Watwala wanafaidika na udini na ukabila wetu!!!

dzed25

Member
Oct 10, 2010
26
2
Sijui kutawaliwa sana na wakoloni kumetufanya kutozingatia kukusanya jamii na kuwa kitu kimoja na badala yake kuzingatia kutawanya watu kutokana na misingi ya itikadi , jinsia,kabila,koo,rangi,na hasa dini.
Imekuwa ikifumbiwa macho na watawala kwa muda mrefu mambo haya yakiwagawa watu mfano:

  • AL huda:Ndani ya gazet hili wakati wa uchaguzi kuna mada zakusikisitisha sana, mfano siku moja wameandika mgombea wa chama fulani hapendi wanawake wa kiislamu.Haya mambo yameachwa na ndio yanayochangia kwa kiasi kikubwa yale yaliopewa jina la majeraha ya uchaguzi.Nataka kuuliza watawala wako wapi jamani kwani haba na haba hujaza kibaba..
  • Matamshi makali kwenye vyombo vya habari:Hili limejitokeza sana wakati uchaguzi wetu ukielekea mwishoni.Tulishuhudia viongozi mbalimbali wa makanisa na misikiti wakitoka mbele ya jamii kupitia vyombo vya habari wakitoa kauli ambazo kwa wengi zilionekana za kawaida lakini kwa mtu makini ilionyeesha kuna vita za ndani kwa ndani ambazo walikuwa wanapigana nazo.Hili pia limejitokeza kwenye vyombo vya habari mfano gazeti moja lilionyeasha idadi ya viongozi wa kikristo na waislamu.Huu ni mojawapo ya mpuzi ambao sikutegemea taifa langu lingekubali ufanyike
Hayo juu ni baadhi tu yapo mambo kadha wa kadha ambayo yamesaidia kukuza nyufa za ubaguzi na kusababisha kutawanywa kwa watanzania ambao baba wa taifa alipigana mchana na usiku kutuweka kuwa kitu kimoja.Kinachonisumbua sana ni juu ya kuachwa kwa mabo hayA yakitokea bila hata kukemea au kwa sababu vilikusaidia kukupa madaraka ?
Naomba watanzania tusikubali udhalimu wa aina hii uendelee kutugawa na kuacha tukilia na ujinga iliokubuhu, maradhi(hata malaria na kipindupindu ambayo yanatokana moja kwa moja na matatizo yao kama watawala) na UMASKINI wa kupindukia.
 
Ni kweli huu ni upuuzi mkubwa. Chanzo chake ni kutokuwa na viongozi wanaojali masilahi ya taifa. Wao wanajali kuingia madarakan kwa gharama zozote hata kama zitahatarisha amani ya taifa. Yote haya hatukuyaona huko nyuma ni kwa awamu hii dhaifu tu. Viongozi hasa wa dini wamekuwa ni sehemu ya siasa,lakini wamejengewa uhalali na viongozi ambao wamekuwa wakiomba wawasaidie kuingia madarakani.
Kuhusu vyombo vya habari, sikubaliani na matamshi yanayotolewa yenye lengo la kuligawa taifa. Lakini ni magazeti haya yanatumiwa na wanasiasa. Mfano Dr Slaa aliposhutumiwa ametumwa na maaskofu chama tawala chenye serikali hakikukemea bali kukaa kimya kwababu kuna maslahi yao yanalindwa. Mimi sioni tatizo kwa gazeti kuandika habari za chama kinachoungwa mkono na gazeti hilo, ili mradi waweke wazi wao wanamuunga mkono nani, hii inafanyika duniani kote. Kufanya kazi chini ya meza ndiko kuna zaa habari za kuligawa taifa.
Lakini pia huenda ni kupitia mijadala ya kipuuzi hata humu JF viongozi wamebaini njia ya makato ni kuingiza upuuzi huo katika siasa.
Unapokuwa na watu kama Ghandhi, Mandela, Nyerere ambao wao husimamia kile wanachoona ni kwa maslahi ya taifa upuuzi huu kamwe haujitokezi. Kwa ufupi chama lege lege huzaa serikali lege lege JK Nyerere
 
Back
Top Bottom