Bhbm
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 714
- 208
Ninaomba kujuzwa wanajf wenzangu, je ni nafaka aina gani zinaweza kuwa na soko zuri hapa mjini Dar? Na je ni mtaji kiasi gani naweza kuanzia nao? Natanguliza thanks.
WADAU WANAOHITAJI MIONGOZO KUHUSU BIASHARA HII
Wanajamvi hope wote mu wazima wa afya njema.
Nataka kufànya biashara ya mazao hasa mahindi na nafaka zingine; lakini kwa kuanzia nataka nianze na mahindi kwanza halafu mtaji ukikua nitaongeza wigo wa mazao mengine.
Ninaomba mnisaidie namna ya kupata mazao huko mikoani ni njia gani zinazotumika ili kuweza kufanikisha kupata mzigo ndani ya muda mfupi na kuuleta Dar?
Pia naomba mnijuze mikoa au wilaya ambazo naweza pata mahindi mengi kwa bei nzuri na ambapo kuna mazao au mahindi ya kutosha ili ukusanyaji uwe wa haraka.
Kuhusu soko kwa hapa Dsm hakuna tatizo kwani nimepata mteja ambaye atachukua. ni mteja wa uhakika kwa hivyo kwa upande wa soko sina tatizo.
Tatizo ni huko mikoani ndio sijui nianzie wapi nimalizie kwa suala zima la ukusanyaji na upatikanaji wa mahindi.
Mtaji wa kuanzia ni 10m nataka kuanza mara moja biashara hii kwa anayejua naomba anisaidie kunielekeza sehemu au mikoa ambayo naweza pata mahindi na pia mbinu za ukusanyaji sbb mi ndio naanza na sio mwenyeji wa biashara hii nahitaji kupata uzoefu kwa wanaofanya au waliokwishakufanya au wanaofahamu.
Thanks in advance
Wanajamvi,habari zenu.
Naomba mwenye ujuzi kuhusu biashara ya mazao anijuze vitu kadhaa,by the way nataka nipate uelewa kidogo kuhusu biashara ya mazao hususan NAFAKA
Mimi ni mmoja kati ya wanaosubiri ajira toka serikalini baada ya kuhitimu chuo.Mpaka sasa nimeshakaa muda mrefu bila ajira ukiacha dili ndogondogo za hapa na pale,nimechoka kukaa bila kuwa na kitu maalum cha kufanya.
Nimepata wazo,na mimi nianze biashara ya mazao yaani niwe nasafiri kwenda vijijini kuchukua/kununua mazao(NAFAKA) Mfano;Ufuta,mahindi,karanga,alizeti na mpunga.
Tatizo ni kwamba sijawahi kufanya biashara yoyote ile,hivi karibuni nilizungumza na rafiki yangu mmoja ambaye yupo kijijini(DODOMA),Yeye anafanya biashara ya mpunga/mchele.ananunua huko kijijini na kuleta mjini.na kuna mjomba wangu yupo hapa mjini,yeye ana store ya mazao hususan Ufuta kwa sasa(maana ndo msimu wake),ananunua na kuuza.
Mjomba yupo tayari kuniunganisha na mtu anayeenda vijijini kununua ufuta anayemfahamu/anayemuamini niende nae vijijini akanifundishe kazi,na rafiki yangu yupo tayari niungane naye kwenye biashara ya mpunga,Wote wawili niliwauliza maswali kadhaa ambayo ningependa na nyinyi wanajamvi mchangie (mengine sikuyauliza kabisa japo yapo hapo chini)
1. Mtaji wa kuanzia wa mpunga/ufuta minimum inaweza kuwa kiasi gani?
2. Bei ya kununua mpunga/ufuta vijijini
3. Gharama za usafirishaji wa mpunga/ufuta
4. Vifaa vya muhimu vya kwenda navyo vijijini mfano;vifaa vya kuhifadhia/packaging kama magunia nk. na gharama zake.
5. Inachukua muda gani kujaza mzigo wa pesa kama 1,000,000/= kwa mpunga/ufuta
6. Faida kwa kila gunia la ufuta/mpunga
7. Upatikanaji wa soko(DODOMA)
8. Bei ya kuuza kwa kila gunia la ufuta/mchele namaanisha kwa kilogram.
9. Challenges/risks za biashara hii ya ufuta/mpunga
10. Matakwa ya kisheria na kodi (mfano VAT) Ipoje?
11. Mengineyo,ambayo sijayaorodhesha hapo juu,tafadhali
NB: Wote wawili walikuwa na uelewa juu ya debe maarufu kama "mozambique" .hili debe lipoje?,kwa nini litumike?,bei ya hlo debe ni kiasi gani? lina tofauti gani na debe la kawaida?
Natanguliza,shukurani.
Ndugu zangu wanajamii,
Mimi nilikuwa nataka ushauri wa biashara ya duka la nafaka na mazao ya muhimu ambayo ni chakula kwa binadamu; yenye mzunguko mzuri kwa biashara.
Heshima kwenu wakuu!
Nimekuwa nikiwaza muda mrefu kuanza biashara ya kilimo. Ninaipenda sana japo sijawahi kuifanya. Nimetamani kuanza kununua mazao ama kwa kuyauza moja kwa moja au kwa kuyatunza katika ghala ili niwe nauza baadaye bei ikiwa nzuri.
Ninao mtaji kidogo kwa kuanzia lengo ni ili niweze kukua kidogo kidogo na sio kuweka pesa nyingi ambayo ninaweza kula hasara kipindi naanza biashara hii.
Sijachagua mazao maalum ya kuanza nayo na ndio maana nahitaji mawazo yenu.
Hivyo basi nipo hapa kuomba ushauri ni mazao gani ninaweza kuanza nayo, mtaji mdogo ambao unaweza kufaa kuanza nao ni kiasi gani, maeneo na masoko ya biashara ya mazao ndani na nje ya nchi ni yapi?.
Nitashukuru hata kwa ushauri wa ziada mtakaonipa.
Habarini wana JamiiForums, ebwana mimi ni kijana na ninatamani sana kuingia katika biashara ya nafaka ila nacho hitaji kufahamu ni wapi naweza pata mazao ya nafaka kama karanga, dengu, mtama, ufuta, ulezi nakadhalika kwa bei za jumla.
Au kama unaweza kujua bei za jumla mkoani kwako mnaweza nijuza naombeni usaidizi kwa hilo jamani.
IFAHAMU BIASHARA YA MAZAO YA CHAKULA
Haijalishi watu ni masikini kiasi gani, wala hali ya kiuchumi ni mbaya kiasi gani, lakini chakula na hasa hasa nafaka kitabakia kuwa hitaji la msingi kabisa la binadamu likifuatiwa na mavazi na malazi. Katika biashara zote, biashara ya kuuza mazao ya chakula kama vile mahindi, mchele, unga wa sembe na dona, maharage, sukari, unga wa ngano na mafuta ya kula ndiyo itakayokuwa ya mwisho kudorora.
Mazao ya vyakula, hususani yale ya nafaka kama mahindi, mpunga, ngano, mtama, mihogo, maharage na jamii zake, pamoja na ulezi vimekuwa na mchango mkubwa sana katika kuongeza fursa za kiuchumi kutokana na sababu kubwa kwamba vyakula hivi ni muhimu kwa binadamu wote duniani bila ya kujali rangi, dini, kabila wala eneo analotoka mtu. Kuanzia Afrika, Asia, Ulaya, Australia, mpaka Marekani ya kusini na Kaskazini, hakuna mtu asiyetumia nafaka hizi.
Sekta hii hufanya kazi katika ngazi tofauti kwenye jamii, kuanzia, ngazi ya kaya ambao mara nyingi hawa ni wakulima wadogowadogo wanaozalisha mazao haya kwa kiasi kidogo tu kwa ajili ya chakula cha kujikimu na familia zao na mara chache kwa ajili ya kuuza kupata fedha kwa ajili ya kununulia mahitaji mengine madogomadogo ya familia. Kuna wakulima wakubwa au makampuni yanayolima mazao ya chakula kwa ajili ya biashara, makampuni ya ndani na wafanyabiashara wakubwa wanaonunua na kuuza mazao ya chakula ndani na nje ya nchi na makampuni makubwa mengine hujihusisha na biashara hii kwa namna moja au nyingine kwa ajili ya soko la Kimataifa.
Wapo wafanyabiashara wanaojihusisha na kununua nafaka kama mahindi na mpunga halafu huenda kukoboa au kusaga, biashara ya kukoboa na kusaga mahindi kwa mfano ni maarufu sana jijini Dar es salaam hasa maeneo ya Manzese na Tandika. Wafanyabiashara hao hasa kina mama wengi wamenufaika sana na biashara hii na huwapatia kipato na faida nyingi. Kuna wanaojihusisha na utengenezaji wa vifungashio tu pamoja na kuweka nembo na wapo wanaojihusisha na uuzaji peke yake. Hawa wanamiliki maduka ya kuuza unga, mchele na nafaka nyinginezo kama maharage nk.
Katika mgawanyo katika sekta ya biashara ya mazao ya biashara, utakuta ni mamilioni ya watu, karibu asilimia 90 ya watu wote katika nchi zinazoendelea kama Tanzania hujihusisha kwa namna moja au nyingine na biashara au ukuzaji wa mazao ya chakula. Lakini bado kuna tatizo moja, watu wengi wanalalamika sekta hii kutokuwa na tija ya kutosha, watu hao wengi watakuambia, kilimo bwana hakilipi, mazao ya chakula ni biashara kichaa haitabiriki, wengine watakuambia kilimo cha mazao kinahitaji mtaji kama biashara zingine hivyo hawana uwezo wa kupata mitaji nk.
Wakati watu hao hasahasa wale wanaoishi mijini wakilalamika na kutoa sababu hizo kibao, bado wapo na wanaendelea kuishi mijini huku wakilalamika kupanda kwa bei ya unga wa sembe na dona. Ukiwauliza wanadhani sababu ya chakula kuwa bei juu kiasi hicho ni nini, wanakujibu majibu wasiyokuwa na uhakika nayo kama vile, mvua haikunyesha ya kutosha, wakulima hawana pembejeo, serikali mpya imekuja na sera mpya ya kupandisha vyakula bei, watu wengi wamekimbilia mijini, shamba hakuna tena walimaji, ni mbinu ya madalali wa mazao kujipatia faida kubwa nk.
Ni kweli pamoja na kwamba ukame unaweza kuwa chanzo kikubwa cha kupanda kwa kasi kwa mazao ya chakula hasa mahindi na mazao yake kama unga wa dona, unga wa sembe na pumba za kulishia wanyama, lakini swali moja la kujiuliza ni kuwa, mbona mazao mengine kama mpunga hayakuathirika kiasi hicho? Ina maana huo ukame ulichagua mahindi na maharage peke yake? Labda unaweza ukasema ni kwa sababu watu wengi hapa Tanzania chakula chao kikubwa ni ugali.
Sababu zote hizo kwa mfano ingelikuwa ni nchi zilizoendelea sidhani kama zingelikuwa na nguvu kama hapa kwetu, usalama wetu wa chakula kwa ujumla haupo imara na hii haiwezi kuwa ni kutokana na sababu hizo zilizotajwa hapo juu, Watanzania kuna hatua tunatakiwa kuchukua ikiwa tutataka kuondokana na hali kama hii nyakati zijazo.
Kama Taifa lilivyoamua kuachana na kutegemea umeme wa maanguko ya maji kama wa mabwawa ya mtera, Kidatu na mengineyo baada ya majanga ya umeme kama yaliyosababisha Richmond, Dowans na skendo zingine kibao za uneme, katika suala la mazao ya chakula pia zinatakiwa zichukuliwe hatua na mikakati mbalimbali. Na hatua hizo si kuiachia tu serikali peke yake, ni suala linalotakiwa kuchukuliwa kwa uzito na wadau wote kwenye sekta wakiwemo wakulima, wafanyabiashara ya mazao ya kilimo, makampuni mbalimbali na mashirika makubwa.
Tatizo kubwa la nchi kama Tanzania hatutumii teknolojia kuhifadhi mazao, kwa mfano mahindi yakishavunwa yangeweza kuhifadhiwa vizuri na kisha kuja kuuzwa baadae wakati wa upungufu wa mahindi lakini hili hufanyika kwa kiasi kidogo sana tena na serikali, kwa upande wa wafanyabiashara siyo wengi wanaofanya hivyo husubiri kwenda kununua tu yaliyokwisha hifadhiwa.
Ikiwa kama utaamua kuwa serious na biashara ya nafaka kwa kutumia teknolojia zinazowezesha mazao kama mahindi kukaa kwa muda mrefu pasipo kuharibika, unaweza kutengeneza pesa nyingi sana katika kipindi cha muda mfupi tu.
Wakulima wadogo kwa upande wao wakisha vuna mahindi mengi wengine huyatumia bila mpango mzuri mfano kutengenezea pombe za kienyeji na kuyauza bei rahisi jambo linayoyafanya yaishe ndani ya kipindi kifupi. Utakachokifanya ni kuwekeza fedha zako kwenye ununuzi wa mahindi au na nafaka nyinginezo kama maharage kipindi cha mavuno kisha unayahifadhi kitaalamu kwa muda wa miezi kadhaa tu au mwaka halafu unaangalia vipindi vyenye upungufu wa mazao ndipo unauza.
Kilimo cha mahindi pia watu wamekuwa wakitegemea mvua zaidi, na zinapokuwa haba na mavuno nayo huwa haba. Tazama zao kama mpunga na ngano, mchele na ngano huzalishwa kwa wingi na makampuni makubwa tena kwa kiasi kikubwa kwa njia za umwagiliaji na ndiyo sababu hata unaweza ukaona mazao haya hayawezi kuathirika sana na ukosefu wa mvua kama ilivyokuwa kwa zao la mahindi.
Faida za kutumia makampuni makubwa kuwekeza katika biashara ya uzalishaji na uuzaji wa mazao ya chakula ni kwamba, huzalisha ajira wakati huo huo yakihakikisha usalama wa chakula unakuwepo. Makampuni makubwa yanakuwa na mitaji mikubwa hivyo kuwa na uwezo mkubwa pia katika uhifadhi na utunzaji wa mazao hayo kabla ya kuuzwa au kutumiwa katika shughuli za kuzalisha bidhaa nyingine. Yanakuwa pia na uwezo mkubwa wa usafirishaji wa mazao katika maeneo mbalimbali ya nchi yanakohitajika au nje ya nchi.
Ndiyo maana nasema bado fursa ni kubwa katika sekta hii tofauti na vile watu wengi mijini wanavyofikiri. Mwaka huu wafanyabiashara waliothubutu tu hata kuanzisha biashara ya kuchukua mazao kutoka mikoa inayozalisha nafaka kwa wingi kama vile, Mbeya, Ruvuma, Sumbawanga, Morogoro na Iringa wengi wao wanacheka, hawawezi kukuelewa ukiwaambia eti biashara zimedorora kwani katika maduka yao kila kukicha watu ni foleni, utasikia wakisema, “nipimie unga kilo 5”, “ nipimie mchele kilo 10”, wengine, “naomba mchele wa mbeya super”, maharage ni shilingi ngapi?”, sembe imepanda tena?” nk.
Tabia ya watu kupenda kula unga wa sembe nayo kwa kiasi fulani inachangia uhaba wa chakula hususani mahindi kwani kiasi kinachopotea kwenye pumba baada ya mahindi kukobolewa ni kikubwa, wanaofanya biashara ya kukoboa na kusaga mahindi wanafahamu sana ni kiasi gani cha pumba kinachopotea. Na kwa bahati mbaya zaidi ugali au unga wa mahindi yaliyokobolewa ni hatari kwa afya za walaji. Unaweza kuona unga wa sembe kuwa ni mzuri machoni au unapokula lakini kiafya ni majanga makubwa, ni chanzo kikubwa cha magojwa yasiyoambukiza kama kisukari, presha na hata unene kupita kiasi. Ingawa dona nayo wakati mwingine inaweza kuwa siyo nzuri sana endapo mahindi yatasagwa bila ya kuaosha vizuri, lakini kama yatasafishwa kikamilifu na kuondolewa yale yaliyoharibika ndicho chakula kizuri chenye afya.
Kuna kasumba nyingine ya watu kutokupenda kula baadhi ya vyakula kwa kuviona kama ni vyakula duni vinavyostahili kuliwa nyakati za njaa tu, vyakula kama vile ugali wa muhogo, ugali wa mtama, uwele na magimbi. Tumezoea kula ugali wa mahindi, wali, viazi, ndizi, mihogo ya kukaanga au ya kuchemsha, tambi na kande tu, wakati vyakula kama ugali wa mtama ni chakula kizuri sana chenye virutubishi vingi na nyuzinyuzi zinazosaidia usagaji mzuri wa chakula tumboni.
Fursa nyingine kubwa kwa wanaopenda kuanzisha makampuni ya kudili na mazao ya chakula hasa nafaka ni kama hii ya kuhakikisha kwa mfano kampuni yako inakuja na mbinu na mikakati mipya ya kijasiriamali kama vile kusaga nafaka na kuzifungasha(pack) katika ubora wa hali ya juu, mandhari ya kuvutia mahali unapofanya shughuli hizo ukizingatia mtu ni afya. Kuwa na nembo(logo) yako mwenyewe iayokutambulisha kibiashara ni muhimu pa. Kwa ujumla hakikisha kampuni yako inakuwa tofauti na kampuni au biashara nyingine zinazojihusisha na biashara ya mazao ya chakula au nafaka.
Ukishakuwa na jina, (brand) yako nzuri unaweza ukauza bidhaa zako kama ni unga wa mahindi unga wa ulezi, unga wa mtama, mafuta ya kupikia, maziwa au chochote kile kinachohusiana na nafaka au chakula nchi nzima na hata nje ya nchi kama vile unavyowaona makampuni kama akina Azam, METL, Azania, Tanga Fresh na wengineo .
Chanzo: jifunzeujasiriamali.co.tz
MICHANGO YA WADAU
LENGA KUONGEZA THAMANI YA NAFAKAKushauri jambo moja:
- Katika swala zima la biashara ya nafaka ni bora ukajikita katika ku ad value au kuongeza thamani ya hizo nafaka
1. Ni bora ukawa na ofisi yako mjini na jaribu kuyaongezea thamani hayo mazo kama vile kugred na kupark kabisa. Hapo utakuwa umeongeza thamani na utauza kwa bei ya juu, na unaweza tafuta hata supermaket tano tu za kuwa sambazia.
2. Hili la kununua mchele kutoka mbeya na kuja kuuza dar kama ulivyo hakuna cha maana sana mtu nacho pata zaidi ya ujanja ujanja wa kuchanganya. Mtu anachukua mchele wa mbeya na kuchanganya na mchele wa Morogoro
Hii biashara ya nafaka si kwa mba inalipa sana ila ni ujanja ujanja unao fanywa na wauzaji kwa kuchanganya changanya. Anaweza chukua gunia la maharage safi akachanganya na nusu gunia la maharage mabovu ndo business inaenda.
Ujanja ujanja ni la muda sana na si endelevu.
So jitajidi upate hata mashine ya kupaki kwenye mifuko, mfano ukipata mashine moja inayo itwa heavy duty sealing machine ni nzuri sana unaweza ukawa na vibarua wako wa kugred na wewe ukawa unapaki na kuuzia watu wa supermarket.
Hiyo mashine niliyo kuambia ni ambayo ina silidi kama vile totopark zinavyo kuwa zimefungwa kwenye vile viloba.
Kuna kampuni moja ya kenya ina tengeneza vifungashio vizuri sana unweza cheki huko
NI MUHIMU KUJIULIZA MASWALI HAYAMilioni tano yaweza kukutoa au yaweza kushindwa kulingana na maswali yafuatayo!
Mkuu, nafaka zinatofautiana maana kuna, mpunga, mahindi, maharagwe, mtama, uwele, ngano, soya, etc, sasa ni nafaka zipi utahitaji kuzinunua?
Utaenda kununua kwa njia ya kukopesha wakati wa kulima ili upate mavuno baadae? Au utasubiri kipindi cha mavuno?
Jiulize, ni sehemu zipi za Tz unategemea kwenda kununua?
Soko lako litakuwa wapi?
Ni wewe mwenyewe unategemea utaifanya hii kazi au utaajiri watu/agents?
Usafirishaji je, utakodi au unao binafsi?
UBORA NA FAIDA YA MCHELEIli kujua mpunga kama ni mzuri huwa tunachukua sample na kuumenya na kisha kutathmini ubora wake-mzuri hutoa punje zilizonyooka na nyeupe wakati mbaya hutoa mpunje zilizovunjikavunjika, ama nyekundu badala ya nyeupe.
Pia ubora wa punje/mchele huweza tegemeana na mashine uliyokobolea na technician anaeseti mashine-kuna mashine zenye wataalam wa kuseti mashine kulingana na mpunga unaokobolewa kwa wakati husika na mchele wote utokao kwenye mashine hizo ni "super" au ulionyooka tu.
-Ubora wa mchele hutathmini faida utakayopiga wakati wa kuuza mchele huo
Kwa mtaji mkubwa wa kuweza kununua tani hata 2 za mchele ni vyema ukauza mchele pale bei ya mchele inapokuwa juu zaidi sokoni wakati mashineni ukiuzwa kwa bei ya chini. Kwa mfano kama mashineni unauzwa kwa Tsh.800 kwa kilo na kuuzwa kwa Tsh. 1400 sokoni na wewe ukanunua tani 2 kwa Tsh. 1,600,000/- na kuuza kwa Tsh. 2,800,000/- wakati gharama ya usafiri ni kama 90,000/- kama utakuwa umetoa mzigo Shinyanga kuja Dar kwa mfano, hapo unakuwa umetengeneza faida ya 700,000/- kwa safari moja.
-Faida itaongezeka kutegemeana na safari unazofanya kwa wiki yaani safari moja, mbili au tatu; na hii inaonesha atakaepiga faida zaidi ni yule anaenunua mchele na kusafirisha moja kwa moja kuliko anaechukua mpunga na kupanga mstari mashineni ili akoboe ambapo anaweza koboa tani chache tu siku.
Kuna wakati pia kununua mpunga na kuuhifadhi kwa ajili ya kukoboa na kuuza baadae kunalipa sana, kwa mfano ikiwa leo gunia linauzwa kwa Tsh. 55,000/- na ukanunua na kulihifadhi hadi mwezi wa 12 (2016) au kwanza mwakani (2017) ambapo bei inaweza kuwa 85,000/- hadi 100,000/- kuna uwezokano wa kupiga faida isiyopungua 25,000/- kwa gunia kama utauza mpunga kama mpunga; ukikoboa na kuuza mchele unapiga zaidi ya hiyo (25,000/-)
Kwa ujumla ni vyema kipiga zote (mchele na mpunga) kulingana na kile kinachotoa faida zaidi kwa msimu husika, eneo unalofanyia biashara kama vyote vinapatikana kama mpunga haupatikana usione tabu kwenda maeneo ama mkoa wanakolima na nununua kisha hifadhi au koboa-ukiwa mfanyabiashara lazima uzungukie maeneo ya interest yako na utajua mikoa mingi na hata vijiji vingi nchini na umbali kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine hususani ukishakuwa na usafiri wako.
USIPIME KINA CHA MTO KWA MIGUU YOTEHongera kwa kutaka kujuajiri kupitia biashara ya nafaka. Nikwambie tu kila biashara unayoiona watu wanafanya ujue inalipa ndio maana watu wanafanya. Kusema inalipa vipi hapo kila mtu anakuwa na siri yake na utofauti unakua katika kujiongeza tu. Kitu kikubwa fanya utafiti na nikwambie tu ukweli hakuna utafiti mwepesi.
Usifanye utafiti kwa kuuliza watu tu, hakika hauta pata taarifa zote na hawata funguka mambo yoote, kuna vitu vidogo vidogo sana watu huwa wanasahau kueleza na wewe katika hesabu zako unaviacha na mwisho wa siku unakumbana na vyo gafla, na kama hauko makini unaweza kukimbia.
Katika tafiti zako uliza mambo ya msingi mfano unapo kaa na wauzaji kwanza usioneshe interest kama unatarajia kufanya biashara hiyo kwani wengi hudhani kuwa unapo muuliza basi umesha mchiunguza na kugundua anafaidika na hivyo atahisi unataka kuleta ushindani na uue hayo ni maisha kwake na hato ruhusu umvuruge kwa kuleta bidhaa sawa na yeye, hofu zaidi huwa ni kugawa wateja.
Anza urafiki na huyo unayetaka kumpeleleza na unaweza amza kama mteja tu wa hata kilo moja na kabla ya kununua ndipo vistori vyako vianzie hapo. Katika maswali yako yanaweza mpa picha kama unataka kujua kitu na anapo gundua ni vema umuonesha kuwa hilo ni ambo ungependa kufanya baadae na pia hauna mpango wa kufanyia mkoa huo na mauanjanja mengine ujuavyo wewe.
Unatakiwa kuchukua kiasi kidogo kama robo tu ya mtaji wako na kuanza nao na safari ya kwanza usitarajie faida maana kutaibuka vimbwanga ambavyo hukuambiwa na hapo ndio utaanza kujifunza na kujua ufanyeje. Kasoro unazo kutana nazo kila wakati ndio kujifunza huko na mwisho wa siku utakuja kuwa mtaalamu na kushauri wengine. Usianze na mtai wote "usipime kina cha mto kwa miguu yote".
Vinginevyo mi naona kila biz inalipa ni wewe tu uchague unaanza na nini.
PIA, SOMA: