ALOYCE MPANDANA
Senior Member
- Oct 1, 2010
- 172
- 58
TAMKO LA WAUGUZI KUHUSU HALI YA HUDUMA ZA AFYA MUHIMBILI KUFUATIA TOFAUTI KATI YA MADAKTARI NA WAFANYAKAZI WENGINE KATIKA SEKTA YA AFYA NA MWAJIRI
Chama cha Wauguzi Tanzania tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili, tunasikitika kwa hali inavyoendelea hadi hivi sasa hatuna taarifa ya kupatikana kwa muafaka kati ya watumishi sekta afya hususani madaktari na Mwajiri (Serikali), kutokana na hali iliyojitokeza bado tunazidi kusisitiza serikali kukaa meza moja na kuangalia kwa kina chimbuko la matatizo yaliyojitokeza ili kuyatafutia ufumbuzi kwa faida ya umma wa watanzania. Matatizo yapo yanajulikana yatafutiwe ufumbuzi haraka, pande zote mbili ziwe flexible katika kufanya maamuzi. ·
Wauguzi hufanya kazi na kada nyingine ikiwa ni pamoja na madaktari hivyo hatuwezi kutimiliza mahitaji ya wagonjwa sisi peke yetu, hali imezidi kuwa mbaya. · Kwa kuwa muuguzi ni mtumishi wa karibu sana na mgonjwa kuliko watumishi wengine wa afya tunaona wanavyoteseka, hali hii inatuumiza kisaikolojia na kimwili pia, wauguzi ndio wanaonekana wabaya na wameshaanza kutukanwa nawagonjwa na ndugu zao kwa kukosa huduma, wizara tumeiambia pia. ·
Hali ya huduma kiujumla imezidi kuzorota na itafika wakati hatutaweza kumudu majukumu yetu ya kazi na hatupendi tufike huko kwani tunajua madhara yake hivyo hatupo tayari kuona hali hii ikiendelea, · Katika mazungumzo yetu na wizara, tunashukuru kwa jitihada zinazochukuliwa na serikali.
Hata hivyo tumeona bado kuna matatizo kwa upande wa uuguzi wizarani, tunaiomba wizara kuunda kurugenzi ya uuguzi ifikapo Julai mwaka huu, hatujapendezwa na suala hili kuchukua muda mrefu pasipo sababu za msingi na tunasikitika kwamba hakuna jitihada za makusudi za kufanikisha kilio hiki cha wauguzi kwa muda wa hivi karibuni. Tunaiomba serikali kuzingatia ombi hili ili kurudisha imani kwa wauguzi.
haki za msingi za wauguzi ikiwa ni pamoja na uniform allowance wauguzi wapewe pesa zao na sio kuwashonea kutoka MSD. Pamoja na haya yapo mengi ambayo tumeongea na wizara tunasubiri kuona utekelezaji wake ni imani yetu kuwa wizara itayatekeleza kwa wakati muafaka. ·
· Tunaomba serikali iwasikilize wafanyakazi kwa ujumla wake katika sekta ya afya na kutafuta suluhu ya matatizo yaliyopo,
· Waziri mkuu atumie busara yake awafuate madakitari na awaite wizara ya afya wazungumuze na madakitari. e
· Tunawaomba wenzetu madaktari na watumishi wengine wakubali kukutana na ujumbe huo.
· Mh. Rais afany mabadiriko ya wizara ya afya · Katibu mkuu ateuliwe anayejua mambo ya afya
·
· Hivyo basi ifikapo Jumatatu tarehe 30 January 2012 bila ya kuwa na muafaka kuhusu tofauti na mvutano uliopo hivi sasa, basi nasi uwezo wetu wa kuvumilia hali hii ya sasa utakuwa umefikia wakati wa kukaa vikao endelevu. . · Chama kinawapongeza wauguzi hospitali ya taifa muhimbili kuendelea kutoa huduma na kinawasihi kuendelea na kazi hadi watakapokuwa wametangaziwa vinginevyo. …………………………
Paul Magesa Mwenyekiti Imetolewa na chama cha wauguzi Tawi la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Nakala; Waziri wa Afya – WAUJ Mkurugenzi Mtendaji – Hospitali ya Taifa Muhimbil Mkurugenzi – Kurugenzi ya Uuguzi na Ubora - Hospitali ya Taifa Muhimbili Mkuu wa Chuo - MUHAS Rais – Chama cha Wauguzi Tanzania Rais – Chama cha Madaktari Mameneja wa majengo – Hospitali ya Taifa Muhimbili
Chama cha Wauguzi Tanzania tawi la Hospitali ya Taifa Muhimbili, tunasikitika kwa hali inavyoendelea hadi hivi sasa hatuna taarifa ya kupatikana kwa muafaka kati ya watumishi sekta afya hususani madaktari na Mwajiri (Serikali), kutokana na hali iliyojitokeza bado tunazidi kusisitiza serikali kukaa meza moja na kuangalia kwa kina chimbuko la matatizo yaliyojitokeza ili kuyatafutia ufumbuzi kwa faida ya umma wa watanzania. Matatizo yapo yanajulikana yatafutiwe ufumbuzi haraka, pande zote mbili ziwe flexible katika kufanya maamuzi. ·
Wauguzi hufanya kazi na kada nyingine ikiwa ni pamoja na madaktari hivyo hatuwezi kutimiliza mahitaji ya wagonjwa sisi peke yetu, hali imezidi kuwa mbaya. · Kwa kuwa muuguzi ni mtumishi wa karibu sana na mgonjwa kuliko watumishi wengine wa afya tunaona wanavyoteseka, hali hii inatuumiza kisaikolojia na kimwili pia, wauguzi ndio wanaonekana wabaya na wameshaanza kutukanwa nawagonjwa na ndugu zao kwa kukosa huduma, wizara tumeiambia pia. ·
Hali ya huduma kiujumla imezidi kuzorota na itafika wakati hatutaweza kumudu majukumu yetu ya kazi na hatupendi tufike huko kwani tunajua madhara yake hivyo hatupo tayari kuona hali hii ikiendelea, · Katika mazungumzo yetu na wizara, tunashukuru kwa jitihada zinazochukuliwa na serikali.
Hata hivyo tumeona bado kuna matatizo kwa upande wa uuguzi wizarani, tunaiomba wizara kuunda kurugenzi ya uuguzi ifikapo Julai mwaka huu, hatujapendezwa na suala hili kuchukua muda mrefu pasipo sababu za msingi na tunasikitika kwamba hakuna jitihada za makusudi za kufanikisha kilio hiki cha wauguzi kwa muda wa hivi karibuni. Tunaiomba serikali kuzingatia ombi hili ili kurudisha imani kwa wauguzi.
haki za msingi za wauguzi ikiwa ni pamoja na uniform allowance wauguzi wapewe pesa zao na sio kuwashonea kutoka MSD. Pamoja na haya yapo mengi ambayo tumeongea na wizara tunasubiri kuona utekelezaji wake ni imani yetu kuwa wizara itayatekeleza kwa wakati muafaka. ·
· Tunaomba serikali iwasikilize wafanyakazi kwa ujumla wake katika sekta ya afya na kutafuta suluhu ya matatizo yaliyopo,
· Waziri mkuu atumie busara yake awafuate madakitari na awaite wizara ya afya wazungumuze na madakitari. e
· Tunawaomba wenzetu madaktari na watumishi wengine wakubali kukutana na ujumbe huo.
· Mh. Rais afany mabadiriko ya wizara ya afya · Katibu mkuu ateuliwe anayejua mambo ya afya
·
· Hivyo basi ifikapo Jumatatu tarehe 30 January 2012 bila ya kuwa na muafaka kuhusu tofauti na mvutano uliopo hivi sasa, basi nasi uwezo wetu wa kuvumilia hali hii ya sasa utakuwa umefikia wakati wa kukaa vikao endelevu. . · Chama kinawapongeza wauguzi hospitali ya taifa muhimbili kuendelea kutoa huduma na kinawasihi kuendelea na kazi hadi watakapokuwa wametangaziwa vinginevyo. …………………………
Paul Magesa Mwenyekiti Imetolewa na chama cha wauguzi Tawi la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Nakala; Waziri wa Afya – WAUJ Mkurugenzi Mtendaji – Hospitali ya Taifa Muhimbil Mkurugenzi – Kurugenzi ya Uuguzi na Ubora - Hospitali ya Taifa Muhimbili Mkuu wa Chuo - MUHAS Rais – Chama cha Wauguzi Tanzania Rais – Chama cha Madaktari Mameneja wa majengo – Hospitali ya Taifa Muhimbili