Wavuvi wa samaki Tanzania wajifunze kwa waturuki

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
670
Uturuki yaingiza dola milioni 9.7 sawa na Tsh bilioni 22.3 katika biashara ya dagaa mwaka 2019. Mauzo ya nje ya dagaa kutoka nchini Uturuki yameongezeka kwa asilimia 1 ikilinganishwa na mwaka uliopita kwa kuuza tani 1996.

Mwaka 2019 tani takribani 1973 za dagaa zimeuzwa kutoka Uturuki na kuingiza dola milioni 9.7 katika uchumi wa Uturuki

Kiwango kikubwa cha dagaa wameuzwa nchini Ukraina, Somalia na Syria. Iko haja ya watanzania kujifunza kitu kwa wizara ya kilimo na uvuvi kujifunza kitu ili Tanzania ianze kusafirisha mazao yanayotokana na uvuvi kwa tija.

Na isiwe kama ilivyo hivi sasa kuwa hata samaki vibua walio wengi tunaingiza kutoka Japan, ilhali tuna mito, mabwawa, maziwa na bahari za kutosha

Kila kitu ni fursa ili tusipofikiri kwa upana, tutakuwa masikini mbali na kuwa na rasilimali za kutosha katika nchi yetu

Hali hiyo kiuchumi inaonyesha kuwa masoko yapo, ni kiasi cha sisi kuwa na tija katika uvunaji wa mazao yanayotokana na mito na bahari. Tuna taasisi nyingi ambazo zinaweza fanya tafiti na mikakati ya kuweza kukuza sekta ya uvuvi, kwa kuwa tuna idara ya uvuvi kwenye kila halmashauri, tuna TAFIRI(Tanzania Fisheries Research Institute) tuna FETA nk

Kama hizo taasisi tunaanzisha ili kuwapa ukurugenzi baadhi ya watu wetu, basi haina tija wala maana lakini kama tuna hizo taasisi, idara na mashirika kwa ajili ya kukuza uchumi basi ni muhimu kuwa na malengo na mikakati ya kukuza uchumi kupitia hivi tulivyo navyo.

Uturuki ni nchi ndogo sana ukilinganisha na Tanzania, ina zungukwa na bahari mbili tu, Mediteranian sea na Black sea, huku ikiwa na maziwa kadhaa ndani yake, lakini njoo kwetu uangalie Indian Ocean ilivyotamalaki ukanda wa pwani kuanzia Mtwara, Dar, Pwani, na Tanga, liko ziwa Victoria, Tanganyika, Nyasa, na mengine madogo mengi, tunashindwaje kuproduce zaidi ya uturuki.

Sio kesi, lakini ni wakati wa vijana kujivika uzalendo ambao haupo kwenye maandamani wala fujo bali kufanya mabadiliko kwenye nafsi zetu ili kuangalia uendelevu wa tunayoyafanya

Signed
Oedipus
 
Hivi lile zoezi la kupima samaki na rula limeisha?
Laiti ungejua vikwazo wanavyokutana navyo wavuvi hapa uswatini wala usingekuja kuwalalamikia wao na kuwaona ni wazembe.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
 
Hivi lile zoezi la kupima samaki na rula limeisha?
Laiti ungejua vikwazo wanavyokutana navyo wavuvi hapa uswatini wala usingekuja kuwalalamikia wao na kuwaona ni wazembe.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
Lile zoezi lilikuwa la hovyo sana aisee..
 
Hivi lile zoezi la kupima samaki na rula limeisha?
Laiti ungejua vikwazo wanavyokutana navyo wavuvi hapa uswatini wala usingekuja kuwalalamikia wao na kuwaona ni wazembe.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
Kuna mwaka Tanzania ilikuwa inaingiza dola 100 Milioni kabla ziwa Victoria halijakaukiwa sangara. Lakini hoja ya mtoa mada INA mashiko maana meli aliyoshika mh.Magufuli ilikuwa na samaki Wa dola 1.2 Milioni na huko deep sea mameli yako mengi Kila wakati yanavua. Namibia hawatuzidi ukanda Wa bahari lakini wanuza nje samaki dola 300 Milioni. Nikidhani mkulu akiwa ikulu atashupalia wizi Wa baharini lakini naona sio agenda yake sasa hivi. Sijui MTU akiingia ikulu analishwa nini hadi anasahau mambo ya msingi kama hayo. Au viongozi wetu wakifika huko juu wanapewa mgao au hisa wamezee? Uingereza ni nchi ndogo sana lakini inauza samaki nchi za nje samaki Wa dola 700 Milioni kwa mwaka .Tanzania tunakwama wapi. Pamoja na kuwa uingereza ni kisiwa lakini sins hakika kama INA maji mengi ya kuvua kutushinda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mwaka Tanzania ilikuwa inaingiza dola 100 Milioni kabla ziwa Victoria halijakaukiwa sangara. Lakini hoja ya mtoa mada INA mashiko maana meli aliyoshika mh.Magufuli ilikuwa na samaki Wa dola 1.2 Milioni na huko deep sea mameli yako mengi Kila wakati yanavua. Namibia hawatuzidi ukanda Wa bahari lakini wanuza nje samaki dola 300 Milioni. Nikidhani mkulu akiwa ikulu atashupalia wizi Wa baharini lakini naona sio agenda yake sasa hivi. Sijui MTU akiingia ikulu analishwa nini hadi anasahau mambo ya msingi kama hayo. Au viongozi wetu wakifika huko juu wanapewa mgao au hisa wamezee? Uingereza ni nchi ndogo sana lakini inauza samaki nchi za nje samaki Wa dola 700 Milioni kwa mwaka .Tanzania tunakwama wapi. Pamoja na kuwa uingereza ni kisiwa lakini sins hakika kama INA maji mengi ya kuvua kutushinda.

Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo kubwa hatuna kipaumbele katika sekta ya uvuvi na kilimo,
Pia hamna sera na hamasa ya kutosha katika exportation ya bidhaa zetu za ndani za kilimo, mifugo na uvuvi.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
 
Tatizo kubwa hatuna kipaumbele katika sekta ya uvuvi na kilimo,
Pia hamna sera na hamasa ya kutosha katika exportation ya bidhaa zetu za ndani za kilimo mifugo na uvuvi.

Sent from my DUB-LX1 using Tapatalk
Sera yetu n kukusanya kodi kwa wananchi huon saiv tunapata tri 1.3 kwa mwez
 
Back
Top Bottom