha uongo hapa.... watu wazima hawawezi kuchukua miaka 50 bila kufikia muafaka eti wewe unalo jibu.
 
kwanza napinga kabisa kuwa uwepo wa rais mwanamke ndo sababu ya Tanzania kupeleka majeshi. Yeye hatawali kwa jinsi yake bali anatawala kama au kupitia taasisi ya serikali. rejea Margaret Thatcher aka Iron Lady na falklands, Indira Gandhi na Kashmir. pili turejee kabla wakoloni hawajaja ziwa halikuwa na watu??

Jibu ni walikuwepo na wakilizunguka hilo ziwa kwa pande zote za sasa Tanzania, Malawi na Msumbiji za sasa. Na hao wakazi walikuwa wengi wao ni wanyasa na ndo maana wakoloni waliita ziwa kuwa Nyasa ingawaje wenyeji waliliita "INYANJA" kama Victoria wenyeji wakiliita Nyanza. Wakati mwingereza anatawala shuleni, wanafunzi Tanganyika, walikuwa wanachora ramani ambazo mpaka ulikuwa unapita ndani ya maji.

Ni baada ya kuondoka mwingereza Malawi imeutoa mpaka majini na kuusogeza nchi kavu wakati Tanzania ikiendelea na michoro ya mpaka kuwa ndani ya maji kama tulivyokuwa tukiuweka wakati waingereza wakiwepo. wananchi hasa wa nchi hizi wamekuwa hawana mpaka katika kulitumia ziwa hili kama vile ambavyo wamekuwa hawana mpaka katika kuoleana. Ningeshauri Malawi wakubali iundwe Mamlaka ya kudumu ya matumizi ya pamoja ya ziwa Nyasa kama ilivyo kwa lake Victoria aka Nyanza na Mto Nile. Malawi iache uroho na ielewe Tanzania ndo yatokayo maji ya kulilisha ziwa hilo. Malawi ina mto mmoja nao unatoa maji Nyasa na kumwaga Bahari Hindi. Mipaka ibakie katika hali ya nchi hizi tatu kuwa huru na hili ziwa.

Vita halitakuwa ni suluhisho kwa itakuwa inaibuka mara na pale yeyote kati ya Malawi na Tanzania anapoona anauwezo wa kupigana vita ya kugombea ziwa letu hili.
 
Usalama wa Tanzania utakuwa mdogo sana kama ziwa lote litakuwa la Malawi... No common sense.

Nchi jirani inaweza kufika mpaka maji ya ziwa Nyasa yaliyopo kyela mjini kwa madai ya kwamba tuko nchini kwetu...... walioweka mipaka walikuwa wendawazimu?????
 
yaani mi nina wasiwasi kama roundtape technique itafanikiwa.... yaani dispute ya namna hii uwa inakuwa resolved by win-win method:israel:. ila kwa namna na nature ya mgogoro huu ulivyo sio kama kuna nchi itakubali kuachia kipande cha ziwa..

lawama zangu ni kwa K.B wa malawi na J.KM wa tanzania ambao waliweka kiporo hili swala, nadhani this time will pay it with profit , nawasiwasi vita inakuja
 
Ziwa Tanganyika lina jina la nchi ya Tanganyika haina maana kwamba ziwa lote ni la kwetu bali limegawanywa hadi Kongo DRC na zambia....

No common sense kusema ziwa kuitwa Malawi au Nyasa ( for Nyasaland) ndio la kwao.


Turudi kwa wazungu tukawaulize ilikuwaje ziwa la nchi zaidi ya moja walikuwa wanatoa jina kwa nchi moja????? tumia common sense.
 
Kuona hii ramani tu ndio unataka kusema ni ushahidi tosha kuwa ziwa ni mali ya Malawi..... kwani uliichora wewe????

Si bora ningechora mimi, hiyo ni mipaka iliyowekwa toka enzi za wakoloni. hatuna ujanja katika hili suala. Tutashindwa na malawi kisheria. Malawi hawataki vita na wala hawana haja na vita, bali sheria itafuata mkondo wake.
 
yaani mi nina wasiwasi kama roundtape technique itafanikiwa.... yaani dispute ya namna hii uwa inakuwa resolved by win-win method:israel:. ila kwa namna na nature ya mgogoro huu ulivyo sio kama kuna nchi itakubali kuachia kipande cha ziwa..

lawama zangu ni kwa K.B wa malawi na J.KM wa tanzania ambao waliweka kiporo hili swala, nadhani this time will pay it with profit , nawasiwasi vita inakuja

Hakuna vita, tuna viongozi makini pande zote mbili. Tutatatua tatizo hili mezani na kama itashindikana basi tutakwenda kwenye sheria.
 
Back
Top Bottom