beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,877
- 6,326
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ameagiza Watumishi wa Halmashauri ambao wametakiwa kuhamia makazi mapya na hawajafanya hivyo kuondoka mara moja.
Amesema "Kipindi cha kuondoka kilishatamkwa na Rais kwahiyo hatuna sababu ya kuwapa muda tena. Endapo hawatafanya hivyo, Mkuu wa Mkoa husika achukue hatua mara moja dhidi ya Watumishi hao".
Kauli ya Majaliwa inakuja baada ya Mbunge Joseph Kasheku kuhoji kauli ya Serikali kuhusu Halmashauri ambazo zimehamisha Ofisi Vijijini lakini Watumishi bado wanarudi kulala Mjini hata kama walipohamia kuna nyumba, hali inayoleta mzigo wa kugharamia mafuta kila siku.
Amesema, Novemba 2019 Rais Magufuli aliagiza Halmashauri za Vijijini zinazokaa Mjini kurejea maeneo husika ndani ya siku 30 ili kuhudumia Wananchi kwa karibu.
Amesema "Kipindi cha kuondoka kilishatamkwa na Rais kwahiyo hatuna sababu ya kuwapa muda tena. Endapo hawatafanya hivyo, Mkuu wa Mkoa husika achukue hatua mara moja dhidi ya Watumishi hao".
Kauli ya Majaliwa inakuja baada ya Mbunge Joseph Kasheku kuhoji kauli ya Serikali kuhusu Halmashauri ambazo zimehamisha Ofisi Vijijini lakini Watumishi bado wanarudi kulala Mjini hata kama walipohamia kuna nyumba, hali inayoleta mzigo wa kugharamia mafuta kila siku.
Amesema, Novemba 2019 Rais Magufuli aliagiza Halmashauri za Vijijini zinazokaa Mjini kurejea maeneo husika ndani ya siku 30 ili kuhudumia Wananchi kwa karibu.