Wauguzi wawili Manyoni wasimamishwa kazi kwa kusababisha mkono wa mtoto wa miezi minne kuoza

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,480
9,236
oza.png


Wauguzi wawili wa Hospitali ya wilaya ya Manyoni mkoni Singida wamesimamishwa kazi,baada ya kumwachia mtoto wa miezi minne kamba kwa muda wa zaidi ya masaa nane ,ambayo waliifunga mkononi kwaajili ya kumwekea dripu ya maji na kusababisha mkono kuoza.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni Bwana Charles Fussi ametoa uamuzi huo baada ya kujirizisha kwa kukaa vikao na uongozi wa hospitali na wao wauguzi Bi.Salima Mkoka na Bi.Specioza Mchunguzi kukiri kusahau kutoa kamba hiyo na kusababisha mkono wa mtoto Cecilia Dastani kuharibika na unaweza kukatwa.

Wakieleza daktari ambapo tukio lilipotokea katika hospitali ya wilaya ya Manyoni Daktari Nelson Bukuu Mganga mkuu wa wilaya amekiri kuwa wauguzi wake wamesahau kwa bahati mbaya hadi siku ya pili,huku Mganga mkuu wa Hopitali ya St Gasper Itigi alipolazwa baada ya kupewa rufaa daktari Anatori Lukonge amesema mtoto Cecilia anaweza kupoteza baadhi ya vidole au kukatwa mkono.

Kwa upande wake mama mtoto Bi Violet Ernest mkazi wa Sasilo wilayani Manyoni amesema hakujua kwanini mtoto wake alikuwa akilia sana tokea awekewe dripu saa saba mchana mpaka siku ya pili asubuhi alipoambiwa daktari na kuja kutambua tatizo hilo .



Chanzo; IPP media
 
Wauguzi wawili Manyoni wasimamishwa kazi kwa kusababisha mkono wa mtoto wa miezi minne kuoza

Wauguzi wawili wa Hospitali ya wilaya ya Manyoni mkoni Singida wamesimamishwa kazi,baada ya kumwachia mtoto wa miezi minne kamba kwa muda wa zaidi ya masaa nane ,ambayo waliifunga mkononi kwaajili ya kumwekea dripu ya maji na kusababisha mkono kuoza.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Manyoni Bwana Charles Fussi ametoa uamuzi huo baada ya kujirizisha kwa kukaa vikao na uongozi wa hospitali na wao wauguzi Bi.Salima Mkoka na Bi.Specioza Mchunguzi kukiri kusahau kutoa kamba hiyo na kusababisha mkono wa mtoto Cecilia Dastani kuharibika na unaweza kukatwa.

Wakieleza daktari ambapo tukio lilipotokea katika hospitali ya wilaya ya Manyoni Daktari Nelson Bukuu Mganga mkuu wa wilaya amekiri kuwa wauguzi wake wamesahau kwa bahati mbaya hadi siku ya pili,huku Mganga mkuu wa Hopitali ya St Gasper Itigi alipolazwa baada ya kupewa rufaa daktari Anatori Lukonge amesema mtoto Cecilia anaweza kupoteza baadhi ya vidole au kukatwa mkono.

Kwa upande wake mama mtoto Bi Violet Ernest mkazi wa Sasilo wilayani Manyoni amesema hakujua kwanini mtoto wake alikuwa akilia sana tokea awekewe dripu saa saba mchana mpaka siku ya pili asubuhi alipoambiwa daktari na kuja kutambua tatizo hilo .

Chanzo: ITV
 
Pamoja na uzembe wa wauguzi sikatai lakini huyo mama wa mtoto kama mtoto muda wote analia kweli huwezi kumuangalia mwanao maungoni kwanini analia tu!!?

Hakuweza hata kutoa taarifa kwa waauguzi kuwa mtoto toka awekewe drip analia tu muda wote!!?
 
Wauguzi kama hawa, unashika, peleka buchani, unamlipa mchinjaji 500 wanalazwa kwenye kile kigogo cha nyama mikono inakatiwa mabegani, (shoka, au kitu chochote chenye ncha kali), wanafungwa tambara wanawahishwa hospitali kwa matibabu
 
Nakumbuka Kuna mwaka Temeke hospital Kuna mtoto alipokelewa kutoka kituo kidogo cha Afya akiwa hoi alipofika Temeke akapewa huduma

Lakini kumbe huko alikotoka wasisahau kamba mkononi na Temeke hawakuiona, mtoto usiku akazidiwa akapelekwa Muhimbili.

Na huko Muhimbili wakagundua mtoto ana kamba mkononi na mkono umepata gangrene au kufa then Muhimbili wakaukata mkono wa mtoto na wale wauguzi na daktari wakasimamishwa kazi.

Katika kazi Kuna human mistake inatakoea Katika Fani yoyote ile iwe ya uhasibu,sheria, elimu,madini n.kk

Lakini kwa Huduma za binadamu makosa yake kiungo kinakatwa au roho inaacha mwili
 
Pamoja na uzembe wa wauguzi sikatai lakini huyo mama wa mtoto kama mtoto muda wote analia kweli huwezi kumuangalia mwanao maungoni kwanini analia tu!!?

Hakuweza hata kutoa taarifa kwa waauguzi kuwa mtoto toka awekewe drip analia tu muda wote!!?[/QUOT

mimi huyu mama ndo amenichosha mara 100 aic yaan hujiongez ht kidg jamani??dah wengin hawakufaa kwenda labor aic
 
Mashetani hao wapigwe chini kazi. Haya majinga yapo kila Hospital. Ukienda manesi wa kike wanamajibu ya kishenzi especially gvt hospitals. Mara mia ukutana nawaume kuliko majinga hayo.
 
Inasikitisha sana...

Kwani hiyo hospitali haina wauguzi wa kutosha? Mpaka kupelekea madaktari kusahau kufanya kazo zao...



Cc: mahondaw
 
Inasikitisha sana, hawa waliohusika na uzembe huu wachukuliwe hatua zaidi

Ili upumbavu wao usizidi kuenea
 
Pamoja na uzembe wa wauguzi sikatai lakini huyo mama wa mtoto kama mtoto muda wote analia kweli huwezi kumuangalia mwanao maungoni kwanini analia tu!!?

Hakuweza hata kutoa taarifa kwa waauguzi kuwa mtoto toka awekewe drip analia tu muda wote!!?
wangekuwa ni walimu hapo nadhani thread hii had sasa ingekuwa na comment 700,000 na kati ya hizo 699,999 yangekuwa ni matusi na kejeli za kutosha kwa walimu Lakin kwa vile ni wauguzi naona watu wana toa comment za upole kwa wanaona hata wao watauguana kuwarudia hao hao tena,laki.n mwalimu alisha kuvusha lasaba hata ukimtukana una hakika hukutani naye tena so hata ukimtusi poa tu.
samahan sijatoka nje ya mada!
POLE MTOTO MUNGU TENDA MUUJIZA WAKO MKONO HUO USIKATWE
 
Wauguzi kama hawa, unashika, peleka buchani, unamlipa mchinjaji 500 wanalazwa kwenye kile kigogo cha nyama mikono inakatiwa mabegani, (shoka, au kitu chochote chenye ncha kali), wanafungwa tambara wanawahishwa hospitali kwa matibabu
Nafikiri kilichotoa huu upuuzi ni matako

Shwain wahed
 
Pamoja na uzembe wa wauguzi sikatai lakini huyo mama wa mtoto kama mtoto muda wote analia kweli huwezi kumuangalia mwanao maungoni kwanini analia tu!!?

Hakuweza hata kutoa taarifa kwa waauguzi kuwa mtoto toka awekewe drip analia tu muda wote!!?
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom