Mzururaji
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 1,559
- 1,272
Jana zilisambaa picha kwenye social media ambazo zilimwonesha Mhe, lowasa akiwa na viongozi wa serikali na chama cha mapinduzi akiwepo Mhe, rais na Katibu Mkuu wa CCM. Picha ilipigwa kanisan huku viongozi hao wakionesha furaha ya waziwazi akiwepo mama Regina LOWASA,
mbali ya kuwa tunajua wana tofauti.
Misingi ya tofauti ya viongozi hawa ni kabla na baada ya uchaguzi mkuu ambapo baada ya matokeo kutoka Mhe, lowasa alinukuliwa sehemu mbalimbali akisema wamemwibia kura hivyo ushindi ulikuwa wake. Toka kipind cha matokeo hakujawahi tokea picha zenye mwonekano wa namna ile ambazo zilizua minong'ono miongoni mwa wananchi wengi wao wakipongeza na wana ukawa wakimpongeza lowasa hasa kuelekea sept mosi.( siku ya UKUTA) Kama utakuwepo.
Kikubwa kilicho zua minong'ono ni aina ya pozi likiwaonesha ni watu wenye furaha na kwamba hakuna lolote kati yao hapa imedhihiri mambo ya majukwaani wameyaweka pembeni na pale walikuwa wanahudhuria ibada ya kikristo ambapo waumini huondoa kinyongo chochote ili kukaribia madhabahu ya Bwana.
Kwa wakristo eneo la msiba na kanisan ni maeneo ya ibada ambapo waumini huwa wanakatazwa kufanya mambo ambayo ni dhambi ambayo yatafanya sala ya toba isipokelewe ndo mana ikaandikwa samehe saba Mara Sabin.
Lakini hayo yakijili kule visiwani kuna waumini wenzetu waligoma kusalimiana kisa siasa tena eneo la msiba. Picha nyingi zilisambaa zikimuonesha maalim seif akigomea salam ya mkono kutoka kwa muumini mwenzie dr shein. Mimi naamini haikuwa sehemu sahihi kuonesha tofauti kwani kwa mujibu wa dini ya kiislam msiba ni ibada ambapo muumini anapata muda wa kutafakari mapito yake wapi anatoka na wapi anaenda ili kujiandalia mwisho mwema kwa mola wake.
Hapa waumini wa kiislam tuna la kujifunza kutoka kwa viongozi hawa waumini wa kikristo ambapo Jana walionesha umoja eneo la kanisa badala ya utengano hapa tegemea kuona wakristo wakiwa wamoja zaidi kupitia viongozi wao ambao wana uwezo Mkubwa kuficha hisia zako kwani kupitia matendo haya ndipo wananchi huungana
Kwetu sisi viongozi ambao ni waumini wa kiislam tunapaswa kujua kuwa waumini wenzetu wanatuangalia na wanajifunza kitu kikubwa kutoka kwetu. Ingawa mnaweza kuhisi kuwa nyie ni viongozi wa kisiasa tuu.
Kwenye majukwaa yenu ya siasa huko haina tatizo lakni tofauti mnapo kuja kizionesha eneo la msiba na nyumba za ibada zinabomoa umoja wa waumini wenzenu.
Mwisho nimpongeze Mhe LOWASA kwani nae alikuwa na nafasi kama yule mwingine kugomea salam au hata kununa.
©malibwadu;-
Kwa sasa mafunzoni kilombero.
mbali ya kuwa tunajua wana tofauti.
Misingi ya tofauti ya viongozi hawa ni kabla na baada ya uchaguzi mkuu ambapo baada ya matokeo kutoka Mhe, lowasa alinukuliwa sehemu mbalimbali akisema wamemwibia kura hivyo ushindi ulikuwa wake. Toka kipind cha matokeo hakujawahi tokea picha zenye mwonekano wa namna ile ambazo zilizua minong'ono miongoni mwa wananchi wengi wao wakipongeza na wana ukawa wakimpongeza lowasa hasa kuelekea sept mosi.( siku ya UKUTA) Kama utakuwepo.
Kikubwa kilicho zua minong'ono ni aina ya pozi likiwaonesha ni watu wenye furaha na kwamba hakuna lolote kati yao hapa imedhihiri mambo ya majukwaani wameyaweka pembeni na pale walikuwa wanahudhuria ibada ya kikristo ambapo waumini huondoa kinyongo chochote ili kukaribia madhabahu ya Bwana.
Kwa wakristo eneo la msiba na kanisan ni maeneo ya ibada ambapo waumini huwa wanakatazwa kufanya mambo ambayo ni dhambi ambayo yatafanya sala ya toba isipokelewe ndo mana ikaandikwa samehe saba Mara Sabin.
Lakini hayo yakijili kule visiwani kuna waumini wenzetu waligoma kusalimiana kisa siasa tena eneo la msiba. Picha nyingi zilisambaa zikimuonesha maalim seif akigomea salam ya mkono kutoka kwa muumini mwenzie dr shein. Mimi naamini haikuwa sehemu sahihi kuonesha tofauti kwani kwa mujibu wa dini ya kiislam msiba ni ibada ambapo muumini anapata muda wa kutafakari mapito yake wapi anatoka na wapi anaenda ili kujiandalia mwisho mwema kwa mola wake.
Hapa waumini wa kiislam tuna la kujifunza kutoka kwa viongozi hawa waumini wa kikristo ambapo Jana walionesha umoja eneo la kanisa badala ya utengano hapa tegemea kuona wakristo wakiwa wamoja zaidi kupitia viongozi wao ambao wana uwezo Mkubwa kuficha hisia zako kwani kupitia matendo haya ndipo wananchi huungana
Kwetu sisi viongozi ambao ni waumini wa kiislam tunapaswa kujua kuwa waumini wenzetu wanatuangalia na wanajifunza kitu kikubwa kutoka kwetu. Ingawa mnaweza kuhisi kuwa nyie ni viongozi wa kisiasa tuu.
Kwenye majukwaa yenu ya siasa huko haina tatizo lakni tofauti mnapo kuja kizionesha eneo la msiba na nyumba za ibada zinabomoa umoja wa waumini wenzenu.
Mwisho nimpongeze Mhe LOWASA kwani nae alikuwa na nafasi kama yule mwingine kugomea salam au hata kununa.
©malibwadu;-
Kwa sasa mafunzoni kilombero.