Baadhi ya viongozi wa juu wa CCM kwa kutoelewa au kwa makusudi na chuki binafsi waliendesha zengwe la kuwashambulia na kuwabatiza wenzao Mapacha watatu na kuwafanya kuonekana kama ndio wamefanya CCM kupoteza mvuto kwa wananchi. Viongozi wanaoipotezea mvuto CCM ni hawa wafuatao;
Ni lazima CCM kama wanataka kurejesha mvuto wake wa kukubalika kwa wananchi ni lazima serikali yake iweke mfumo utakaoboresha utoaji huduma mzuri kwa watanzania. Sio dhana ya kujivua gamba.
- Watendaji wa vijijini na kata ,mahakimu wa mwanzo, waganga na manesi wa zahanati, walimu wa shule za msingi na sekondari wasotimiza wajibu wao kwa haki, kwa wakati na bila choyo, chuki, upendeleo na kupenda rushwa. Hawa ndio huhudumia kundi kubwa la watanzania.
- Idara mbalimbali za serikali zinazotoa huduma kwa wananchi kama TRA, Shirika la Reli, watumishi wa hospitali za wilaya na mikoa, mahakama nchini, Bandari, watumishi wa Halmashauri za serikali za mitaa, polisi, magereza n.k
Ni lazima CCM kama wanataka kurejesha mvuto wake wa kukubalika kwa wananchi ni lazima serikali yake iweke mfumo utakaoboresha utoaji huduma mzuri kwa watanzania. Sio dhana ya kujivua gamba.