Waumini watengwa kwa kuichagua CCM

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mamia ya waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, mkoani Rukwa, wamejikuta katika wakati mgumu baada ya uongozi wa kanisa hilo kutangaza kuwatenga na wengine kufukuzwa kutokana na madai ya kukiuka kanuni za kanisa hilo.
Habari za uhakika ambazo zimethibitishwa na baadhi ya waumini hao waliokumbwa na mkasa wa kutengwa na kufukuzwa walidai kuwa kufukuzwa kwao kumetokana na wao kushabikia Chama cha Mapinduzi CCM) katika kampezi za uchaguzi mkuu uliopita wa Oktoba 31 mwaka huu.

Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja idadi ya waumini waliofukuzwa na kanisa hilo kwa kuwa inadaiwa kuwa ni wa kutoka vigango tofauti vya jimbo hilo na kwamba kila kigango kilipewa taarifa kwa wakati tofauti za waumini wake kusimamishwa au kufukuzwa.

Katika jitihada za kupata ukweli wa tukio hilo, Tanzania Daima ilifanikiwa kuonana na baadhi ya viongozi wa kanisa hilo jimboni hapo ambao walikiri kuwepo kwa tukio hilo.

Padri Deogratius Simemba na Padri Leonard Teza, wa familia takatifu, walipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya sakata hilo, walisema kuwa kwa mujibu wa sheria za kanisa hilo waumini hawaruhusiwi kujihusisha moja kwa moja na masuala ya siasa kwa mgongo wa kanisa, hivyo kama kuna waumini walikiuka wanapaswa kuchukuliwa hatua.

Lakini pia waliongeza kuwa hawakufukuzwa bali tayari walishajitenga na kanisa kutokana na kuidhalilisha imani ya kanisa hilo.
 
Kwanza sijakuelewa unamaanisha nini hapa! pili hauna hushahidi wowote wa jambo hilo.
tatu haipendezi na si vizuri kuleta thread za mambo yanayoweza kuleta misuguano kwenye jamii.
 
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mamia ya waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga, mkoani Rukwa, wamejikuta katika wakati mgumu baada ya uongozi wa kanisa hilo kutangaza kuwatenga na wengine kufukuzwa kutokana na madai ya kukiuka kanuni za kanisa hilo.
Habari za uhakika ambazo zimethibitishwa na baadhi ya waumini hao waliokumbwa na mkasa wa kutengwa na kufukuzwa walidai kuwa kufukuzwa kwao kumetokana na wao kushabikia Chama cha Mapinduzi CCM) katika kampezi za uchaguzi mkuu uliopita wa Oktoba 31 mwaka huu.

Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja idadi ya waumini waliofukuzwa na kanisa hilo kwa kuwa inadaiwa kuwa ni wa kutoka vigango tofauti vya jimbo hilo na kwamba kila kigango kilipewa taarifa kwa wakati tofauti za waumini wake kusimamishwa au kufukuzwa.

Katika jitihada za kupata ukweli wa tukio hilo, Tanzania Daima ilifanikiwa kuonana na baadhi ya viongozi wa kanisa hilo jimboni hapo ambao walikiri kuwepo kwa tukio hilo.

Padri Deogratius Simemba na Padri Leonard Teza, wa familia takatifu, walipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya sakata hilo, walisema kuwa kwa mujibu wa sheria za kanisa hilo waumini hawaruhusiwi kujihusisha moja kwa moja na masuala ya siasa kwa mgongo wa kanisa, hivyo kama kuna waumini walikiuka wanapaswa kuchukuliwa hatua.

Lakini pia waliongeza kuwa hawakufukuzwa bali tayari walishajitenga na kanisa kutokana na kuidhalilisha imani ya kanisa hilo.
uache uzabazabina wewe... ukisoma ulicho-post, hawajatengwa kwa kukipigia CCM bali kukifanyia kampeni kanisani na ni viongozi walipata dhahama hiyo
 
Back
Top Bottom