Kichwa Ngumu
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 1,726
- 312
Wiki chache zilizopita tulisikia Wanachuo wa Mlimani wamegoma kuingia madarasani kwa sababu ya fedha wanayopewa meal na accomodation Tsh. 5,000/= haitoshi, sina shaka na hilo na pia naamini kuwa haitoshi kweli kwa sababu miaka miwili iliyopita nilikuwa pale na matatizo kama hayo yalinikuta.
Waligoma wakitaka hela hiyo iongezwe toka Tsh. 5,000 hadi 10,000
Nashindwa kuielewa serikali katika hili ilifikiria nini? Mwanachuo ambaye analipwa Tsh. 5000 ni kwa ajili yake yeye mwenyewe bila kujali kama anafamilia au hana na hata kama anayo serikali haitambui hilo; kwa mwanachuo kulipwa Tsh. 5000 kwa siku ni sawa na Tsh. 150,000.00 kwa mwezi kama ungekuwa ni mshahara tunaita TAKE HOME, wengine wanaita NET PAY.
NASHANGAZWA
Mtumishi wa Serikali ambaye Serikali inatambua kuwa anafamilia ya watu sita yaani yeye, mke/mme na watoto wanne analipwa kima cha chini cha Tsh. 135,000.00 (TGOS A) as gross pay ukitoa michango ya kijamii analipwa Tsh. sio zaidi 125,000.00 na huyo mtumishi anafanya kazi labda DSM ambapo ugumu wa maisha hauna tofauti kati ya mwanachuo na huyo mtumishi ambaye anafamilia ya watu sita.
Tena mwanachuo analipwa kwa ajili ya meal na accomodation tu lakini mtumishi ni kwa ajili ya matumizi yote ya binadamu, pia inaaminika mwanachuo anaweza kupata msaada kutoka kwa wazazi wake
NAAMINI
Mwaka ujao wa fedha Serikali itaongeza hela ya meal na accomodation kwa wanachuo ingawa inaweza isifike Tsh. 10,000.00
NAPENDEKEZA
Serikali imlipa Mwanachuo chini ya kima cha chini cha mshahara wa mtumishi yaani kama mwanachuo atalipwa Tsh. 7,500 kwa siku basi mtumishi alipwe Tsh. 12,500 kwa siku kama kima cha chini.
KAMA SERIKALI HAITA ZINGATIA PENDEKEZO LANGU NATABIRI
Waligoma wakitaka hela hiyo iongezwe toka Tsh. 5,000 hadi 10,000
Nashindwa kuielewa serikali katika hili ilifikiria nini? Mwanachuo ambaye analipwa Tsh. 5000 ni kwa ajili yake yeye mwenyewe bila kujali kama anafamilia au hana na hata kama anayo serikali haitambui hilo; kwa mwanachuo kulipwa Tsh. 5000 kwa siku ni sawa na Tsh. 150,000.00 kwa mwezi kama ungekuwa ni mshahara tunaita TAKE HOME, wengine wanaita NET PAY.
NASHANGAZWA
Mtumishi wa Serikali ambaye Serikali inatambua kuwa anafamilia ya watu sita yaani yeye, mke/mme na watoto wanne analipwa kima cha chini cha Tsh. 135,000.00 (TGOS A) as gross pay ukitoa michango ya kijamii analipwa Tsh. sio zaidi 125,000.00 na huyo mtumishi anafanya kazi labda DSM ambapo ugumu wa maisha hauna tofauti kati ya mwanachuo na huyo mtumishi ambaye anafamilia ya watu sita.
Tena mwanachuo analipwa kwa ajili ya meal na accomodation tu lakini mtumishi ni kwa ajili ya matumizi yote ya binadamu, pia inaaminika mwanachuo anaweza kupata msaada kutoka kwa wazazi wake
NAAMINI
Mwaka ujao wa fedha Serikali itaongeza hela ya meal na accomodation kwa wanachuo ingawa inaweza isifike Tsh. 10,000.00
NAPENDEKEZA
Serikali imlipa Mwanachuo chini ya kima cha chini cha mshahara wa mtumishi yaani kama mwanachuo atalipwa Tsh. 7,500 kwa siku basi mtumishi alipwe Tsh. 12,500 kwa siku kama kima cha chini.
KAMA SERIKALI HAITA ZINGATIA PENDEKEZO LANGU NATABIRI
- Kutajitokeza mgomo wa wafanyakazi nchi nzima na utaivuruga serikali
- Kwa sasa molali ya wafanyakazi imeshuka na itazidi kushuka zaidi hivyo kazi zitafanyika bila kuwa na tija (mafanikio) uzembe mdogo mdogo ambao utasababisha majanga makubwa kama ya Gongo la Mboto utaongezeka na Serikali itatumia fedha nyingi kuurekebisha.
- Ufisadi mdogo mdogo maofisini kwa kila mfanyakazi utaongezeka ambao ukijumuishwa mfanyakazi na mfanyakazi utaleta hasara kubwa kwa Serikali