Watunzi wa maneno ya kiswahili wanakifanya kigumu

Rwaz

JF-Expert Member
May 3, 2013
1,958
3,307
Hoja yangu ni fupi. Tunaelewa bidii kubwa inafanyika kiswahili kijitosheleze kwa misamiat kadri dunia inavyozalisha vitu vipya. Lakin naona baraza la kiswahili wanatumia njia moja zaid ya kutohoa maneno toka mfano kiingereza na kuunda kiswahili chake. Matokeo yake tunapata misamiat migumu kias unataman kuendelea na kiingereza au lugha ya kigeni.

Nataman tutungiane maneno mafupi na yanatamkika kirahisi. Si lazma kunyambulisha neno kama vile inatafsiriwa sentensi. Bilinguals wananielewa bila mifano
 
Naunga mkono hoja, pia kuna tabia ya kutafuta maana ya Majina ya Vitu na Kutaka hiyo maana ndio iwe jina ka hiko kitu... ila ukichunguza majina ya vitu vingine miaka ya nyuma yaliachwa kama yalivyo kilichobadilika ni kukiandika kwa kiswahili... mfano Radio - Redio inakuwaje kwa Computer iwe Mashine Tanakirishi na Sio Kompyuta?
 
Tasnimu iliyotumika kudhanibu aduwai tasnifu imekinzana na mbinu angalizi za kutambua na kushamirisha lugha sanifu.
 
Naunga mkono hoja, pia kuna tabia ya kutafuta maana ya Majina ya Vitu na Kutaka hiyo maana ndio iwe jina ka hiko kitu... ila ukichunguza majina ya vitu vingine miaka ya nyuma yaliachwa kama yalivyo kilichobadilika ni kukiandika kwa kiswahili... mfano Radio - Redio inakuwaje kwa Computer iwe Mashine Tanakirishi na Sio Kompyuta?
Kompyuta, tarakilishi, tarakisibu, etc humaanisha computer. Lugha inakua na inapaswa iwe na maneno ya kutosha
 
Mi naona wataalam wetu wamewekeza akili za lugha kwenye kuhuisha neno la kigeni kuja lugha yetu. Kwani haiwezekan neno la kigen sisi tukaunda msamiat wetu ambao si kama unatafsiri?

Mf. Incubator tukaita tu zuchu. Sio kutafsiri tafsir ..kizalishio. Kama tunataka kiswahili kiongeleke hasa kwa maneno ya kisayansi, walau njia hiyo ya kuandika kwa kiswahili neno la kigeni itumike zaid. Mana hata kiswahili chetu kina maneno meng ni kiarabu.
 
Kompyuta, tarakilishi, tarakisibu, etc humaanisha computer. Lugha inakua na inapaswa iwe na maneno ya kutosha


Lugha inakua kwa kuazima maneno pia sio lazima kutafuta maneno mapya ikizingatiwa kwamba tayari kunakuwa na neno la kigeni lililoisha ota mizizi katika matumizi ya kawaida, mfano Computer (Kompyuta), Engine (Injini) nk,
 
Mi naona wataalam wetu wamewekeza akili za lugha kwenye kuhuisha neno la kigeni kuja lugha yetu. Kwani haiwezekan neno la kigen sisi tukaunda msamiat wetu ambao si kama unatafsiri? Mf. Incubator tukaita tu zuchu. Sio kutafsiri tafsir ..kizalishio. Kama tunataka kiswahili kiongeleke hasa kwa maneno ya kisayansi, walau njia hiyo ya kuandika kwa kiswahili neno la kigeni. Mana hata kiswahili chetu kina maneno meng ni kiarabu.
^zuchu^ naona huyu msanii kakukaa kwelikweli. Ila sasa unambandulia lebo hivo
 
Tasnimu iliyotumika kudhanibu aduwai tasnifu imekinzana na mbinu angalizi za kutambua na kushamirisha lugha sanifu.
We lugha yako imekomaa mno ukiitwa interview au kuwasilisha mada utaona wanatoka nje mmoja mmoja. Utadhan si kiswahili ni mkusanyiko wa virai [phrases] aisee.
 
WaTz ni hodari katika kufanya kila jambo liwe gumu, badala ya kurahisisha. Na kwa hii tabia, mambo yetu mengi hayavutii na hayasongi mbele.
 
WaTz ni hodari katika kufanya kila jambo liwe gumu, badala ya kurahisisha. Na kwa hii tabia, mambo yetu mengi hayavutii na hayasongi mbele.
Hiyo ni kweli kabisa, ni kama kukomoana hivi. Mfano mnaweza kubishana kuhusu kuijua hesabu badala mfu akupe zakuzidisha atataka usolve Matrix...

Lugha yetu hata kama tutataka itumike kufundishia tukiitumia ya Tuki ndio tutapotea kabisa maana katika mazingira yetu haipo kama tunavyofeli kwa kiingereza.

Huwa nnawaza hivi tukitumia hii lugha ya kiswahili tunayoitumia na kuelewana ikawekwa katika kufundishia ni nani atafeli kuelewa?

Mfano leo hii umtume mtu akuletee Kurunzi
Namimi nimtume mtu huyo akaniletee Tochi ni nani ataeleweka kwa haraka?

Kuna haja Bakita wakaacha Mbwembwe nyingi wakati wanakubali kuwa lugha inaweza kukopa maneno kama ilivyofanya kwa kiarabu, kijeruman, kiingereza nk.
 
Hiyo ni kweli kabisa, ni kama kukomoana hivi. Mfano mnaweza kubishana kuhusu kuijua hesabu badala mfu akupe zakuzidisha atataka usolve Matrix...

Lugha yetu hata kama tutataka itumike kufundishia tukiitumia ya Tuki ndio tutapotea kabisa maana katika mazingira yetu haipo kama tunavyofeli kwa kiingereza.

Huwa nnawaza hivi tukitumia hii lugha ya kiswahili tunayoitumia na kuelewana ikawekwa katika kufundishia ni nani atafeli kuelewa?

Mfano leo hii umtume mtu akuletee Kurunzi
Namimi nimtume mtu huyo akaniletee Tochi ni nani ataeleweka kwa haraka?

Kuna haja Bakita wakaacha Mbwembwe nyingi wakati wanakubali kuwa lugha inaweza kukopa maneno kama ilivyofanya kwa kiarabu, kijeruman, kiingereza nk.
Yan lugha ni yetu lakin ngumu kuliko ya kigeni. Wasisahau hata kiswahili tunajifunza wengine. Si lugha mama. Tuna za makabila wengine. Ndo maana ukisikiliza interview yoyote siku hizi hata kwa viongoz unataman kubadili channel mana hakuna mwenye uwezo wa kuongea lugha moja. Iwe mgen iwe mtangazaj. Wanaua lugha iliyofariki
 
Back
Top Bottom