Watumishi majizi na wazembe Sekta ya Afya ndiyo wanaoongoza kumpinga Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima

COARTEM

JF-Expert Member
Nov 26, 2013
3,598
3,644
Mahospitalini Kuna ubadhirifu wa fedha za umma kupitia WIZI wa MADAWA, kuchukua rushwa kwa Wagonjwa, kufanya uharibifu wa makusudi wa vifaa tiba ili visiwe vinafanya kazi na kisha wagonjwa waelekezwe hospitali binafsi za watumishi hao.

Nani asiyejua namna watumishi wa Afya (madaktari na manesi) wanavyoiibia serikali pesa kwa kuchukuwa pesa kwa wagonjwa. Mnachukua pesa kwa wagonjwa, risiti hamtoi zinaingia mifukoni mwenu halafu mnakuja piga kelele kuwa hospitali haina dawa na vitendanishi ili hali pesa ambazo hospitali ingezitumia kununulia vitu hivyo imeingia mifukoni mwenu? Anachokifanya Dr Dorothy Gwajima ni kuwafumbua macho wananchi, kurudisha uwajibikaji kwa watumishi wa sekta ya umma ya Afya.

Wananchi mnayotendewa Hospitali za serikali siyo mnayotendewa Hospitali binafsi. Daktari ukimkuta Hospitali ya serikali huwa hana Good customer care, lakini daktari huyo huyo mkute Private hospital hutaamini kwa ukarimu atakao kuonyesha.

Kiufupi viongozi MAHOSPITALINI huandaa taarifa nyingi za uongo anapokuja waziri husika. Sasa kumdanganya huyu waziri wa sasa lazima uwe na PhD ya uongo.

Nani asiyejua kuwa madaktari Bingwa wengi ikifika saa nne asubuhi wanaondoka kwenye hospitali za serikali wanakolipwa mishahara na wamakwenda kufanya kazi kwenye hospitali binafsi ndani ya muda wa kazi wa serikali? Kwanini waziri akiwabana mnaanza kulialia?
Hivi ni mwananchi gani asiyefahamu lugha za karaha kutoka kwa wahudumu wa Afya? Hilo nalo waziri anapolikemea mnasema anawasuta?

Vifo vingapi vinasababishwa na uzembe wa watoa huduma mahospitalini? Waziri anapotoa ujumbe kuwa madaktari wapite ward rounds zote inavyotakiwa kwanini mnanuna?

Nenda mahospitalini kipindi hiki mambo yameanza kubadilika kabisa kisa kumhofia Mheshimiwa waziri.

Ukweli ndiyo huo
 
Hizo swaga namuonaga mama mwingine wa baraza moja la kitaaluma huwa anazo sana. Sidhani kama ni rahisi kuwabadilisha ila tu kama wako kwenye haki acha wafanye tu, ndio kina mama wetu wa kiafrika. Hawaja ji edit, wako kihalisia, hawafeki mannerism zao.

Mungu awape hekima tu wasionee wala kunyanyasa mtu asiye na hatia
 
Huwezi iba dawa za GOT kibiashara. Ukiona mtumishi kaiba ujue kaiba dozi moja au mbili akatumie au ampe mshkaji wake.

Je, unakumbuka mwezi mmoja uliopita mh waziri alikuwa anagombana na msd kwakuwa hawapeleki dawa hospitalini.

Je, unajua wajawazito, watoto na wazee ndio kundi kubwa la wagonjwa ktk Hosp za serikali na wanatibiwa bure.

Je, unajua mchakato wa manunuzi ulivyo mrefu kiasi kwamba kuhakikisha upatikanaji wa dawa kwa mwaka mzima ni ngumu sana.

Mwisho, tatizo la dawa nchini ni pana zaidi ya wanasiasa wanavyotuaminisha. Kwanini hawatukamatii hawa wezi?
 
Sehemu anapolipwa mshahara mara mbili kwanini asiwe mkarimu

Serikali inakupa ela kidogo bado ikunyime promotion na bado haupandi daraja unategemea nn kama mtu hataamua kuuza tu dawa

Tutaelewana
 
Changamoto ktk sekta ya afya na elimu nchini haziwezi kutatuliwa kisiasa. Lazima zitatuliwe kitaalamu na kiweledi wa hali ya juu.
Ila wanasiasa wameshajua wananchi wanataka amsha amsha na wanawapa mnachotaka na wao wanapiga kivyao na hutawaona wanatibiwa serikalini au watoto wao wakisoma serikalini
 
Huwezi kuiba kibiashara? Je, kama mtu kaiba hizo dozi mbili tatu kaenda kuweka kwenye 'pharmacy' hiyo tunaiitaje? Naona unajaribu kutetea lakini utetezi wako umekosa nyama hivyo kuufanya unapwaya.

Naamini hospitali kuna mifumo ya kutunza kumbukumbu za dawa wanazopokea na zile wanazotoa, ukilinganisha takwimu ya hivyo na ukaona havilingani hapo hatuwezi kusema kuna wizi wa dawa.

Tumpongeze Mama kwa kujitahidi kulisema hilo tatizo hata kama halitadhibitika lakini kulisema tu inatosha kuelezea ujasiri wake na umuhimu wake kwenye hiyo wizara
 
Huwezi kuiba kibiashara? Je, kama mtu kaiba hizo dozi mbili tatu kaenda kuweka kwenye 'pharmacy' hiyo tunaiitaje? Naona unajaribu kutetea lakini utetezi wako umekosa nyama hivyo kuufanya unapwaya....
Zunguka famasi zote mjini kanunue dawa kama utapata ya GOT, hakuna mfanyabiashara mjinga anaweza uza dawa za GOT. Na ndio maana husikii serikali ikisema imekamata dawa zake zikiuzwa sehemu fulani.

Na kama unafuatilia kwa makini utagundua hizi kelele za wizi wa dawa hakuna mtu anakamatwa na bado hakuna dawa hospitalini. Nimekwambia swala la dawa hospitalini ni pana zaidi ya ngonjera za kuwa watumishi wanaiba
 
Huwezi kuiba kibiashara? Je, kama mtu kaiba hizo dozi mbili tatu kaenda kuweka kwenye 'pharmacy' hiyo tunaiitaje? Naona unajaribu kutetea lakini utetezi wako umekosa nyama hivyo kuufanya unapwaya...
Be informed kwamba dawa za serikali zina chapa ya GOT, Tena sio kwenye makasha tu bali mpaka kidonge chenyewe waweza kuta neno GOT.

Najua wawezapenda waziri anavyopambana, pia Mimi napenda wapambanaji ila tupambane kwa kuzingatia ukweli na tija.
Kama wezi wapo wakamatwe, washtakiwe tusonge mbele, ila kupiga kelele kila siku tunaibiwa halafu hatupewi mwizi!!!!!!!!!
 
Be informed kwamba dawa za serikali zina chapa ya GOT, Tena sio kwenye makasha tu bali mpaka kidonge chenyewe waweza kuta neno GOT
Najua wawezapenda waziri anavyopambana, pia Mimi napenda wapambanaji ila tupambane kwa kuzingatia ukweli na tija.
Kama wezi wapo wakamatwe, washtakiwe tusonge mbele, ila kupiga kelele kila siku tunaibiwa halafu hatupewi mwizi!!!!!!!!!
Ninachojua wizi ndani ya taasisi nao ni mfumo ndani ya taasisi, kuna watu wanaoratibu huo mfumo mpaka unakamilika. Hizo dawa kama zinakuja na chapa ya GOT maana yake zinakuja kwa idadi maalumu , na utokaji wake hauna budi kutoka kama zilivyokuja. Inapoonekana zimetoka chache na zilikuja nyingi na hakuna kilichobaki stock hapo ndio tunasema wizi umefanyika. Au siyo?

Hivyo siamini katika wizi wa namna hii wakubwa hawawezi kuhusika na kama hawahusiki basi ni wazembe wameshindwa kufatilia matumizi ya dawa hizo mpaka zinaondoka.

Mama anapofanya hayo anajaribu kulitatua tatizo hilo kwa busara na hekima kubwa, bila hivyo utumbuaji utakuwa mkubwa sana. Tushukuru wizara imepata anayelionya kabla ya kuchukua hatua.
 
Mijizi imeguswa upande huo sahv wanaliaaa
Kuna watu walikuwa wanapiga sana upande wa madawa mamaeee sahv anawanyoosha
Maana wazir anaijua sekta ya afya vilivyoo
Huyo syo ummy ohooooo

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom