voicer
JF-Expert Member
- Jul 13, 2020
- 5,551
- 11,881
Ni aibu..Wavuvi wameokoa Manusura,Serikali imeopowa Marehemu!
Je! Kuna
"Royal Tour" au
"Roho Tua"?
Kumbukizi.
Mei /21/1996.
Meli ya MV Bukoba ilipinduka na kuzama ndani ya Ziwa Victoria Siku ya Jumanne alfajiri . Kuzama kwa meli hiyo kulisababisha watu zaidi ya 800 kupoteza maisha baada ya kufa maji.
18 September2018
Watu 224 walithibitishwa kufa kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere,huko Ukara/Ukerewe.katika Ziwa Victoria.
06/November/2022
Ndege ya Precision Air ilipata ajali na kusababisha vifo vya watu 19 ndani ya ziwa victoria huko Bukoba,umbali mfupi kutoka fukwe ya ziwa hilo.
Waliostahili kufanya uokozi Bukoba,walifika eneo la tukio wakiwa ba Simu za Bei ghali,pamoja na Magari ya Bei ghari. Lakini bila vifaa wala mbinu za uokozi.
Badala yake wavuvi ndio wakatumia Mitumbwi yao Duni na kasia zao na hatimae kuweza kuokoa maisha ya baadhi ya abiria 26,waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.
Baadae masaa zaidi ya manne mpaka sita,ndio Serikali ikafanikiwa kuopowa miili ya Marehemu waliokuwa wamefia ndani ya ndege hiyo.
Mara zoote serikali inaishia na Ahadi, Porojo na Mazishi ya kisiasa.
Baadae Business as Usual...
Ni aibu kuitangaza Royal Tour( Roho Tua) kwa mbwembwe Duniani.Huku tukionyesha vituko Duniani.
Kwenye sekta mtambuka kama ya Usafiri wa Anga,ambayo ndio kiunganishi muhimu na kikuu cha Utalii kwa nchi yetu!
Hivi kwa hili la Precision Air, tumeitangazia nini Dunia,kuhusu sekta ya utalii?
Kituko zaidi,Serikali inatoa agizo kwa kijana shupavu,aliyetumia mbinu zake binafsi na kufanikiwa kuokowa manusura kwenye ajali hiyo.
Kwamba akapewe mafunzo na wale walioshindwa kuokoa wahanga wa ajali.
Hii imekaaje?
Ni lini na wapi serikali itaamua kuimarisha utayari wa vitengo vya uokoaji wa ajali kama hizi?
Hivi boat za Uokozi za Hiyo inayoitwa Marine Police zilienda wapi?
Mbaya kabisa,Rais wetu anaishia Twitter kwa Rambirambi na kisha kuzamia Misri.
Kati ya V8 na vifaa vya uokozi,kipi ni kipaumbele cha taifa?
Je!
Hata waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mh Byabato.....
Hakuona Umuhimu wa kutuma kikosi maalum cha Marine Navy na Helkopta za Jeshi kuwahi eneo la tukio.
Badala yake wakategemea vifaa vya kutoka GGM-Geita,Kagera Sugar na SONGORO MARINE kutoka Mwanza?
Je!
Watu wanapopiga kelele za Serikali na waziri husika kuwajibika wanakosea?
Haya bhana....
Alamsikhi!
10101
Je! Kuna
"Royal Tour" au
"Roho Tua"?
Kumbukizi.
Mei /21/1996.
Meli ya MV Bukoba ilipinduka na kuzama ndani ya Ziwa Victoria Siku ya Jumanne alfajiri . Kuzama kwa meli hiyo kulisababisha watu zaidi ya 800 kupoteza maisha baada ya kufa maji.
18 September2018
Watu 224 walithibitishwa kufa kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere,huko Ukara/Ukerewe.katika Ziwa Victoria.
06/November/2022
Ndege ya Precision Air ilipata ajali na kusababisha vifo vya watu 19 ndani ya ziwa victoria huko Bukoba,umbali mfupi kutoka fukwe ya ziwa hilo.
Waliostahili kufanya uokozi Bukoba,walifika eneo la tukio wakiwa ba Simu za Bei ghali,pamoja na Magari ya Bei ghari. Lakini bila vifaa wala mbinu za uokozi.
Badala yake wavuvi ndio wakatumia Mitumbwi yao Duni na kasia zao na hatimae kuweza kuokoa maisha ya baadhi ya abiria 26,waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.
Baadae masaa zaidi ya manne mpaka sita,ndio Serikali ikafanikiwa kuopowa miili ya Marehemu waliokuwa wamefia ndani ya ndege hiyo.
Mara zoote serikali inaishia na Ahadi, Porojo na Mazishi ya kisiasa.
Baadae Business as Usual...
Ni aibu kuitangaza Royal Tour( Roho Tua) kwa mbwembwe Duniani.Huku tukionyesha vituko Duniani.
Kwenye sekta mtambuka kama ya Usafiri wa Anga,ambayo ndio kiunganishi muhimu na kikuu cha Utalii kwa nchi yetu!
Hivi kwa hili la Precision Air, tumeitangazia nini Dunia,kuhusu sekta ya utalii?
Kituko zaidi,Serikali inatoa agizo kwa kijana shupavu,aliyetumia mbinu zake binafsi na kufanikiwa kuokowa manusura kwenye ajali hiyo.
Kwamba akapewe mafunzo na wale walioshindwa kuokoa wahanga wa ajali.
Hii imekaaje?
Ni lini na wapi serikali itaamua kuimarisha utayari wa vitengo vya uokoaji wa ajali kama hizi?
Hivi boat za Uokozi za Hiyo inayoitwa Marine Police zilienda wapi?
Mbaya kabisa,Rais wetu anaishia Twitter kwa Rambirambi na kisha kuzamia Misri.
Kati ya V8 na vifaa vya uokozi,kipi ni kipaumbele cha taifa?
Je!
Hata waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mh Byabato.....
Hakuona Umuhimu wa kutuma kikosi maalum cha Marine Navy na Helkopta za Jeshi kuwahi eneo la tukio.
Badala yake wakategemea vifaa vya kutoka GGM-Geita,Kagera Sugar na SONGORO MARINE kutoka Mwanza?
Je!
Watu wanapopiga kelele za Serikali na waziri husika kuwajibika wanakosea?
Haya bhana....
Alamsikhi!
10101