#COVID19 Watumishi 9 wa Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 Uwanja wa JNIA Nyerere wasimamishwa kazi kwa kutofika kazini

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,545

Watumishi tisa wa Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA) wamesimamishwa kazi kwa kosa la kutokufika kazini kutoa huduma ya vipimo hivyo kwa wasafiri bila taarifa.

"Imeonekana hapa hili zoezi la baadhi ya watumishi kutokuja kazini limekuwepo, sasa hii imenisikitisha sana kwa baadhi ya viongozi kushindwa kuchukua hatua zinazostahili na kulindana kwa kuficha uozo"

Ni kauli ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi baada ya kuwasimamisha kazi Watumishi tisa wa afya katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa juzi alipofika katika uwanja huo akiwa ameambatana na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi.

Sambamba na hilo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi amewataka Watumishi wanaotoa huduma za Afya hususan katika maeneo ya mipaka ya nchi kavu, maji na ardhi kufanya kazi yao kwa uzalendo na kwa budii ili kuitunza taswira nzuri ya nchi.

Prof. Makubi amesisitiza hilo alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa juzi alipofika katika uwanja huo akiwa ameambatana na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi.
 
Watumishi tisa wamesimamishwa kazi katika Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).
Agizo hilo limetolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi alipofanya ziara uwanjani hapo.
 
Watumishi tisa wamesimamishwa kazi katika Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).
Agizo hilo limetolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi alipofanya ziara uwanjani hapo.
... huyu profesa kipindi cha mwendazake alikana katakata kuwepo kwa Covid-19 nchini. Je, Covid-19 imeingia Tz baada ya Machi 17? Hebu atujuze kwanza.
 
Watumishi tisa wamesimamishwa kazi katika Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).

Agizo hilo limetolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Abel Makubi alipofanya ziara uwanjani hapo kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa juzi alipofika hapo akiwa ameambatana na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi.

Prof. Makubi amesema hakufurahishwa na kitendo cha utovu wa nidhamu, kilichofanywa na watumishi cha kutokufika kazini bila kutoa taarifa rasmi kwa uongozi hapo jana na leo.

"Jana watumishi wanane hawakufika na leo mmoja bila kutoa sababu ya msingi, jumla wanakuwa tisa," amebainisha.

Ameongeza "Imeonekana hapa hili zoezi la baadhi ya watumishi kutokuja kazini limekuwepo, sasa hii imenisikitisha sana kwa baadhi ya viongozi kushindwa kuchukua hatua zinazostahili na kulindana kwa kuficha uozo.

"Kwa hiyo hawa ambao hawakufika jana ambao jumla walikuwa wanane na kati yao wanne walikuwa wameajiriwa na Wizara ya Afya na wanne wameajiriwa na Manispaa ya Dar es Salaam, wapo chini ya RAS wa Dar es Salaam.

"Nimeagiza hawa walio chini ya Wizara ya Afya wasimame kufanya kazi ili tufanye uchunguzi na kuchukua hatua stahiki.

"Huu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu ambapo mtumishi anaamua kuacha kuja kazini na kusababisha usumbufu kwa wenzake na abiria ambao wanakuja hapa kwa sababu yeye 'gap yake haijawa covered' na mtu yeyote," amesisitiza.

Prof. Makubi ameongeza "Lakini vile vile ambao wameajiriwa na Ofisi ya RAS nitashauri mamlaka husika nao wachukuliwe hatua hivyo hivyo ambazo zimechukuliwa kwa hawa wa Wizara.

Amesema Serikali haiwezi kuvumilia watumishi wasio na nidhamu na wanaodharau majukumu wanayopewa.

"Hizo ndizo hatua ambazo tumechukua, lakini pia tutahakikisha tutaleta wengine 'ku-replace' hao tisa waweze kuendelea ili tusije tukaathiri hizi shughuli za upimaji hapa 'airport'," amesema.

Ametoa onyo kwa watumishi wa afya nchini, wawe tayari kufanya kazi popote pale watakapopangiwa.

"Waende wakafanye kazi siyo kwamba ukipelekwa upande mmoja unaamua kususia kama hawa ambavyo waliamua ni kwa sababu walihamishwa kutoka kwenye vituo vyao vya awali wameletwa huku.

Amewataka watumishi wote wa afya kutanguliza uzalendo wa hali ya juu katika utendaji wa kazi zao na kwa kujituma.

"Hapa tunapofanya upimaji, ni upimaji unawakilisha sura ya Nchi yetu. Kwa hiyo mtu yeyote anayeletwa hapa maana yake ndiye anayetoa taswira ya nchi yetu kwa ujumla.

"Anavyohudumia wasafiri, customer care yake na yeye mwenyewe kujibidiisha wanapofika hapa. Niwaombe watumishi ni vizuri watangulize uzalendo katika kazi zao lakini pia kuwajibika kwa kile walichopangiwa kwa kujitoa ili kuepusha malalamiko kwa wananchi.

"Najua watumishi wengi wanaojituma ila kwa hawa wachache niwaombe wazingatie uzalendo, uwajibika na 'customer care' nzuri wanapohudumia wananchi," ameagiza.

Awali, Prof. Makubi amesema maelekezo waliyoyatoa na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi yametekelezwa ikiwamo la kuongeza watumishi katika eneo la upimaji.

"Nimefarijika kuna maboresho zaidi yamefanyika, hasa hasa kuongeza sehemu za kupima lakini pia maeneo ambayo abiria wanaweza kuwa wanapimwa.

"Nimeona wameongeza upande mmoja ambao abiria watakuwa wanaingia wakifuata mstari na pia kwa umbali wa mita moja moja kwa kuachana.

"Lakini pia upande wa kushoto na kwenyewe nimekuta kumeongezwa maeneo ambayo watakuwa wanaingia na kupimwa na kuna watumishi 20 tumeongeza kama tulivyokuwa tumeongea siku zile," amesema.

Amesema watumishi hao wameongezeka kulingana na ongezeko la abiria.

"Kwa sababu mwanzoni abiria walikuwa wachache sasa hivi wamekuwa wengi, kwa hiyo kama Wizara tumeweza kuhakikisha kwamba ile changamoto waliyokuwa nayo ya watumishi ili waweze kuendana na abiria imeweza kutekelezwa, wameshafika na wamefanyiwa 'orientation' ili waweze kufanya kazi na wenzao" amesema.








 
Si hamtaki kuwalipa watumishi mshahara stahiki eti wajiongeze kwenye ujasiriamali, sasa hao walijipa likizo kwenda angalau kukagua namna biashara zao zinavyoenda, mnawafukuza kazi......hii haiwezi kuwa haki kwa watumishi wanaojiongeza ili kukidhi mahitaji, TUCTA itabidi waliangalie hili...
 
Watumishi tisa wamesimamishwa kazi katika Kitengo cha upimaji wa COVID - 19 kwa wasafiri katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere (JNIA).

Agizo hilo limetolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Prof. Abel Makubi alipofanya ziara uwanjani hapo kukagua utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa juzi alipofika hapo akiwa ameambatana na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi.

Prof. Makubi amesema hakufurahishwa na kitendo cha utovu wa nidhamu, kilichofanywa na watumishi cha kutokufika kazini bila kutoa taarifa rasmi kwa uongozi hapo jana na leo.

"Jana watumishi wanane hawakufika na leo mmoja bila kutoa sababu ya msingi, jumla wanakuwa tisa," amebainisha.

Ameongeza "Imeonekana hapa hili zoezi la baadhi ya watumishi kutokuja kazini limekuwepo, sasa hii imenisikitisha sana kwa baadhi ya viongozi kushindwa kuchukua hatua zinazostahili na kulindana kwa kuficha uozo.

"Kwa hiyo hawa ambao hawakufika jana ambao jumla walikuwa wanane na kati yao wanne walikuwa wameajiriwa na Wizara ya Afya na wanne wameajiriwa na Manispaa ya Dar es Salaam, wapo chini ya RAS wa Dar es Salaam.

"Nimeagiza hawa walio chini ya Wizara ya Afya wasimame kufanya kazi ili tufanye uchunguzi na kuchukua hatua stahiki.

"Huu ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu ambapo mtumishi anaamua kuacha kuja kazini na kusababisha usumbufu kwa wenzake na abiria ambao wanakuja hapa kwa sababu yeye 'gap yake haijawa covered' na mtu yeyote," amesisitiza.

Prof. Makubi ameongeza "Lakini vile vile ambao wameajiriwa na Ofisi ya RAS nitashauri mamlaka husika nao wachukuliwe hatua hivyo hivyo ambazo zimechukuliwa kwa hawa wa Wizara.

Amesema Serikali haiwezi kuvumilia watumishi wasio na nidhamu na wanaodharau majukumu wanayopewa.

"Hizo ndizo hatua ambazo tumechukua, lakini pia tutahakikisha tutaleta wengine 'ku-replace' hao tisa waweze kuendelea ili tusije tukaathiri hizi shughuli za upimaji hapa 'airport'," amesema.

Ametoa onyo kwa watumishi wa afya nchini, wawe tayari kufanya kazi popote pale watakapopangiwa.

"Waende wakafanye kazi siyo kwamba ukipelekwa upande mmoja unaamua kususia kama hawa ambavyo waliamua ni kwa sababu walihamishwa kutoka kwenye vituo vyao vya awali wameletwa huku.

Amewataka watumishi wote wa afya kutanguliza uzalendo wa hali ya juu katika utendaji wa kazi zao na kwa kujituma.

"Hapa tunapofanya upimaji, ni upimaji unawakilisha sura ya Nchi yetu. Kwa hiyo mtu yeyote anayeletwa hapa maana yake ndiye anayetoa taswira ya nchi yetu kwa ujumla.

"Anavyohudumia wasafiri, customer care yake na yeye mwenyewe kujibidiisha wanapofika hapa. Niwaombe watumishi ni vizuri watangulize uzalendo katika kazi zao lakini pia kuwajibika kwa kile walichopangiwa kwa kujitoa ili kuepusha malalamiko kwa wananchi.

"Najua watumishi wengi wanaojituma ila kwa hawa wachache niwaombe wazingatie uzalendo, uwajibika na 'customer care' nzuri wanapohudumia wananchi," ameagiza.

Awali, Prof. Makubi amesema maelekezo waliyoyatoa na Katibu mwenzake wa Wizara ya Uchukuzi yametekelezwa ikiwamo la kuongeza watumishi katika eneo la upimaji.

"Nimefarijika kuna maboresho zaidi yamefanyika, hasa hasa kuongeza sehemu za kupima lakini pia maeneo ambayo abiria wanaweza kuwa wanapimwa.

"Nimeona wameongeza upande mmoja ambao abiria watakuwa wanaingia wakifuata mstari na pia kwa umbali wa mita moja moja kwa kuachana.

"Lakini pia upande wa kushoto na kwenyewe nimekuta kumeongezwa maeneo ambayo watakuwa wanaingia na kupimwa na kuna watumishi 20 tumeongeza kama tulivyokuwa tumeongea siku zile," amesema.

Amesema watumishi hao wameongezeka kulingana na ongezeko la abiria.

"Kwa sababu mwanzoni abiria walikuwa wachache sasa hivi wamekuwa wengi, kwa hiyo kama Wizara tumeweza kuhakikisha kwamba ile changamoto waliyokuwa nayo ya watumishi ili waweze kuendana na abiria imeweza kutekelezwa, wameshafika na wamefanyiwa 'orientation' ili waweze kufanya kazi na wenzao" amesema.









Hivi Tanzania tunafuata taratibu za WHO? Kwa nini abiria ambae anawasili Tanzania, akiwa amepimwa huko alikotoka, na ana certificate ya kuonyesha yuko negative, na certificate iko valid, ndani ya saa 96; bado analazimishwa kupimwa akifika JNIA? Mbona tukisafiri nchi nyingine, kwa kutumia certificate za kutoka Tanzania, zilizotolewa na National Public Health Laboratory, huwa hatupimwi tena huko nje? Ina maana Tanzania haiamini certificate zinazotolewa huko nje?
 
Wameondolewa wawekwe wanaotakiwa na wao...

Mabadiliko...

Tisa...wasije wote?!
 
We unatoka Geita unaishia Chato utajuaje mambo ya watu wanaosafiri kwenda nchi za watu? We kula mapapai tafuna karanga ukalale mengine tuachie wa mjini.
Bila kusahau miogo mibichi,maana watu Wa huko kazi yaoni kufyatuana2.

Tena hapo gheita korona IPO sana tu.
 
Hata katika mahospital watumishi wana hangaika na wagonjwa was aina hiyo lakin hata motisha tu hakuna wakati wanahatarisha maisha yao kila siku lakin hill hawajali.serikali ijiulize hapo si bure.
 
Hivi Tanzania tunafuata taratibu za WHO? Kwa nini abiria ambae anawasili Tanzania, akiwa amepimwa huko alikotoka, na ana certificate ya kuonyesha yuko negative, na certificate iko valid, ndani ya saa 96; bado analazimishwa kupimwa akifika JNIA? Mbona tukisafiri nchi nyingine, kwa kutumia certificate za kutoka Tanzania, zilizotolewa na National Public Health Laboratory, huwa hatupimwi tena huko nje? Ina maana Tanzania haiamini certificate zinazotolewa huko nje?
Hili swala ni la kuangalia kwa kina sana. Point muhimu sana hii Maana haiwezekani mtu ana kila kielelezo bado akalipishwa anapowasili huo ni uharamu
 
Back
Top Bottom